Kwanini Rais Magufuli alimfunga Kabendera?

Kwanini Rais Magufuli alimfunga Kabendera?

Ukitaka kujua ni kwa nini kabendera alikamatwa. Kwanza lazima ujue kabendera ni mwandishi wa habari za kichunguzi. Na habari zake alikuwa anayatumia makampuni ya kigeni hasa wingereza. Fikiria mwandishi achunguze na kupata habari nyeti na kuzituma nje ya nchi si hatari hiyo?
Ukizingatia kipindi cha magufuli kuna watu walikuwa wamejipanga kuhakikisha wanampa wakati mgumu katika kuiongoza hii nchi.

Hata hivyo nadhan kabendera ana mtandao mkubwa ndani ya serhkali unaomlinda maana mara nyingi mtu ukijua siri za ikulu usalama wako ni mdogo.
Mimi naona wengi mnaliongelea hili suala kama vile Magufuli aliongoza nchi kwa utulivu pasipo YEYE MWENYEWE kufanya Declaration ya kwenda kinyume na makubaliano au mikataba ya umoja wa mataifa. Kiufupi HAKUJALI

Mfano mdogo tu ni issue ya mabinti wa shule waliopata mimba kuendelea na masomo baada ya kujifungua.

Alikuwa ni kiongozi ambaye negative news zilikuwa zinatoka kila mara kutokana na kauli zake au actions zake YEYE MWENYEWE

Yes kabendera yawezekana alikuwa akitumika na wazungu kwa sababu tu anapokea pesa zao lakini ni wanaharakati, mashirika na miradi mingapi hadi sasa inategemea pesa za wahisani?....

Nachokiona tu hapa watu mnatetea mtu au watu na sio hoja. Natamani mjadala kama huu ungejawa facts na sio hisia
 
Achafue kitu kilichokuwa kimechafuka

Mbona ilikuwa wazi kuwa Magufuli hakujali kuhusu uhusiano wa kidiplomasia na nchi kubwa hususani nchi za magharibi

Yeye mwenyewe mara zote alitoa kauli controversial kwa kushutumu kuanzia viongozi wa ndani hadi mabeberu kwa matatizo yote.

Au kuweka bunge lote kuwa la kijani katika uchaguzi wa 2020, nalo kasingiziwa

Mara ngapi yeye mwenyewe alienda kinyume na makubaliano au mikataba iliyopelekea ndege za nchi kuzuiwa na billions of money serikali kulipa baada ya kifo chake ili kurudisha hayo mahusiano na nchi za kimataifa na wawekezaji.

Vitu ambavyo Tindu alivipigia kelele siku zote na vitu vilivyokuja kutokea.

Magufuli alikuwa ni Rais Mtendaji ndio maana kwenye physical infrastructures ameacha legacy kubwa Ila tukiongelea katika diplomasia, intellect, utawala wa sheria, na Demokrasia. Toka vyama vingi vianze anaweza kuwa the worst president

Na ubaya wa nchi hii ni wanachi kutetea vyama na viongozi kuliko kutetea nchi yao. Hii ndio sababu tumefika hapa
Hizi ni hadithi za JF, kutokana na narrative ambayo ilikuwa shaped na makuwadi wa mafisadi.

Unaweza toa mfano hata wa nchi iliyokuwa na diplomatic row na Tanzania. Zaidi ya ushahidi wa nakala za wachonganishi nje ya nchi na sisi wenyewe kushadidia wakati mwandishi ni Kabendera.

Wao walikuwa wanamtumia Kabendera kama source of pressure ya mikataba yao au kupinga sheria zetu za kulinda rasimali (ni sponsored articles). Halafu wanazileta humu JF kuponda serikali inaharibu mambo (utoto) na team mafisadi kushindilia fitna.

Kwa Lissu naweza muongelea kwa content nyingine za sheria, lakini sio mambo ya mikataba ya biashara hasa ya natural resource (hana anachokijua huko) so is Kabudi sasa sijui uwa anaongea nao nini huko.

Ndio ukweli.
 
umeandika maoni mazuri kabisa yasiyo na chembe ya unafiki. Kuhusu mabeberu nadhani alikuwa anasema ukweli japo wenyewe hawapendi kuambiwa.
Ni sawa kabisa. Magufuli alitoa declaration of war na "mabeberu" Kwa kauli na matendo yake kwa hiyo sioni sababu za kusema kabendera alikuwa anamchafua kwa kutumia vitu vile vile kuandika makala za kiingereza ambazo kiuhalisia zinalenga elite class na watu wa nje
 
