#COVID19 Kwanini Rais ameamua kujificha nyuma ya kamati ya Corona? Anaogopa nini kuwambia Watanzania wajiandae na AstraZeneca? Anaogopa nini?

Rais wetu anajua kabisa Sayansi ni Sayansi na sio Siasa, lazima ashauriwe na Wanasayansi sio Lumumba
Hao wanasayansi wenye uwezo wa kushauri mapambano ya corona nchi hii ni kina nani?
Wanawazidi kweli wanasayansi wa China,Marekani,Brazili na hata Itali na Spain?
 
Bahati mbaya mie nimesoma vet medicine. So sio kwamba sijui nachoongea.

Kujifanya msomi na mjuaji sana mbele za watu, haitakusaidia sana.
Medicine expert nilitegemea uwe maabara unasaka suluhisho la Covid should it strike Vets!! Lakini mpo busy mitandaoni kukejeli efforts za wenzenu!!

To be honest unaona ni sawa?
 
Kenya wanaofuata COVID19 protocols wako wapi?
Je hamsikii hosptali na mfumo wa afya ulivyozidiwa?
Mbona bongo tunaishi na vizuri tu na maisha yanaendelea kama kawaida?
Tunataka maisha gani zaidi?
Yaani siku wakinikanyaga wakasema lockdown....ndo siku serikali itatambua kuna mwananchi kavurugwa. Naahidi kuwa sauti ya wengi. Wawekane lockdown hao viongozi huko,sisi watuache na haso zetu.
 
Suala la bando lilikuwa ni suala la kutoa kauli moja tu mambo yarudi kama yalivyokuwa. Unawaambia watu wakaangalie la kufanya na tatizo lisijirudie tena ilhali halijaondoka.

Yaani hii nchi italiwa mpaka basi.
Hapa ndio najua watu sio wasomaji.... Kwa miongozo ya TCRA price per MB ceiling ni 9 Tshs ina maana kihalali kabisa GB 1 inatakiwa iuzwe elfu 9!!!

So hapo voda walipandisha hadi Tsh 4 tu ndio kelele zote zile. Ssa inatakiwa TCRA ndio warudi kupunguza ceiling za Price per MB na sio eti kuwaambia mitandao ishushe, it's wrong tunawaonea tu.

So statement ya mama inagusia huko maana shida ni TCRA sio Mitandao.
 
Kwenye covid maguful alikua sahih 100%.
Huyu mama asitake kutuletea mabalaa yake
 
Kwenye covid maguful alikua sahih 100%.
Huyu mama asitake kutuletea mabalaa yake
he wasnt. maybe 40%. alikuwa anataka ku induce mentality ya kupotezea mambo ya maana. kufanya kama hayapo kwamba yatapotea yenyewe.
thats his mistake lakin pia ni kinyume na kauli ya mwalimu J.K.Nyerere
 
Unataka tuweke lock down, huo ndio utaalam unaotaka, hao wenye lock down wanakufa wengi zaidi ya Tz sasa nini faida ya lockdown ? SSH ana tatizo, tena ni KUBWA.
Tunaongelea lockdown au chanjo ya korona?
 
Yaani siku wakinikanyaga wakasema lockdown....ndo siku serikali itatambua kuna mwananchi kavurugwa. Naahidi kuwa sauti ya wengi. Wawekane lockdown hao viongozi huko,sisi watuache na haso zetu.
nani kwakwambia wataweka lockdown?
yaani you guys mkisikia covid mnarukia lock down?

SSH hakusema lockdown..ila iyaundwa kamati maalum ya kufanya uchunguzi halaf ije na suggestion. nothing else.
 
SSH hakusema watu wasilipe kodi au waonewe huruma.
suala la kodi liko kisheria, hilo halikwepeki.
instead of kutumia too much power , akili zaidi ..iendane na itashi wa ukusanyaji kodi.

uzuri sheria za ukusanyaji kodi ziko open kabisa. na zimesha ainisha nini kifanyike kwa atakaegoma kulipa kodi.
 
Hamna kitu pale, mbaya zaidi anajiona ana akili halafu ni mtupu kabisa, JPM alificha madhaifu ya wengi wa pembeni yake. Rais anaruhusu vipi expatriates wapewe vibali ovyo tu kwa kuwa muwekezaji ametaka, anaenda ku sign mkataba wa LNG Lindi , mkataba wa 30bn USD kwa kukurupuka, ameshatoa maagizi gesi ya Hellium iuzwe tayari, ndani ya 3 weeks unaona kabisa tumerudi 15yrs back.
 
