Kwanini Ndege(Roketi/Contrail) huacha mstari wa Moshi Mweupe?

Kwanini Ndege(Roketi/Contrail) huacha mstari wa Moshi Mweupe?

Kuna muda angani inapita rocket au ndege(sina uhakika kama ni plane)
Inakuwa inatoa moshi mwingi unaotengeneza kama njia ivi,
unakuta hata hiyo ndege yenyewe imeshapita na haionekani tena lakini ule moshi unabakia umechora njia,
Sasa wakuu hivi kile ni chombo gani?
Manake najiuliza katika karne hii wameshindwa kweli kubuni chombo kisichotoa moshi namna ile au ule moshi unaotoka unamaanisha nini?
Hebu mwenye Ufahamu atudadavulie ili tukifahamu zaidi,
Umenikumbusha mambo ya utotoni.

Ni hivi, zile ni ndege kama ndege nyingine tofauti yake ni kwamba zenyewe ni ndege kubwa ambazo zinaruka kwenye anga ya juu sana ambapo nyuzijoto zinakuwa hadi zaidi hasi ishirini (-2). Kwa hiyo moshi wa injini ya ndege unapotoka tu unaganda maramoja na ndiyo maana sisi huona kitu kama mstari. Kifupi ni hivyo
 
Siyo lazima mtu akiwa angani
afungue dirisha la ndege kujua hali ya joto iliyopo nje kwani vipimo vya ndani ya ndege vinatoa taarifa ya hali ya hewa iliyopo nje ya ndege kwa waliopo ndani ya ndege.

Ndiyo maana Enzi za Mwalimu wakati watanzania wengi walikuwa hawana fursa ya kusafiri kwenda Ng'ambo yeye alikuwa akienda na kurudi afu anaanza kupiga stori wakati wa kutoa hutuba zake hadhira ikawa inaona ni mambo ya ajabu sana.
 
Huo Moshi kwa ufupi unaitwa MPEMBA EFFECT.
Erasto Mpemba alikuwa akichemsha maziwa na anaingiza kwenye friji wakati akiwa shule. Wenzake waliweka bila kuchemsha. Ila maajabu yalikuwa kwamba maziwa yake yaliganda mapema kuliko ya wenzake.

Alipomuambia Mwalimu alimuona kichaa kwani kwa sheria za Fizikia ni yale ya baridi yalitakiwa kuganda mapema kwa formula iitwayo q=mct (hii usiniulize kwa Kiswahili maana siwezi kuilezea)
Baada ya utafiti hapo UDSM na nchi za nje, waliamua kumuenzi Mtanzania huyo kwa kuipa hiyo kitu Mpemba Effect.

Kwa maana hiyohiyo, moshi/hewa na maji yanayotoka kwenye ndege ikiwa juu, yanaganda haraka sana na kutengeneza barafu ambayo unaiona. Baada ya muda huchanganyika au kulingana na eneo jingine na kupotea.
Ukiweza angalia hii video chini:



Mkuu Mwamba028, swali lako kwa nini ndege zinapita juu sana ni kwa sababu wanataka kuchoma mafuta kidogo kwa safari za mbali. Tuseme kama ndege ya KLM inapotoka asubuhi Schiphol Airport na kufika usiku Kilimanjaro na huwa angani kama masaa 10. Ili kupunguza utumiaji wa mafuta basi ndege huenda 10 km juu ya usawa wa bahari. Huko ndiyo huanza safari kwa speed ya 1000km/hr. Faida ya kuwa huko juu sana ni kwamba kwanza Gravitation (Msukumo uliopo kwenye sayari ya dunia kuvuta vitu kwenye uso wake) ni kubwa na matokeo yake kuishikilia ndege angani inahitaji mafuta mengi uchome. Ukiwa 10km angani, gravitation inapungua na unaokoa mafuta.

Pia upepo mkali uliopo ardhini huko juu unapungua hivyo ndege inateleza taratibu bila msuguano mkali na ardhi. Ila wanaweka hapo na si juu zaidi kwa sababu mambo ya hewa na Pressure wakipandisha ndege juu zaidi inakuwa shida.
Kama unakumbuka yule jamaa wa Baloon la Red Bull, aliruka hadi akawa amekaribia umbali huo bila kuwa na mitungi ya hewa ya Oxygen.

Mapanga Boy yanahitaji Msuguano na hewa ili yaendelee kuishika ndege angani na kusonga mbele. Hivyo huwa zinakuwa hazipai angani sana. Kama sikosei hata zetu zitakuwa zinakwenda kwenye speed hiyo ya 700km/hr na urefu kama 7km kutoka usawa wa bahari,

Wadau hamujaniambia kwann hizi ndege huwa zinapita juu sana kuliko ndege zingine

Nataka ninunue moja
 
mm nazani kwa elimu yangu ya hapa na pale yaani ya kubahatisha kule juu kuna vumbi sana linalotimuliwa na hizo jets zenu
 
This needs the very cold, very dry air at higher altitudes between 6000m and 12000m. These trails can form condensation cores for humidity already present, so the trail grows over time and stays in place for hours. They are called condensation trails or "contrails

Most aircraft that leave trails aren't leaving smoke. It's condensed water vapour; essentially, clouds. These are called contrails. This can be caused by the water in the engine exhaust condensing, or by the disruption of the air by the passage of the aircraft triggering the condensation of water that was already present.

