jiwe angavu
JF-Expert Member
- Aug 28, 2015
- 20,419
- 39,217
Huo ujinga ulioaminishwa na Mwendazake ni scam.
Tazara bei ni nafuu,wanayotumia huo usafiri vs Mabasi ni wangapi? Hakuna mtu atapanda treni za ubabaishaji za Bongo aache basi hayupo
Nimekwambia Sgr haitakuwa nafuu ni kama BRT na daladala DarAcha upuuzi,kati ya nauli ya treni na basi na ndege,wapi kuna nauli nafuu katika usafirishaji wa raia na mizigo??
Inategemea, baadhi ya nchi basi ndio usafiri nafuu kabisa, huku nchi nyingine treni ndio usafiri nafuu kabisa.Acha upuuzi,kati ya nauli ya treni na basi na ndege,wapi kuna nauli nafuu katika usafirishaji wa raia na mizigo??
Kuna bandiko juu ya nauli zinazopendekezwa za SGR kati ya Dar na Morogoro. Nauli hizo zipo juu sana ni kama mara tatu zaidi ya nauli ya basiNimekwambia Sgr haitakuwa nafuu ni kama BRT na daladala Dar
Hilo li Sgr litaendelea kuwa mwiba hata baada ya kukamilika.Kuna bandiko juu ya nauli zinazopendekezwa za SGR kati ya Dar na Morogoro. Nauli hizo zipo juu sana ni kama mara tatu zaidi ya nauli ya basi
Njia mwafaka ya kusafirisha gesi ni pipeline , hayo mahindi na korosho quantity zivunazwo barabara tosha , reli ile haina umuhimu wowote kwa sasa economically , ni deni tu tunaongezaMikoa inayoongoza Kwa uzalishaji wa mahindi ni Ruvuma,mbeya,Rukwa na uzalishaji wa korosho mtwara na Lindi , bado gesi maendeleo yangekuwepo iwapo miundombinu kama Reli , barabara vingepelekwa sijajua Kwa nini serikali Ina project za mikoa mingine na kusahau kusini na hata viongozi wengi wa kusini sijui Kwa nini wanasahau kwao pamoja na jamii ya kusini Kwa ujumla wakiondoka kwao hawarudi na wakirudi ni Kwa mbinde sana
Sent from my ZTE T1002 using JamiiForums mobile app
Mpunguze uchawi na ushirikinaMikoa inayoongoza Kwa uzalishaji wa mahindi ni Ruvuma,mbeya,Rukwa na uzalishaji wa korosho mtwara na Lindi , bado gesi maendeleo yangekuwepo iwapo miundombinu kama Reli , barabara vingepelekwa sijajua Kwa nini serikali Ina project za mikoa mingine na kusahau kusini na hata viongozi wengi wa kusini sijui Kwa nini wanasahau kwao pamoja na jamii ya kusini Kwa ujumla wakiondoka kwao hawarudi na wakirudi ni Kwa mbinde sana
Sent from my ZTE T1002 using JamiiForums mobile app
Wewe ni muongo wa kutupwa huku kusini watu tuna elimu ndio maana hausikii matendo ya kuuwa vikongwe,kuua albino,mauaji ya visa vya mapenzi nk hii yote ni kutokana na kuelimika kwetu au wewe unadhani dhumuni la elimu ni lipi?, na unapozungumzia miundombinu unataka kuniambia sisi kusini tumezidiwa na wapi? Na ukija kwenye upande wa uchumi wa mtu mmoja mmoja sisi tuna nafuu kubwa mno kwasababu tunalima korosho zao ambalo hata wewe taarifa zake unazoKusini sio elimu
Sio miundombinu
Sio kipato cha mtu mmoja mmoja hakuna nafuu(nimefika nimejionea
Kama huku kuna uchawi mbona hamna mauaji ya vikongwe na albino?Mpunguze uchawi na ushirikina
Nikweli mashamba yalikuwa nachingwea na sio mikindaniReli ilijengwa kutoka bandari ya mikindani mtwara kwenda nachingwea kwenye mashamba ya karanga,mleta mada weka sawa historia yako.