Akili zipi ? Kama kodi ni kubwa angesema sheria ibadilishwe kwa wote Ila saivi ametoa mwanya wa rushwa, wengine hawatalipa kodi kwa kuwa “watafikiriwa “ na TRA, huyu mama ni mzigo na anaongea mambo mazito ambayo hana uelewa nayo.
 
Mkuu unaongea sana kuhusu mzee wako na hiyo covid,mbona mie mzee wangu hakuwahi kulazwa hospitali ila ilikuja kutokea alilazwa kwa malaria lakini mbona sipigi kelele humu kuhusu malaria? Au ulitaka na mimi nianze kupiga kelele na kwamba malaria hatari kisa mzee wangu alilazwa na malaria.
 
Haupigi kelele sababu alitumia dawa ya malaria na sindano zilizotengenezwa na mabeberu!! Ila cha kushangaza mabeberu hao hao wakitengeneza chanjo ya Covid wanageuka WAUAJI!!
 
Kwani rais ni mtaalamu wa chanjo au afya hadi ajuwe hayo yote?
 
Unataka tuweke lock down, huo ndio utaalam unaotaka, hao wenye lock down wanakufa wengi zaidi ya Tz sasa nini faida ya lockdown ? SSH ana tatizo, tena ni KUBWA.

Acha basi ujinga, mkuu. Kwani lockdown ndio kitu pekee kinahitajinkufanyika?? Vipi kuhusu mikusanyiko, kuvaa barakoa, vipi kukiri korona ipo na tukapima na kutoa taarifa??

Mama amesema kabisa - swala hili litashughulikiwa kisayansi. Kuwa na subira kujua ni hatua gani za kisayansi zitapendekezwa na zinatekelezeka. Kwa aina ya uchumi wetu “lockdown” is not an option. Hautuiwezi.

Umejuaje kama wanakufa wengi zaidi ya Tanzania wakati hapa nyumbani hakuna vipimo hata kwa wagonjwa walio mahospitali?? Unawezaje kulinganisha statistics wakati una za upande mmoja tu? Huoni unatakiwa kupewa takwimu za Tz ili ufanye ulinganifu? Mna akili gani lakini aisee????
 
Nani kakuambia Tz hakuna kipimo cha Corona? Unaongea ujinga gani wewe?
 
Haupigi kelele sababu alitumia dawa ya malaria na sindano zilizotengenezwa na mabeberu!! Ila cha kushangaza mabeberu hao hao wakitengeneza chanjo ya Covid wanageuka WAUAJI!!
Unajua hata hao Mabeberu wenyewe watakushangaa kwa sababu umekazania hizo chanjo kuliko hata wao, wao huko wenyewe wanaona Astrazeneca zinagandisha damu na hadi wameacha kuzitumia kwa baadhi ya makundi ya watu ila wewe bado huoni shida katika hizo chanjo na unatushambulie sisi hutaki tuseme kuwa hizo chanjo zina shida kisa et tunatumia chanjo zengine za mabeberu hivyo na hizi hutaki tuseme hata kama zina shida.
 
Nadhani kufa sana kwenye corona kunaendana na kasi ya maambukizi na ndio maana wenzetu wameweka hadi lockdown ili kupunguza hiyo kasi ya maambukizi na ndio tunaambiwa kama si kuchukua hizo tahadhari basi hali ingekuwa mbaya zaidi, sasa sisi ambao hatuchukui tahadhari kabisa na mikusanyiko inaendelea kama kawaida unadhani hali ingekuwaje? maana huko kwa wenzetu kuna muda tunasikia hadi wanazidiwa na wagonjwa na ndio huduma zao za afya zipo vizuri.
 
Ulaya nzima wamechoma AstraZeneca na cases za matatizo ni chache.

Wewe mleta mada ni Mbumbumbu. Kwanini usizungimze chanjo ya Johnson au pfizer umeitaja Astra?

Hii sio nchi tajiri yenye uwezo wa kuchanja kila mtu. Chanjo ikija kama wewe hutaki usichanje na kama hutaki kuvaa barakoa pia ni sawa hayo ni maisha yako hakuna atakayekulazimisha.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…