Patience123
JF-Expert Member
- Mar 10, 2013
- 5,092
- 8,784
Shkamoo Kiranga.Kumbe ndio maana hatuelewani mara nyingine.
Ningezaa kwa kuwahi kuwahi Kiswahili Swahili wewe ungekuwa mwanangu wa tatu.
Yani wewe umri wako wa sasa ni mdogo kuliko umri wangu nilivyomuona Puza mara ya mwisho Tambaza.
Acha uchokoziTeh!halafu wewe LIKUD nahisi ulikuwa mnyonge mnyonge sana.
Hivi yale maandazi yaliyokuwa yanapitishwa break time ushawahi kula hata siku moja wewe?
MkuuDuh, umenikumbusha Busianya mzee wa Fegi na anaongea kwa pozi na kujiamini sana, na ndie aliyetangaza Msiba wa Puza, maana Puza alijiua wakati wa likizo na tulipofungua tu yeye ndiye aliyetangaza
Pamoja na hayo yote hakuwahi kuwa Head master Tambaza, alikuwa second Master , maana baada ya Mushi kuchemsha Mziki wa TSS kijiti alipewa Mtela
Sawa kaka majina yalinichanganya kidogo, umri nao umeenda haya tunayoyaongea yametokea miaka 27-30 iliyopita, ni vile nafsi haizeeki tu, maana nikifumba macho nayaona matukio kama yametokea jana tu, kweli bwana alikuwa anaitwa Hawanga na baada ya hapo Tambaza nadhani aliendaga Navy KigamboniMkuu
Busanya alikuwa ni mwanamke, yeye alihamishiwa Forodhani kuwa Head mistress.
Huyo mvuta fegi alikuwa anaitwa Hawanga, yeye na Mushi ndio walishindwa kuihimili Tambaza, matokeo yake ndio tunayoyaona leo.
Nakumbuka group iliyoletwa Kwiro boys kutoka Tambaza tuliwapokea getini kwa kuwapiga kwenzi Na kuwarusha vichura sana, hatukutaka ujinga kabisa!!!Ha ha ha kitambo Sana daah...nakumbuka uuzwaji wa kiwanja cha mpira kutoka Tambaza kwenda muhimbili Primaly..mkaguzi wa Elimu sec Alexzander Ndeki akaja mkutanoni akamwaga data...,namkumbuka,Puza,Sagapower,Vimto..... Makamu WA shule Mr Wajimira,yule mzee aliyekuwa mkuu WA shule jina nimemsahau....baada ya fujo na Azania 1994,form wote tukasimamishwa shule mwaka nzima...mwaka uliofuata tukaperekwa shule za mikoani,...form one yetu ya 1993 ilikuwa na watu wakorofi Sana...
Huyu ni rwegoshora ambaye siku hizi ni mkaguzi hapo st Anne Marie? Maana naskia alifundisha Azania maths na PhysicsMwaka 1988 mechi ya Tambaza na Azania ilipigwa uwanja wa magunia msasani ambapo wanafunzi wa Azania na mwalimu wao wa michezo rwegoshora waliangushiwa kipigo cha mbwa mwaka 1989 mechi hii ilipigwa ndani ya uwanja wa Azania refa rii akiwa kanali kipingu baada mechi Azania walilazimika kuvua kaptula za khaki na kutembea kwa miguu adi majumbani kwao ili kunusuru maisha yao!
Wapi kaka Pascal Mayala atupe michapo ya Tambaza ya akina shetani, no-mbungi, Okelo, chapa?
Kweli kakaSawa kaka majina yalinichanganya kidogo, umri nao umeenda haya tunayoyaongea yametokea miaka 27-30 iliyopita, ni vile nafsi haizeeki tu, maana nikifumba macho nayaona matukio kama yametokea jana tu, kweli bwana alikuwa anaitwa Hawanga na baada ya hapo Tambaza nadhani aliendaga Navy Kigamboni
Haahaaa kumbe hapo ningeambiwa nimenunua chetiKweli kaka
Ni muhimu kurekebishana - maana nasikia kwenye uhakiki wa vyeti unaulizwa hadi walimu wako waliokufundisha.
Kama wangeuliza swali la jinsia, kwa kweli ungelezea umekinunua bei gani hicho chetiHaahaaa kumbe hapo ningeambiwa nimenunua cheti
Mkuu uko vizuri sana kumbu kumbu!Mwaka 1988 mechi ya Tambaza na Azania ilipigwa uwanja wa magunia msasani ambapo wanafunzi wa Azania na mwalimu wao wa michezo rwegoshora waliangushiwa kipigo cha mbwa mwaka 1989 mechi hii ilipigwa ndani ya uwanja wa Azania refa rii akiwa kanali kipingu baada mechi Azania walilazimika kuvua kaptula za khaki na kutembea kwa miguu adi majumbani kwao ili kunusuru maisha yao!
Wapi kaka Pascal Mayala atupe michapo ya Tambaza ya akina shetani, no-mbungi, Okelo, chapa?
Wababe wa enzi hizo na kichwani zilikuwemo. Walichofanya ni mambo ya umri wao na mazingira yao. Yasemekana katika shule hizo kulikuwa na watoto wa kishua na watoto wa kitaa pia na kila mmoja alijiona ni sehemu ya familia hiyoo. Kulikuwa na tofauti kati ya shule hizo za wagumu na zile za mchanganyiko kama Forodhani na Kibasila. Ni watu wa maana katika jamii yetu na wala si wa hovyoo! !Je Puza asingejiuwa angekuwa mtu wa aina gani leo hii?
Angekuwa ni kiongozi mashuhuri au angekuwa jela?
Saa zingine inabidi tujiulize kuwa baada ya kifo tunaacha historia gani kwa kizazi kijacho.
Wakati Puza anahangaika na fujo kuna wanafunzi wengine ambao hawakuwa na majina pale Tambaza walikuwa wanahangaika na masomo na mungu si athumani wengine wamekuwa wanasheria, madaktari nk.
Napenda kujua hatima ya wababe wengine wa Tambaza kama akina Buchiza,Bedui, Emmanuel Mbwili, Tyson nk
Huyu Lulindi alikuwa burudani sana watu walikuwa wanazamia hadi kipindi chake anapokuwa darasa jingine!Hapo Juma Bios na Lulindi Swahili, unamkumbuka mwalimu wa Siasa Manyasi?
Mzee wa Socrates.Huyu Lulindi alikuwa burudani sana watu walikuwa wanazamia hadi kipindi chake anapokuwa darasa jingine!