Kwanini ng’ombe wasipigwe nusu kaputi kabla ya kuchinjwa?

Kwanini ng’ombe wasipigwe nusu kaputi kabla ya kuchinjwa?

Hivi what if mtu ukifa unazaliwa tena kiumbe kingine, mfano unazaliwa ng’ombe? Incase ni hivyo, si ingependeza kama kabla ya kuchinjwa upigwe kwanza nusu kaputi, au nakosea?
Mbona wanapigwa mkuu, kama umewahi kuhudhuria machinjioni huwa kinapigwa kitu chenye ncha kwenye fuvu la kichwa kinachoenda kuvuruga ubongo na hivyo ngo'mbe huanguka kwa kukosa fahamu, baada ya hapo ndo anachinjwa bila maumivu.....
 
Wafanyiwe ‘Bolt stunning’ basi angalau
Kwa sisi waisilamu na mayahudi Kuna kitu kinaitwa Dhabiha na Shechita hii ni njia ya kawaida ya kuchinja na kuacha damu imwagike.

Baadae Nchi za magharibi zikaanzisha hio njia ya kustun kwamba ili mnyama asipate maumivu anapigwa shoti Kisha anachinjwa.

Ila tafiti mbalimbali za kisayansi zilizofanywa ni kwamba mnyama anapata maivu makubwa akiwa stunned kuliko akichinjwa kawaida.

Utafiti huu umefanywa na Professor Wilhelm Schulze wa Chuo kikuu Cha Ujerumani, Na hata 2008 waziri wa Chakula wa Ufaransa kwenye report yake uchijani wa kawaida ilikuwa ni WA kibinadamu zaidi kuliko ku stun.

Utafiti mwengine wa Dr. Karuna Chaturvedi ulionesha Nyama ya kuchinja kawaida ni nzuri kuliko ya kustun ki afya sababu mnyama anapochinjwa kawaida bado moyo una pump damu, sababu pale anapochinjwa Pana mshipa mkubwa basi inamwagika damu nyingi hivyo damu inatoka na sumu sumu na micro organism wengine.

Pia utafiti wa Dr modi huko India Nyama ya kuchinja kawaida inakuwa ni soft na tamu zaidi, Ina PH chini ya 7 (wingi wa acid) sababu mnyama hapati shida sana anapokufa tofauti na ile ya kustun ambayo Ina acid ya kutosha.

Hivyo mkuu kama unataka kuishi Kwa afya mnyama akichinjwa kawaida ni vizuri zaidi kidini na kisayansi. Kama unataka magonjwa ya ajabu ajabu tafuta means za kumchinja mnyama bila damu kumwagika.
 
Sasa si bora ng'ombe
Ukiona nguruwe anavyopigwa wakati wa kuchinjwa unaweza kulia
 
Kwa sisi waisilamu na mayahudi Kuna kitu kinaitwa Dhabiha na Shechita hii ni njia ya kawaida ya kuchinja na kuacha damu imwagike.

Baadae Nchi za magharibi zikaanzisha hio njia ya kustun kwamba ili mnyama asipate maumivu anapigwa shoti Kisha anachinjwa.

Ila tafiti mbalimbali za kisayansi zilizofanywa ni kwamba mnyama anapata maivu makubwa akiwa stunned kuliko akichinjwa kawaida.

Utafiti huu umefanywa na Professor Wilhelm Schulze wa Chuo kikuu Cha Ujerumani, Na hata 2008 waziri wa Chakula wa Ufaransa kwenye report yake uchijani wa kawaida ilikuwa ni WA kibinadamu zaidi kuliko ku stun.

Utafiti mwengine wa Dr. Karuna Chaturvedi ulionesha Nyama ya kuchinja kawaida ni nzuri kuliko ya kustun ki afya sababu mnyama anapochinjwa kawaida bado moyo una pump damu, sababu pale anapochinjwa Pana mshipa mkubwa basi inamwagika damu nyingi hivyo damu inatoka na sumu sumu na micro organism wengine.

Pia utafiti wa Dr modi huko India Nyama ya kuchinja kawaida inakuwa ni soft na tamu zaidi, Ina PH chini ya 7 (wingi wa acid) sababu mnyama hapati shida sana anapokufa tofauti na ile ya kustun ambayo Ina acid ya kutosha.

Hivyo mkuu kama unataka kuishi Kwa afya mnyama akichinjwa kawaida ni vizuri zaidi kidini na kisayansi. Kama unataka magonjwa ya ajabu ajabu tafuta means za kumchinja mnyama bila damu kumwagika.
Kama ni hivyo, apigwe risasi ya kichwa, then ile akipoteza fahamu tu, achinjwe papo hapo.., tafiti ziendelee, vyovyote iwavyo, si vyema kwa sisi viumbe tuliopewa ufahamu (intelligence) kuendelea kutesa viumbe wengine namna hii wakati tunaweza kufanya tafiti na kuwapa unafuu. Ila hiyo ‘Bolt stunning’ bado naamini ni nzuri, maana ubongo unachomwa na kitu chenye ncha kali, hivyo lazima apoteze fahamu tu.
 
Changamoto ni "wash out period" yani muda ambao dawa itaishi kwenye mwili wa ng'ombe kabla ya kutoka nje kupitia mkojo au njia zingine.

Inapaswa ng'ombe alie kwenye tiba akae walau siku 14-28( kutegemea na dawa) ndipo achinjwe, ili kiruhusu dawa hiyo itoke nje ya mwili na kuepuka madhara kwa mtumiaji

Ndio maana hatutumii nusu kaputi kabla ya kuchinja wanyama hawa
Basi Watz wengi twala dawa
 
Hiwa wanafanyaje, mimi sijawahi kuona, huwa inakuwaje kwani?
Umewahi kuona kifo cha wanyama kama nyati, swala, nyumbu etc mbele ya kundi la mbwa mwitu? Wao hata huko kuchinja wanaona ni kupoteza muda. Wanaanza kuchokonoa sehemu laini zenye matundu kama za haja kubwa na kuchomoa utumbo kidogo kidogo huku wakiendela kula mpaka mnyama ajifie mwenyewe. Kuna wale mijusi wanaoitwa komodo dragon. Wao wanang'ata sehemu ndogo sana na kuacha sumu ambayo itafanya mnyama aanze kuoza kidogo kidogo mpaka ajifie mwenyewe ndipo wanamla. Na inaweza kuchukuwa hata wiki, wao kazi yao ni kumfuatilia kwa nyuma tu. Bila shaka hata chatu nadhani unajua yeye anameza windo likiwa nusu hai. Ninachotaka kusema hapa ni kuwa tuache nature ichukuwe mkondo wake. Tunaweza kuwaonea ng'ombe huruma lakini bado kuna ma-elfu ya viumbe wengine wanakufa na kuliwa kwa mateso makali.
 
Kwenye machinjio kubwa duniani ngombe hupigwa shot ya umeme na kuzima
 
Back
Top Bottom