Kwanini Paul Kagame aangalie jeshi letu kwa dharau likionesha uwezo wake kwenye maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru?

Kwanini Paul Kagame aangalie jeshi letu kwa dharau likionesha uwezo wake kwenye maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru?

Rafiki yangu tafuta vitu vya kuandika basi kama huna unaonaje ukikaa kimya kwani nani atakuona hujui fb?

Huu ni upimbi watu wanahitaji mijadala inayowajengea weledi siyo upumbavu kama huu.

Ifikie maadmin nyuzi kama hizi zisizo na tija zifutwe kabisa, ujinga gani huu?
Kama umeona ni upimbi basi jina pimbi unatakiwa uitwe wewe kwa upimbi ulio nao kichwani!
 
Africa Mashariki nzima mwenye ndege za kisasa ni Uganda. Nakumbuka wao wana Sukhoi (Su-30)5 na Mig 21 kama 6. Pia wana helikopta Mi Mi-24 kama 5. Ilibidi wavunje benki kununua hizo. Hiyo ni fire power kubwa sana si ya kuchezea.
Sisi bado tuna Wachina Shenyang-6 na 7.
Na saivi anafanya mashambani ya anga kule Congo DRC kuwasaka waasi wa ADF.
 
Mimi nilifurahi sana yale madude kupita mbele yake najua zile ni outdated tu version Jeiwii wanazo dhana za kisasa zaidi ziko huko ndani ndani zimefichwa .

Kama analeta dharau ajaribu moto wake
 
Kubeba mzigo wa kilo zaidi ya 30 kisha unaruka ruka nao na ile ya kuvunja matofari kwa mikono sidhani kama ndio uwezo wa komandoo,isitoshe kwa nini haswa hawa special forces washirikishwe kwenye maparade???tena mbele ya wageni tena majirani zako??
 
Mtu pekee anaeweza kumu outsmart PK ni JK na mimi tu,, huyu jamaa tayari ana Blackhawk attack helcopters, na hii ni tabu kweli kweli,, inabidi angalau nasisi tutafute HIND..
In order to outsmart that guy, you must think like him,,, he is very smart
Sisi soon tutachukua Chinook
 
Ila kwa kweli sikujua hasa shabaha ya waliotaka kuonesha vifaa vya kijeshi! Kama ni kuonesha tuna 'vifaa' wamefeli sana. Vingi ni obsolete na hata vimesahauliwa (Mig 21). Badali yake, imetoa picha kuwa hata makamanda wakuu wa jeshi letu hawajui maendeleo makubwa yaliyopo katika zana za kijeshi. Afadhali wangeficha aibu na kuleta kile tunachofanya vizuri zaidi tu: muziki.
Uhuru wetu hatukuupata kwa vita, wala hatuna vita hivi sasa au hatari ya karibu, kwa nini ikawa lazima kuonesha vifaa vya kijeshi kama 'maendeleo ya miaka 60?' hasa ukijua kuwa hatutengenezi chochote katika hivyo! Beats me.
Wewe ndio itakuwa mjinga

Ushaambiwa taarifa nyingi za jeshi letu ni siri

Huwezi jua huko jeshini kuna zana gani za kisasa

Hizo ambazo outdated hazina madhara kabisa

Pale zililetwa kwa gwaride tu
 
Alichokiongea Masanja ni matokeo ya Siasa za kusifia kila kitu.Hakuwa na kitu kichwani zaidi ya kusifia mpaka akajikuta anaongea upuuzi
Magufuli aliwatia sumu wapumbavu wengi sana

Wengine ndio wana recover wengine wako critical mentally

Tuache tabia za kusifia sifia upumbavu.
 
Ubora? Labda kwa idadi ga askari lakini sio ubora

Jeshi makomandoo wake wanateswa na makachero km watt na JWTZ liko kimya!

Unajua PK ndie alieliongoza jeshi letu kumtoa Idd Amin?

Au mlidanganywa kuwa ni Mayunga?

PK ni extreme fighter sio level yetu mkuu
Mimi nilikuwepo wakati wa vita ya Kagera,japo sikupigana.
Kagame namfahamu nnje ndani,ni mwanafunzi wetu.
Kagame alichojaliwa zaidi kama "individual" ni "akili kubwa ya kikatili". Kagame kuwa "exteme fighter" hakumfanyi kuwa na jeshi bora zaidi ya JWTZ.
 