Bahati nzuri huku si kwetu Mimi ni mtu wa Kilimanjaro ila nipo huku mwaka wa 10 sasa uchawi na ushirikina Kila sehemu upo nacho jaribu kutafakariMpunguze uchawi na ushirikina
Kanda zote zimesaulika labda Dar na huko kaskazini kuna upendeleo.Bahati nzuri huku si kwetu Mimi ni mtu wa Kilimanjaro ila nipo huku mwaka wa 10 sasa uchawi na ushirikina Kila sehemu upo nacho jaribu kutafakari
Kielimu kusini ipo nyuma
Kimiundombinu kusini ipo nyuma
Kiuchumi kusini ipo nyuma
Kimaendeleo basi mtu moja mmoja bado pia ipo nyuma
Serikali na viongozi kiujumla mikoa ya kusini wamechukulia mikoa ya adhabu Kuna kipindi teuzi zikifanyika utasikia utaenda sehemu flani upate kujifunza kidogo hii kasumba iondoke na serikali iweke mpango mkakati wa maendeleo Kwa mikoa ya kusini
Sent from my ZTE T1002 using JamiiForums mobile app
Mna elimu wakati maendeleo sifuri tukianza kutafuta shule za mwisho kwa Tanzania bara top 10 kusini inaweza toa shule mpaka 6Wewe ni muongo wa kutupwa huku kusini watu tuna elimu ndio maana hausikii matendo ya kuuwa vikongwe,kuua albino,mauaji ya visa vya mapenzi nk hii yote ni kutokana na kuelimika kwetu au wewe unadhani dhumuni la elimu ni lipi?, na unapozungumzia miundombinu unataka kuniambia sisi kusini tumezidiwa na wapi? Na ukija kwenye upande wa uchumi wa mtu mmoja mmoja sisi tuna nafuu kubwa mno kwasababu tunalima korosho zao ambalo hata wewe taarifa zake unazo
Hapo ndipo unafeli dogo kwahiyo kipimo chako wewe cha elimu ni matokeo ya shule? Mimi watoto wangu wawili na watoto watatu wa dada zangu wapo shule moja inaitwa wenda ipo mbeya huko ndiko wanasoma na hao watoto kwao ni huku kusini je sasa wakishaandika mitihani na matokeo yakatoka watahesabika ni wawapi?na pia kuna shule inaitwa abbey ipo mwena ndanda hapo kuna mchanganyiko wa wanafunzi kutoka mikoa tofauti ya tanzania ila shule ipo mtwaraMna elimu wakati maendeleo sifuri tukianza kutafuta shule za mwisho kwa Tanzania bara top 10 kusini inaweza toa shule mpaka 6
Acha ubishi mzee kusini sio elimu sio miundombinu sio pato la mtummoja moja hali ni tete unabisha nini sasa, elimh nimetoa mfano maana siwezi andika mengiHapo ndipo unafeli dogo kwahiyo kipimo chako wewe cha elimu ni matokeo ya shule? Mimi watoto wangu wawili na watoto watatu wa dada zangu wapo shule moja inaitwa wenda ipo mbeya huko ndiko wanasoma na hao watoto kwao ni huku kusini je sasa wakishaandika mitihani na matokeo yakatoka watahesabika ni wawapi?na pia kuna shule inaitwa abbey ipo mwena ndanda hapo kuna mchanganyiko wa wanafunzi kutoka mikoa tofauti ya tanzania ila shule ipo mtwara
Bhaaa akil zang siziamin aminSaidi chopeka
Wana mtwara tupunguze uchawa. Alizi mnageuza kuwa ngumu
Hauna hata aibu unadanganya hapa eti pato ni teteAcha ubishi mzee kusini sio elimu sio miundombinu sio pato la mtummoja moja hali ni tete unabisha nini sasa, elimh nimetoa mfano maana siwezi andika mengi
Msimuliaji aliniambia kuwa kumbe wazee wa eneo hilo walifikisha ujumbe kwa wanyapara kuwa mzungu asifanye lolote eneo hilo mpaka tambiko la ruhusa ya miungu lifanyike.[emoji419][emoji375]Tanzania huwa haina utaratibu wa kuachia nyaraka za siri zinapofikia umri wa kueksipaya (Declassified)
Kuna mtu mmoja kutoka serikali ya Uingereza alinisimulia kashfa kubwa ambayo ingegharimu sana reputation ya Malkia wa Uingereza. Jambo lenyewe lipo hivi.
Baada ya Vita ya Pili ya dunia, Uingereza iliongeza makoloni yake ambapo Germany East Africa walipewa Uingereza kwa sababu majeshi yao (KAR) waliwafurusha majeshi ya Ujerumani..
Serikali ya Uingereza walibuni mpango wa kutengeneza na kusambaza Ulaya siagi ya karanga. Hivyo waliweka mkakati wa kuanzisha kilimo kikubwa cha karanga kwenye makoloni yake. Tanganyika ilikuwa miongoni mwa makoloni yaliyoteuliwa kuwemo kwenye mradi huo. Maeneo ya Kongwa Dodoma na Mikindani Mtwara yaliwekwa kwenye mkakati huo. Hiki ndo chanzo cha karanga kulimwa kwa wingi Dodoma na ushoroba wa Singida.
Maafisa wasimamizi wa mradi waliletwa nchini miaka ya 1950s. Aliyenisimulia hii issue ni mtoto wa mmoja wa maafisa wa mradi huu ulioitwa GROUNDNUTS SCHEME. Walikuja na kuishi kwenye quarters za gerezani Dar. Kota hizo zilikuja kufanywa makazi ya wafanyakazi wa reli na hatimaye sehemu ya nyumba ndogondogo eneo la Kamata limevunjwa na Serikali kupisha mradi wa BRT na SGR pamoja na Bandari Kavu.
