Kwanini Serikali inaogopa wachunguzi wa Kimataifa?

Kwanini Serikali inaogopa wachunguzi wa Kimataifa?

Lilikuwa jambo la heri sana kuwa hatimaye serikali imeona ni busara kuhusika katika kugharimia matibabu ya mh. Lissu popote kule duniani. Lilikuwa jambo la heri sana sasa kwa vikwazo vyovyote vilivyoko kuwekwa pembeni kuwezesha hili la wadau wote kuchangia ikiwamo serikali kutokea. Ilikuwa ni jambo la heri kubwa kwa pande zinazohusika kuwekeana wepesi katika hili ili kuhakikisha mgonjwa wetu huyu ambaye ni mtanzania mwenzetu kama ambavyo ingekuwa kwa mwingine awaye yote anatendewa haki japo leo yu mahututi hospitalini.

Waswahili wanasema ndugu wawili wakigombana chukua jembe ukalime.

Mh. Lissu hakutendewa haki na waliojaribu kumtoa uhai wake. Mh. Lissu leo hayuko kwenye nafasi ya kujisimamia mwenyewe kuhusiana na hatima ya matibabu yake kwa sasa. Mh. Lissu asiingizwe katika marumbano haya ya kuchangia tiba yake. Hebu sisi kama ndugu tumtangulize mgonjwa wetu mbele dhidi ya maslahi yoyote yale (au ego yoyote ile). Tusimhukumu mgonjwa wetu kwa kuacha kutoa michango yetu kumsaidia wakati angali mzima. Historia isije ikatuhukumu kwa kuendekeza marumbano ya kuhusiana na michango yetu tukimtelekeza mgonjwa wetu wakati tulikuwa katika nafasi ya kuweza kumsaidia akiwa hai. Ya Arabi sisi, tutaziweka wapi nyuso zetu kwa kumtelekeza mgonjwa wetu wakati nafasi hiyo Mnyazi Mungu alitupa kuonesha huruma yetu na bado tukawa hatukufanya hivyo?

Misahafu inasema: "Heri walio na Huruma maana nao watahurumiwa" na pia "Heri wenye mioyo safi maana hao watamwona Mungu".

"Eeeh mola wetu hebu ukatujalie mioyo ya imani tukaweke tofauti zetu pembeni na kukubaliana kuwa suala la muhimu sana lilopo mbele yetu kwa sasa hivi ni kwa mheshimiwa huyu kupata huruma zetu wote kabisa na kwa umoja wetu na tukamtendee haki kuwa kuhakikisha pesa kuhusiana na tiba yake zipo bila ya kujali nani katoa nini (be it serikali, watu binafsi nk) kwani kutoa ni moyo na si utajiri."

Kimsingi lingekuwa ni jambo la faraja kubwa mno hata kwa mgonjwa wetu kwa serikali kuchukua jukumu kubwa zaidi katika kuhakikisha kuwa hakuna upungufu wa rasilimali katika tiba zake kulingana na madaktari wake huko aliko wanavyoshauri. Hii ni kama ambavyo serikali imekuwa ikifanya kwa wagonjwa wake kwenye hali tete kama hizi za kupigania maisha na hasa uwezekano wa full recovery unapokuwapo.

Baada ya utangulizi huu narejea katika hoja yangu ya leo:

Limekuwa jambo la kujiuliza hasa kuhusiana na kauli ya Mh. Jaji mkuu ya kutohitaji msaada wowote kwenye uchunguzi wa tukio la shambulizi la mh. Lissu.

Ninadhani hapa kinachogomba si msaada bali kuna hali ya kutoaminiana jambo ambalo haliwezi kuondoshwa kwa kukanusha tu kuwa fulani hakuhusika. Kwenye matukio tata kama haya kwa kawaida kumekuwa na matumizi ya chunguzi tofauti na zile za kawaida zilizozoeleka wanazofanya polisi. Serikali au vyombo vyake vinapotuhumiwa kuhusika hapo panakuwa na hali ya kutokuaminiana.

Kulikuwa na issue ya kuuwawa wachimba madini wa Ifakara ambapo kuliundwa na tume ya Jaji Kipenka. Kulikuwa na case za Richmond kulikuwa na tume iliundwa kuchunguza mambo ya Richmond nk nk. Yote haya yakiwa na nia njema ya kuhakikisha kuwa ukweli na ukweli peke yake unawekwa wazi pasipokuwa na pingamizi lolote. Ninaamini tume zote hizi zimekuwa na access ya resources zote ndani na nje ya nchi katika kuhakikisha kuwa ukweli unapatikana down to the ground.