Natumai itasaidia kidogo.. kwa hiyo ile kitu siyo moshi
To add on FAZA1980, due to the combustion of the engine some aerosols are produced and discarded through the engine exhaust. These aerosols act as condensation nuclei - since the moist air above is at a supercooled level but lack condensation nuclei to form clouds; the moment the exhaust air is released into the atmosphere it supplies that needed nuclei hence instant cloud formation that lags the moving plane.
 
Inavyoeleweka huku angani kuna upepo wenye kasi kubwa (marekebisho kama siko sahihi).

Mara nyingi nimeona zile ndege zinazopita juu sana zamani tukiziita 'roketi' zinaacha mstari mweupe wa moshi na mstari huu unachukua muda kupotea/kutawanyika unaweza kuchukua hata dakika 10 au zaidi.

Je, kwa nini hali hiyo inatokea au inawezekana kuwa si kweli kuna upepo mkali huko angani?
Kwa ndege na rocketi principle ni ile ile. nyuma ya engine kuna exhaust system ambayo hutoa compressed air ambayo ni ya joto kali sana. Joto hili linatoka kwenye mazingira ambayo temprature pamoja na pressure ziko chini sana na matokeo yake ni kwamba ile hewa yenye joto kali sana hukutana na mazingira ya baridi sana na ndiyo huo mstari mweupe uuonao.
Unaweza kujaribu hata nyumbani. Chukua chuma na ukiweke kwenye moto mkali kwa muda halafu ukitoe na kukiingiza chuma hicho cha moto kwenye maji baridi.
 
Tulipokuwa wadogo tuliaminishwa kwamba hizo ndio roketi.

Tuliambiwa kwa afrika zinatua Misri na Afrika kusini tu.

Tuliambiwa kama kama umeiona ukiwa arusha(kwa mfano) ujue ipo misri.

Hata hivyo waliotuambia habari hizo hawakuwa na lengo la kutupotosha; huo ndio ulikuwa uelewa wao.

Nimewasamehe wote.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] umewasamehe?
 
Mnatuchosha mimi mwenyewe mimacho kodoo kupata maujuzi lakini holaa.
Ule kweli sio moshi kabisa , kama ingekuwa moshi basi hiyo ndege au kama ulivyoita ingekuwa haifai kabisa

ninavyofahamu kutoka kwa wataalam wa anga wanasema: chombo kile kipo juu sana na kule kuna baridi sana kwahiyo kwakuwa chombo kile kinaproduce joto bac ile inakuwa ule ubaridi mkali kama unatoweka kwa minajisi ya mvuke ndio maana kwa kadri kinavyoenda mbali au kusogea basi ule mstari uliosema kama moshi ambao sio unatawanyika. yaani kama unarudia ile hali yake ya awali kwani lile joto la chombo kile halipo tena.

(pengine atatokea ambaye anaweza kueleza vizuri zaidi ya hapo tena kitaalam zaidi hiyo ni kwa kifupi tu na kirahisi rahisi)
 
Zile ni ndege za kawaida ambazo nyingi huruka zaidi ya km 11 toka usawa wa bahari. Sasa ule moshi wake huwa ni muunguzo wa mafuta na Oxijen kutengeneza maji na kabon dioxide. Yali maji yakitoka yanakuwa kati ka hali ya mvuke. Ule mvuke unachukua mda kuganda na kufanya matone ya maji ambayo baadaye hupotelea huko angani.
 
Joto kali linalotolewa na injini za ndege linapokutana na baridi kali iliyopo huko juu, funua kifuniko kilichoziba kitu kichemkacho utaona kitu hicho uitacho moshi, ikiwa na injini 2 ugaona miatari miwili, zikiwa 4 utaona mi4.
 
...jion hii kwa hapa dar ukiangalia juu utaona kitu kimepita kinaacha kitu kama njia au moshi ni nini hicho...mwenye kujua tafadhal
 
...jion hii kwa hapa dar ukiangalia juu utaona kitu kimepita kinaacha kitu kama njia au moshi ni nini hicho...mwenye kujua tafadhal
Ndege inapita kwenye international airspace ni juu sana na kwasababu kuna baridi hewa ya moto inayotolewa na engine ndio inasababisha hio njia kama moshi. Ukienda sehemu za baridi puliza/pumua kwa mdomo utaona kitu kama hicho.
 
Ndege inapita kwenye international airspace ni juu sana na kwasababu kuna baridi hewa ya moto inayotolewa na engine ndio inasababisha hio njia kama moshi. Ukienda sehemu za baridi puliza/pumua kwa mdomo utaona kitu kama hicho.
Asante...hio ni ndege ya kawaida au special ndege zinazoweza kupita huko maana ni nadra kuziona
 
Tulipokuwa wadogo tuliaminishwa kwamba hizo ndio roketi.

Tuliambiwa kwa afrika zinatua Misri na Afrika kusini tu.

Tuliambiwa kama kama umeiona ukiwa arusha(kwa mfano) ujue ipo misri.

Hata hivyo waliotuambia habari hizo hawakuwa na lengo la kutupotosha; huo ndio ulikuwa uelewa wao.

Nimewasamehe wote.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji3] [emoji2] [emoji1]
 
Wakuu naomba kuuliza,kuna kile chombo huwa kinapita juu kabisa ya anga inaacha moshi nyuma,tukiwa wadogo tuliambiwa ni rocket.kwa hapa africa inatua south africa na egypt tu.ss tumekua najua rocket ni ile iendayo nje ya dunia.naomba kujuzwa wakuu ni ni nini ile?
 
Back
Top Bottom