Kabendera alikuwa anatumika na watu wa nje kumhujumu Magufuli alitaka kupindua utawala wa Magu.
Mwandishi wa habari unaandika artcles 4 kwa mwezi kwenye akaunt yako unalipwa million 300. Unachomoa pesa unazitawanya kwa wakosoaji wa serikali mitandaoni. Hiyo investigative journalism kilikuwa kichaka cha money laundering alikuwa anatumika kwa kazi maalum kazi chafu.
toeni kitabu kinachopinga kitabu cha kabendera
 
Mimi naona wengi mnaliongelea hili suala kama vile Magufuli aliongoza nchi kwa utulivu pasipo YEYE MWENYEWE kufanya Declaration ya kwenda kinyume na makubaliano au mikataba ya umoja wa mataifa. Kiufupi HAKUJALI

Mfano mdogo tu ni issue ya mabinti wa shule waliopata mimba kuendelea na masomo baada ya kujifungua.

Alikuwa ni kiongozi ambaye negative news zilikuwa zinatoka kila mara kutokana na kauli zake au actions zake YEYE MWENYEWE

Yes kabendera yawezekana alikuwa akitumika na wazungu kwa sababu tu anapokea pesa zao lakini ni wanaharakati, mashirika na miradi mingapi hadi sasa inategemea pesa za wahisani?....

Nachokiona tu hapa watu mnatetea mtu au watu na sio hoja. Natamani mjadala kama huu ungejawa facts na sio hisia
uko sahihi kabisa. Kuna mambo mengi magufuli alikosea. Na kuna mazuri pia alifanya. Kipindi anaingia madarakan nchi ilikuwa na hali mbaya zaid. Kuna baadhi ya vitu alifanya ambavyo hata ingekuwa wewe ndo uko madarakani kwa wakati ule ungefanya kama yeye alivofanya. Kwa mtawala kuua watu ambao wako kinyume nae ilikuwepo tangu zamani.

Labda utakubaliana na mimi kuwa wakosoaji wengi wamejikita kubainisha mabaya ya magufuli na kumchora vibaya kwa jamii iliyokuwa ikimuona kama kiongozi bora. Jiulize nia yao ni nini hasa?
 
Hizi ni hadithi za JF, kutokana na narrative ambayo ilikuwa shaped na makuwadi wa mafisadi.

Unaweza toa mfano hata wa nchi iliyokuwa diplomatic row na Tanzania. Na wachonganishi ni nakala zao za nje.

Wao walikuwa mtumia Kabendera kama pressure ya mikataba yao au kupinga sheria zetu za kulinda rasimali (ni sponsored articles). Halafu wanazileta humu JF kuponda serikali inaharibu mambo (utoto).

Kwa Lissu naweza muongelea kwa content nyingine za sheria, lakini sio mambo ya mikataba ya biashara hasa ya natural resource (hana anachokijua huko) so is Kabudi sasa sijui uwa anaongea nao nini huko.

Ndio ukweli.

Unaweza kuniambia kwa nini magufuli alienda kuchukua mikopo kwenye bank ya Exim ambayo ina interests za kibiashara na kuacha nchi za wahisani na mashirika ya fedha za kimataifa yenye riba maalum kwa nchi ??...

Unadhani ni nchi ngapi ziliondoa funds zake kwenye miradi mbalimbali ya serikali na hata NGOs kuja Tanzania ikiwemo USA ambaye alipata guts za kumpiga ban mkuu wa mkoa wa nchi asiingie marekani kwa kuhusishwa na utishiaji wa maisha na uhuru wa watu..

Articles zoteee zipo mtandaoni au unadhani uhusiano wa kidiplomasia ni kuingia katika vita mkuu.

Mbona vitu vipo wazi...

Najua wengi mlimpenda Magufuli kama dini na mnaumia mkisikia kasemwa kwa lolote na hata Mimi kuna baadhi ya vitu naona anaonewa sometimes Ila kuna vitu vingi alivifanya ambavyo vitakuwa doa katika utawala wake kama ambavyo Nyerere na Mkapa walikiri baadae kuwa kuna pahali walikosea. Kwa hiyo hamuwezi kugeuza nyeupe kuwa nyeusi, historia ya Magufuli itamuhukumu kama inavyopasa
 
Unadhan kabendera alifanya ivo kwa faida ya nani? Nani alikuwa nyuma yake? Ingekuwa wewd ndo prezida ungefanya nini? Ukumbuke kabendera anataja mabaya ya magufuli je yeye hana makosa? Kwa nini hasemi na ya kwake, siku zote msema peke hushinda
Ni sawa kabisa. Magufuli alitoa declaration of war na "mabeberu" Kwa kauli na matendo yake kwa hiyo sioni sababu za kusema kabendera alikuwa anamchafua kwa kutumia vitu vile vile kuandika makala za kiingereza ambazo kiuhalisia zinalenga elite class na watu wa nje
 
uko sahihi kabisa. Kuna mambo mengi magufuli alikosea. Na kuna mazuri pia alifanya. Kipindi anaingia madarakan nchi ilikuwa na hali mbaya zaid. Kuna baadhi ya vitu alifanya ambavyo hata ingekuwa wewe ndo uko madarakani kwa wakati ule ungefanya kama yeye alivofanya. Kwa mtawala kuua watu ambao wako kinyume nae ilikuwepo tangu zamani.