Kwa nini serikali inaona ugumu kwenye kuhakikisha kama ilivyokuwa kwa wafanya biashara wa madini Ifakara, Richmond, au kama ilivyokuwa kwa case za kina Ouko na kina Saitoti Kenya sote kabisa pasipo na kujali tuko upande upi katika kadhia hili tunapata kujiridhisha ni nani kabisa na kwa nini walikuwa nyuma ya tukio hili ili wakatiwa adabu vilivyo bila kujali nyadhifa zao katika kuhakikisha matukio kama haya hayajitokezi tena?

Kwa maslahi ya nani tunaogopa au kupinga uchunguzi huru hata kama utahusisha agencies zozote za nje kutusaidia?

Mbona tunasaidiwa katika nyanja nyingi tu na hata katika kujenga "Fly Overs"?
 
Vyombo vya ulinzi na usalama vya serikali ndio wahusika wakuu wa tukio la kutaka kumuua TL.
 
Bila ya uchunguzi huru, serikali itabakia kuwa mshukiwa milele hata wakamatwe watu fulani fulani na kufikishwa mahakamani.
 
Jaji mkuu mjue ni mtu wa kanda ya ziwa kama alivyo mkuu wa JW, AG, DPP, master GVT cashier, IGPI, etc. Nchi imepatwa.
 
Habari wakuu,,,,

Rais Alituambia Alikesha Ili Kuteua Wasaidizi Wake, Kwa Akili Hizi Ni Heri Rais Wetu Angelala Tu !!

Msemaji wa serikali.

1.Kunapotokea kosa la jinai iwe dhidi ya mwanasiasa au raia wa kawaida busara ni kuviachia vyombo vya dola vifanye kazi yao kwanza.

2.Kutuhumiana bila msingi kunaweza kutufikisha mahali tukaona kuwa hata wewe unayetuhumu wenzio kumbe ni mtuhumiwa namba 1.

3.Waje wazungu?Wamekufa watu wangapi Kibiti hatukuita wazungu?Lakini hatujui pia hata hao wazungu kwao makosa ya jinai pia yamewazidi nguvu?

ALLY SALUM HAPI

Watu wasio na hatia walikua wanauawa Kibiti.Ila hamkupaza sauti za michango wala kudai uchunguzi wa kimataifa.Shame!


Hayo ni mawazo ya viongozi wetu

Majibu yangu kwa ally salum hapi

Wewe uliwachangia wanakibiti? Kinachokukera wenzio kuchangiwa ni nini? Wewe ni kiongozi, chagua aina ya chuki ya kuionesha. Chuki hii mbaya!

Hii ishu ya Lisu inahusiana nn na Kibiti. Mlitaka kibiti tuwachangie nn na walikua wanauwawa? Kuna aliekua hosp hoi? Mbona kama mnajitetea.

Majibu yangu kwa msemaji wa serikali.

Ni Lini Vyombo Vya Dola Vilileta Majibu Ya Kazi Tuliyowaachia Waifanye? Kubenea? Kibanda? Ulimboka? Ben Saanane? ROMA? Mawazo? LINI?

Yaani Raia Watuhumu na Serikali Nayo Ituhumu? Kwanini Msichukue HATUA? Hivi Mnajielewa Kweli Nyie?

Hao Wazungu Wakija Mtapoteza Nini? Mbona Mliwaita Kwenye Swala La Mapadri ZNZ? Leo Mnaogopa Nini? NIMEKUMBUKA The Guilty are Always Afraid !



Kama Bado Unaamini Polisi Watawakamata Watu Waliomshambulia Tundu Lissu Basi Sehemu Yoyote Utakaposikia Neno MPUMBAVU Simama Na Useme NIPOO.

mr mkiki.
 
Huyu Jamaal mshika pua anatupoteza watanzania 2020 hata Kwa njia ya mbada Maxima apogee Tu nje sender sale chatu Niko



Swissme
 
Maumiv ya kichwa huanaza pole poleeee...unajiskia maumivu makaali kupita kiasi...
Hebu malizia lile tangazo la kipind cha wahenga.
 
Kuna uchunguzi BADO Dr ulimboka kuna kibanda kuna Roma kuna Ben sanane kuna nape atuoni mnachokifana zaidi ya kupendezea kodi zetu
 
Habari wakuu,,,,

Rais Alituambia Alikesha Ili Kuteua Wasaidizi Wake, Kwa Akili Hizi Ni Heri Rais Wetu Angelala Tu !!

Msemaji wa serikali.

1.Kunapotokea kosa la jinai iwe dhidi ya mwanasiasa au raia wa kawaida busara ni kuviachia vyombo vya dola vifanye kazi yao kwanza.

2.Kutuhumiana bila msingi kunaweza kutufikisha mahali tukaona kuwa hata wewe unayetuhumu wenzio kumbe ni mtuhumiwa namba 1.

3.Waje wazungu?Wamekufa watu wangapi Kibiti hatukuita wazungu?Lakini hatujui pia hata hao wazungu kwao makosa ya jinai pia yamewazidi nguvu?