Kongwa mradi ulienda vizuri, reli ya kati iliyokuwa imejengwa na Mjerumani ilisaidia sana kupeleka pembejeo za kilimo. Ikumbukwe serikali ya Uingereza ilifanya mazungumzo na Marekani ikachukua sehemu kubwa ya vifaru vilivyotumika kwenye vita ya pili ya dunia na ikavikarabati na kugeuza matrekta. Ndo ikawa mwanzo wa trekta zenye magurudumu reli (kama ya vifaru) kuwepo.
Kwa Tanzania ofisi za Groundnuts Scheme zilikuwa eneo ambalo kwa sasa ni Ubalozi wa Zambia Dar.
Makao makuu ya Mradi yalikuwa London. Msimuliaji anasema kuwa jengo la huo mradi sasa linamilikiwa na benki ya Standard Chatterd. Na hata wamiliki hawajui whereabouts za mradi huo. M16 imehusika kwa kiasi kikubwa kulifuta jambo hili kwenye vivid history
Mradi huu upande wa Mtwara, ulipelekea hitaji la kujenga reli ya kusini na kuimarisha miundombinu ya usafirishaji ikiwemo mkakati wa kuijenga na kupanua bandari ya Mtwara kwa minajili ya usafirishajiwa karanga Uingereza.
Baada ya hatua za awali za kusafisha eneo la.kilimo kufanyika Mikindani. Ikumbukwe udongo wa maeneo yote ya mradi ulipimwa kitaalam kwenye maabara na kuthibitika unafaa. Eneo hilo likageuka kuwa ardhi ngumu ghafla. Hapo awali udobfo ulikuwa wenye rutubana kitifu safi. Uingereza iliyachukua maeneo hayo bila utaratibu kwani ilikuwa ndoyo mkoloni na ikajimilikisha bila kutafiti shughuli za kibinadamu eneo hilo.
Mikindani na Tandahimba ni maeneo ambayo wakazi wa asili wa maeneo hayo wanadumisha mila za miungu ya Kiafrika (Mshana Jr), hivyo matambiko na maombi kwa miungu na mizimu yalikuwa yanafanyika kwenye mapori ya eneo hilo. Msimuliaji aliniambia kuwa kumbe wazee wa eneo hilo walifikisha ujumbe kwa wanyapara kuwa mzungu asifanye lolote eneo hilo mpaka tambiko la ruhusa ya miungu lifanyike.
Baada ya ardhi kugeuka kuwa ngumu, na hili linatokea kabla hata hawajakamilisha clearance ya shamba hilo. Na zikaanza kutokea ajali za ajabu kama vile matekta kuangukiwa na miti mikubwa, majoka kujaa eneo hilo na kadhalika. Waingereza wakaongeza funding ya mradi kwa kusegment irrigation system ili kuhakikisha ardhi inakuwa tayari kwa kilimo. Lakini haikufaidia. Zilitumia fedha nyingi sana kutoka mfuko wa Malkia. Mamilion ya Pounds yaliteketea
Wakati hayo yanatokea, pale bonde la Rufiji ilianza kulimwa pamba. Pamba ile ilikuwa bora kuliko inayolimwa kanda ya ziwa.
Waingereza walipigwa butwaa na matokeo ya kumwama kuendeleza mradi kule Mikindani. Na mpaka leo mtu anayeenda kutembelea huko atakuta scapers za matrekta na zana za kilimo walizoziacha waingereza.madubwasha hayo yapo porini ndani kabisa. Kuna mzee mmoja (Saidi Chopeka) mpaka mwaka 2008 alikuwepo eneo hilo ambaye wazazi wake walikuwa walinzi wa kambi ya shamba hilo.
Serikali ya Uingereza iliamua kuficha hii failure ili kukwepa kuiingiza familia ya Kifalme kwenye kashfa ya aibu. Na hasa baada ya uhuru walifanya makubaliano na serikali ya Tanzania kww kuipatia (malipo?) Incentives za kuhakikisha kumbukumbu ya mradi wa Mikindani inafichwa. Hivyo baadaye hata kuondolewa kwa reli ya kusini ilisemekana ni katika kuficha ama kufunika kashfa hii.
Kwa nini nayasema.haya sasa.
Mama aliyenisimulia, alinionesha evidences nyingi za kuniridhisha zikiwemo picha na hata alipokuja hapa Tanzania na familia yao yeye alikuwa na umri wa miaka 8. Alikuja kusoma baadaye sekondari ya forodhani. Alinipeleka Kurasini kuonanana Sister (bibi haswaa) aliyekuwa Headmistress wa kwanza wa shule ya Forodhani (St. Joseph) iliyokuwa chini ya kanisa Katoliki.
Aliniomba kwamba endapo itatokea akaaga dunia basi nisimulie mkasa huu kwa jamii yangu wajue namna serikali yao inavyohusika kwa sehemu kwenye kukwamisha maendeleo ya kisekta hususan kuushawishi kufa kwa reli ya kusini.
HITIMISHO
Nimetimiza wajibu