Labda utakubaliana na mimi kuwa wakosoaji wengi wamejikita kubainisha mabaya ya magufuli na kumchora vibaya kwa jamii iliyokuwa ikimuona kama kiongozi bora. Jiulize nia yao ni nini hasa?

Amini usiamini watu wengi waliotaka demokrasia waliumizwa.. Mfano mdogo Fatma Karume ofisi yake ilichomwa na haki yake ya kupractice elimu yake ya sheria ilichukuliwa

Huyu ni mjukuu wa Karume senior na mtoto wa Karume junior. Binti wa Royal Family,

Jiulize vipi kuhusu wengine ambao hawana hiyo protection ya Kifalme

Kwa hiyo Mimi ninawaelewa, watu wengi wana machungu

Japo unalosema kwa mfano, wizi mwingi wa nchi huwa unatumia kalamu na udhaifu wa sheria zilizopo kuiba. Kwa hiyo kuna namna watu flani ilikuwa lazma waumizwe ilo nchi ipige hatua

Lakini huku kwenye makelele, sikuona umuhimu wa kutumia nguvu kubwa sana maana ndio iliozaa uchawa wa kisiasa. Watu kusifu na, kuabudu ili wapewe favour, kitu ambacho kinatughalimu hadi sasa maana kila mtu anaongea vitu vinavyomuweka katika nafasi ya kumfurahisha Rais na kusahau kitu kilicho bora kwa nchi ikiwemo kuongea ukweli unaoumiza.
 
Msikilize Kabendera aliokuwa kafungwa nao zama za Magufuli na kumpa umbea wa kitabu chake cha hovyo.

We unadhani kujitoa muhanga kama Magufuli kwa nchi kama Tanzania ni rahisi. .

Sisi watanzania ni ungratef tulipna mengoul people yaani tunathubutu kumtukana kabisa Magufuli.
Kabe kaandika kitabu poa sana. Uzuri tz tulikuwepo
 
Amini usiamini watu wengi waliotaka demokrasia waliumizwa.. Mfano mdogo Fatma Karume ofisi yake ilichomwa na haki yake ya kupractice elimu yake ya sheria ilichukuliwa

Huyu ni mjukuu wa Karume senior na mtoto wa Karume junior. Binti wa Royal Family,

Jiulize vipi kuhusu wengine ambao hawana hiyo protection ya Kifalme

Kwa hiyo Mimi ninawaelewa, watu wengi wana machungu

Japo unalosema kwa mfano, wizi mwingi wa nchi huwa unatumia kalamu na udhaifu wa sheria zilizopo kuiba. Kwa hiyo kuna namna watu flani ilikuwa lazma waumizwe ilo nchi ipige hatua

Lakini huku kwenye makelele, sikuona umuhimu wa kutumia nguvu kubwa sana maana ndio iliozaa uchawa wa kisiasa. Watu kusifu na, kuabudu ili wapewe favour, kitu ambacho kinatughalimu hadi sasa maana kila mtu anaongea vitu vinavyomuweka katika nafasi ya kumfurahisha Rais na kusahau kitu kilicho bora kwa nchi ikiwemo kuongea ukweli unaoumiza.
Hakika.....nikikumbuka eti Ofisi za Imma adv zilitupiwa bomu 🤣🤣🤣🤣
ZIlikuwa ni hasira zisizo za kawaida
 
Unaweza kuniambia kwa nini magufuli alienda kuchukua mikopo kwenye bank ya Exim ambayo ina interests za kibiashara na kuacha nchi za wahisani na mashirika ya fedha za kimataifa yenye riba maalum kwa nchi ??...

Unadhani ni nchi ngapi ziliondoa funds zake kwenye miradi mbalimbali ya serikali na hata NGOs kuja Tanzania ikiwemo USA ambaye alipata guts za kumpiga ban mkuu wa mkoa wa nchi asiingie marekani kwa kuhusishwa na utishiaji wa maisha na uhuru wa watu..

Articles zoteee zipo mtandaoni au unadhani uhusiano wa kidiplomasia ni kuingia katika vita mkuu.

Mbona vitu vipo wazi...