Mimi nilikuwepo wakati wa vita ya Kagera,japo sikupigana.
Kagame namfahamu nnje ndani,ni mwanafunzi wetu.
Kagame alichojaliwa zaidi kama "individual" ni "akili kubwa ya kikatili". Kagame kuwa "exteme fighter" hakumfanyi kuwa na jeshi bora zaidi ya JWTZ.
Ulikuwepo ukupiga,ndo nini? Mbona ata mimi nilikuwepo sana tu.

PK sio tu alisoma Tz bali alipata pia mafunzo ya juu ya kijasusi marekani...ivyo ni mwl wetu na sio mwanafunzi tena.

JWTZ limechapwa mbaya uko Msumbiji na magaidi,PK kaombwa kuingiza jeshi lake uko ata wiki haijaisha habari ya magaidi imefifia kabisa uko Msumbiji
 
Jeshi hatari sana hili, siliwezi abadan.

FB_IMG_16391136146139547.jpg
 
Hao hao ndio waliomfurumusha kule Congo DRC kwa jina la M23....hawawezi kamwe. Ana wagambo wanaosumbua disorganized armies Kama DrC Congo,UPDF,wale Magaidi wa Mozambique,Waasi wake n.k.

Jwtz ni organized, experienced and well equipped army. There is nothing to compare with tiny Rwandan Army.
Waambie
 
Ujinga ninkutokuwa na info za kutosha.

PK kaanza vita akiwa kijana mdogo sana na alishiriki vita ya Uganda mstari wa mbele kabisa km kiongozi wala sio informer,umepotoshwa..soma!

PK ndie aliemfurusha Idd Amin ndipo akina Mayunga wakafuata..soma!

M7 alipoingia madarakani alimpa cheo PK cha kusimamia na kulinoa jeshi la Uganda...soma!

Baadae PK alirudi msituni kuikomboa Rwanda chini ya utawala wa wahutu...soma!
Wewe ndie huna info za kutosha, au umeamua tu kusema uongo! Sio kweli kwamba eti PK ndie alimfurusha Amin! Vita ambavyo PK alipigana inaitwa Uganda Bush War na sio Kagera War!! Hii vita ilikuja baada ya Obotte kushinda kiti cha urais na Museven akakataa matokeo kwahiyo akaingia msituni, na kwahiyo alisaidia kumwondoa Obotte madarakani na sio Idd Amin!
Hakuna vita PK aliwahi kushindwa,
Vita ipi za kujivunia alizopigana na kudai eti hajawahi kushindwa?! Unazungumzia vita ya kupigana na wanamgambo ambao majority hawana any formal military trainings au unazungumzia vita dhidi ya jeshi dhaifu la DRC wasiolipwa hata mishahara?! Unazungumzia Vita Dhidi ya Wauaji wa Kihutu waliokuwa wanatumia mapanga, au vita ipi hasa?
ndje jasusi bora kabisa kuwahi tokea kusini mwa sahara...US wanajua,Nyerere,JK,JPM hawa wote na ubabe wao kwa 'slim' hawakuwahi kumchokoza
Kwahiyo huo ubora ni kwa sababu kasomea US, au?! Hivi kwa akili yako unaamini kabisa kwamba ni PK pekee ndie kasomea ujasusi US?! Au unamuona bonge la jasusi kwa sababu huwa anafanikiwa kuua wapinzani wake ?! Huo ubobevu wake unaupima kwa kutumia vigezo gani?!

On top of that, huyo Nyerere, JK na JPM waliwahi kumchokoza nani? Unadhani kila rais ni mpenda vita na kuua kama alivyo Kagame? Btw, pale vikaragosi wake wa M23 waliposambaratishwa alifanya nini?!
Wewe una taarifa sahihi sana za PK.

Jeshi letu lina idadi kubwa ya wanajeshi lakini halina ubora wowote ukilinganisha na la Rwanda.
Ubora wa Jeshi la Rwanda unaupima na nini?!
PK ni level nyingine kabisa acha atudharau km makomandoo wetu wanapigwa vibao na askari polisi hakuna namna,dharau lazima
Kwahiyo kwavile ni makomandoo unadhani wao ni watu wa vurugu?! Kwamba wakikutana na polisi, wanadindisha na kuanza kupiga majudo!! Au kwavile polisi waliwapiga makofi makomandoo kama unavyodai, ndo unataka kuaminisha watu kwamba polisi wetu ni bora kuliko makomandoo?!
 
Back
Top Bottom