ALLY SALUM HAPI

Watu wasio na hatia walikua wanauawa Kibiti.Ila hamkupaza sauti za michango wala kudai uchunguzi wa kimataifa.Shame!


Hayo ni mawazo ya viongozi wetu

Majibu yangu kwa ally salum hapi

Wewe uliwachangia wanakibiti? Kinachokukera wenzio kuchangiwa ni nini? Wewe ni kiongozi, chagua aina ya chuki ya kuionesha. Chuki hii mbaya!

Hii ishu ya Lisu inahusiana nn na Kibiti. Mlitaka kibiti tuwachangie nn na walikua wanauwawa? Kuna aliekua hosp hoi? Mbona kama mnajitetea.

Majibu yangu kwa msemaji wa serikali.

Ni Lini Vyombo Vya Dola Vilileta Majibu Ya Kazi Tuliyowaachia Waifanye? Kubenea? Kibanda? Ulimboka? Ben Saanane? ROMA? Mawazo? LINI?

Yaani Raia Watuhumu na Serikali Nayo Ituhumu? Kwanini Msichukue HATUA? Hivi Mnajielewa Kweli Nyie?

Hao Wazungu Wakija Mtapoteza Nini? Mbona Mliwaita Kwenye Swala La Mapadri ZNZ? Leo Mnaogopa Nini? NIMEKUMBUKA The Guilty are Always Afraid !



Kama Bado Unaamini Polisi Watawakamata Watu Waliomshambulia Tundu Lissu Basi Sehemu Yoyote Utakaposikia Neno MPUMBAVU Simama Na Useme NIPOO.

mr mkiki.
Hahaha kuna ded mmoja huko mafia bwana erick mapunda yeye ndio ananunua kila kitu cha halmashauri. Cement kanunua yeye, mbao yeye, kashonesha manesi na madr nguo bila.kufuata taratibu za manunuzi! Kampa kimada wake pesa taslimu ts4. 5 ml at wakachimbe bwawa la maonesho ya 88.
Sasa unajiuliza hivi raisi alipokuwa anakesha na kuwatafuta hawa kina erick mapunda wa mafia alikuwa anaangalia vigezo vya nani fisadi zaidi ya mwenzie ama?
 
Habari wakuu,,,,

Rais Alituambia Alikesha Ili Kuteua Wasaidizi Wake, Kwa Akili Hizi Ni Heri Rais Wetu Angelala Tu !!

Msemaji wa serikali.

1.Kunapotokea kosa la jinai iwe dhidi ya mwanasiasa au raia wa kawaida busara ni kuviachia vyombo vya dola vifanye kazi yao kwanza.

2.Kutuhumiana bila msingi kunaweza kutufikisha mahali tukaona kuwa hata wewe unayetuhumu wenzio kumbe ni mtuhumiwa namba 1.

3.Waje wazungu?Wamekufa watu wangapi Kibiti hatukuita wazungu?Lakini hatujui pia hata hao wazungu kwao makosa ya jinai pia yamewazidi nguvu?

ALLY SALUM HAPI

Watu wasio na hatia walikua wanauawa Kibiti.Ila hamkupaza sauti za michango wala kudai uchunguzi wa kimataifa.Shame!


Hayo ni mawazo ya viongozi wetu

Majibu yangu kwa ally salum hapi

Wewe uliwachangia wanakibiti? Kinachokukera wenzio kuchangiwa ni nini? Wewe ni kiongozi, chagua aina ya chuki ya kuionesha. Chuki hii mbaya!

Hii ishu ya Lisu inahusiana nn na Kibiti. Mlitaka kibiti tuwachangie nn na walikua wanauwawa? Kuna aliekua hosp hoi? Mbona kama mnajitetea.

Majibu yangu kwa msemaji wa serikali.

Ni Lini Vyombo Vya Dola Vilileta Majibu Ya Kazi Tuliyowaachia Waifanye? Kubenea? Kibanda? Ulimboka? Ben Saanane? ROMA? Mawazo? LINI?

Yaani Raia Watuhumu na Serikali Nayo Ituhumu? Kwanini Msichukue HATUA? Hivi Mnajielewa Kweli Nyie?

Hao Wazungu Wakija Mtapoteza Nini? Mbona Mliwaita Kwenye Swala La Mapadri ZNZ? Leo Mnaogopa Nini? NIMEKUMBUKA The Guilty are Always Afraid !



Kama Bado Unaamini Polisi Watawakamata Watu Waliomshambulia Tundu Lissu Basi Sehemu Yoyote Utakaposikia Neno MPUMBAVU Simama Na Useme NIPOO.

mr mkiki.
Ww ni miongoni mwa Member wanaowafanya watz wengi wafunguke macho, akili na ufahamu....asante kuwajuza "walevi hao wa madaraka"
 
Back
Top Bottom