Najua wengi mlimpenda Magufuli kama dini na mnaumia mkisikia kasemwa kwa lolote na hata Mimi kuna baadhi ya vitu naona anaonewa sometimes Ila kuna vitu vingi alivifanya ambavyo vitakuwa doa katika utawala wake kama ambavyo Nyerere na Mkapa walikiri baadae kuwa kuna pahali walikosea. Kwa hiyo hamuwezi kugeuza nyeupe kuwa nyeusi, historia ya Magufuli itamuhukumu kama inavyopasa
uko sahihi pia ukumbuke hayo maswali uliyouliza chanzo chake ni athari zilizotokana na habari walizokuwa wanaandika kina kabendera
 
Unadhan kabendera alifanya ivo kwa faida ya nani? Nani alikuwa nyuma yake? Ingekuwa wewd ndo prezida ungefanya nini? Ukumbuke kabendera anataja mabaya ya magufuli je yeye hana makosa? Kwa nini hasemi na ya kwake, siku zote msema peke hushinda
Kuna mtu alisemwa nchi hii kama Kikwete tena kwa matusi, kuanzia mtaani, wasanii kuimba nyimbo kali kama za Roma na upinzani kukua kwa kasi.

Lakini hadi leo watu wanakumbuka kesi ya Dr Ulimboka na labda Mwangosi.

Vipi kwa Magufuli, kuna mangapi

Nadhani licha ya Magufuli kuwa kiongozi mtendaji mkubwa kiasi cha kufanikisha mengi kwa wakati mfupi lakini hakuwa kiongozi mwenye uvumulivu na ustahimilivu dhidi ya wakosoaji wake. Hakupenda si kutukanwa Ila kukosolewa au kupewa alternatives za kufanya vitu. Alikuwa anaamini zaidi katika maono na akili yake binafsi ndio maana alijizungusha na watu ambao wasingeweza kumuhoji zaidi ya kutekeleza kama makonda.

Ulikuwa ni udhaifu binafsi tu
 
uko sahihi pia ukumbuke hayo maswali uliyouliza chanzo chake ni athari zilizotokana na habari walizokuwa wanaandika kina kabendera
Hapana.. Kina Kabendera walipata vya kuandika kutokana na matendo na kauli za mkuu. Tusiwape watu wengine lawama, tukubaliane na uhalisia wake

Kama ambayo alikuwa yupo vizuri kwa jambo moja, hakuwa katika jambo lingine na ipo sawa
 
Unaweza kuniambia kwa nini magufuli alienda kuchukua mikopo kwenye bank ya Exim ambayo ina interests za kibiashara na kuacha nchi za wahisani na mashirika ya fedha za kimataifa yenye riba maalum kwa nchi ??...

Unadhani ni nchi ngapi ziliondoa funds zake kwenye miradi mbalimbali ya serikali na hata NGOs kuja Tanzania ikiwemo USA ambaye alipata guts za kumpiga ban mkuu wa mkoa wa nchi asiingie marekani kwa kuhusishwa na utishiaji wa maisha na uhuru wa watu..

Articles zoteee zipo mtandaoni au unadhani uhusiano wa kidiplomasia ni kuingia katika vita mkuu.

Mbona vitu vipo wazi...

Najua wengi mlimpenda Magufuli kama dini na mnaumia mkisikia kasemwa kwa lolote na hata Mimi kuna baadhi ya vitu naona anaonewa sometimes Ila kuna vitu vingi alivifanya ambavyo vitakuwa doa katika utawala wake kama ambavyo Nyerere na Mkapa walikiri baadae kuwa kuna pahali walikosea. Kwa hiyo hamuwezi kugeuza nyeupe kuwa nyeusi, historia ya Magufuli itamuhukumu kama inavyopasa
Tanzania ni nchi maskini bado.

This is how it works kuna kinaitwa DeMPA👇

Kuna taratibu zake kabla nchi maskini ujaenda kuchukua mikopo kwenye private banks.

Kwa sababu nyingi, default risks na cash flow yako. Kabla private banks awaja kukopa wanataka kuona income yako na against current current liability.

Na world bank nao wana monitor, bank itakayopa nchi yenye B rating bila ya kuongea na IMF au WB inanunua ugomvi mkubwa wa irresponsible lending kwa kuchezea amana za wateja wao. Waulize Credit Suisse fines walizochezea EU kwa kuikopa Mozambique bila kufuata DeMPA.

Unadhani unakopeshwa tu na private banks, muulize Mwigulu si alienda kutafuta mkopo NY through private banks (Paris Club), huo mkopo alipata.

Hadi ukoposhwe na banks nchi ya third na IMF/WB wakae kimya maana yake cash flow yako ipo vizuri.

Tatizo lenu tunajazana upepo kwenye story zetu sana humu JF na kudhani, that’s how things work.

Magufuli hakuwa wa mzaha-mzaha
 
Back
Top Bottom