Kwanini Serikali iliamua kununua mabasi ya mwendokasi yenye injini za CUMMINS wakati si imara wala madhubuti?

Si mnakumbuka zenji ndege ilikua inasukumwa kama gari za mchuzi juu?

Mi nahisi hata hizi ndege za magufuli namashaka nazo huwenda waliwekea injini ya pawatila kisha wakaifanyia mod kuifunga kwenye bonet ya ndege
Engine ya ndege ni tofauti sana na ya gari.
 
Joto na masaa havimati...

Mimi nilishakutana na engine ambazo kuzimwa kwake ni wakati wa service tu... Na kuhusu joto la dar ni cha mtoto kwasababu ndani ya engine kuna joto kubwa kuliko so hiyo haiwezi kuwa sababu.
 
Mkuu umemaliza kila kitu au kwa kiswahili cha humu ndani ni kwamba umefunga uzi.
 
Tatizo sio mabasi tatizo ni mfumo mzima wa usafiri ni corrupt. Jiji lenye wakazi karibu milion 10 wanategemea usafiri wa mabasi na daladala au bajaji na bodaboda. Unategemea hayo mabasi ya operete vizuri kweli?

Katika hili Hayati Rais Magufuli kusema kweli alitereza kidogo. Mjini kwote trams zilihitajika na kutoka mjini kwenda vitongoji vingine kama Kibaha, Mkulanga na Bagamoyo kupitia Bunju commuter trains zilitakiwa ziwe zina operate. Mabasi, Daladala, Bajaji na Bodaboda kazi zake ni kuwatoa na kuwaleta watu kutoka kwenye vituo vya trains kutoka vitongoji vidogo

Mji kama Berlin nchini Ujerumani una wakazi milion 4.3 hivi, lakini una usafiri kemkem kama; S-Bahn, Trams, Underground trains, buses na kadhalika. Katika mji wenye milion 7 na ushee usafiru mbona ni kichekesho
 
Nimeshaona engines za CUMMINGS kwenye minara ya simu, hasa airtel, ziliondolewa zote... maana zilileta shida sana... Kuna moja kubwa ilikuwa pale kijitonyama (sayansi jengo la TTCL enzi celtel wapo pale... ni balaa
Ile CUMMINGS ya kule data center ilikuwa ni ya mda mrefu sana mkuu. Na hata kile kidogo kilikuwa pale switch kilikuwa hoi sana. Pale Gen set waliyokuwa wanaitegemea ni ile CAT nafiri pia walinunua likiwa jipya kabisa
 
Ile CUMMINGS ya kule data center ilikuwa ni ya mda mrefu sana mkuu. Na hata kile kidogo kilikuwa pale switch kilikuwa hoi sana. Pale Gen set waliyokuwa wanaitegemea ni ile CAT nafiri pia walinunua likiwa jipya kabisa
Nilikuwepo pale toka inawekwa mbaka inafanya kazi.. Ishanihangaisha vya kutosha.. 500kVA. Achana na zile CAT za kule SWITCH (COeT), huku sayansi... Zile nishasema nazo sana... ILA CUMMINGS KIMEO TU... Hadi kwenye towers ilikuwa shida... KITU YANMAR BWANA
 
halafu leo waziri anaenda kungaka eti kwanini magari mabovu, Buses 56 kati ya 140 zina shida ya gear box bado tu hatuchukui hatua, au tuliuziwa used?
 
Kwa mafundi wengi wa serikali na taasisi service zao ni kufanya replacement ya spare hii na kuweka nyingine.
Kama walinunua gari hazina ubora wangejitahidi katika maintainance yote yangekuwa barabarani.

Hizo basi 56 zilizoharibika hapahapa bongo kuna mafundi mahiri wa hizo injini na gearbox wakipewa zinarudi barabarani kwa muda mfupi.
 
Inashangaza sana hivi kweli wataalamu wetu hawajui mazingira ya engine nyuma huku kwetu?kama yalikuwa zaidi ya 200 means walikuwa na nguvu ya ku-require kutegemeana na mazingira ya kwetu otherwise ni upigaji tu nakumbuka mwanzoni kwenye majaribio basi nililoliona lilikuwa ni brand ya MAN.
 
Tulioneshwa MAN zikaja GOLDEN DRAGON!View attachment 1760001
 

Attachments

  • Bus%20Mwendo%20Kasi%20%40%20Patapicha.PNG
    24.9 KB · Views: 13
Kwa ushauri wako, walitakiwa kuchukua zenye engine gani?
 
Tatizo lenu mnaleta siasa. Kuanzia lini injini za kichina zimekuwa imara?
Angalia mabasi ya Safari ndefu, bodi mchina injini Scania
Na safari fupi wanafunga engine gani?

Au Morrocco - Gerezani ni safari ndefu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…