Kwanini serikali isiwachukue hawa vichaa wanaozagaa mitaani na kuwaweka kwenye makempu kwa ajili ya kuwahudumia na kuwatibia

Matibabu n buree mengine ndugu zao
Wapi wanatibu kichaa bure? Kusingekuwa na machizi kuzagaa mtaani kiasi hiki matibabu yao ni gharama sana hasa kwa hospital za uhakika
 
Wapi wanatibu kichaa bure? Kusingekuwa na machizi kuzagaa mtaani kiasi hiki matibabu yao ni gharama sana hasa kwa hospital za uhakika
Mkuu muhimbil /mloganzila , au wameach ckuhz?
 
Bongo nuksi sana
Noma mkuu hili kundi serikali linawachukulia kama wafu wakati ni watu hai kabisa yaani haionekani hata ikiweka jitihada kwenye tiba wala harambee yeyote tofauti na makundi mengine ya ulemavu
 
ok,ok,okay
 
kIukwel serikal ingefanya kitu,kuna mmoja huwa namuona mtaan kila mara siku moja nikamuona kwenye mtaro usiku kalala nilisikitika sana
Kama jamii tuwasaidie,kama hapo ungeanza wewe na mwingine akipokea na mwingine...hao wa Serikali wangefanya kama wewe tu kusikitika na kusepa.
 
Kama jamii tuwasaidie,kama hapo ungeanza wewe na mwingine akipokea na mwingine...hao wa Serikali wangefanya kama wewe tu kusikitika na kusepa.
Serikali ina wajibu wa kuwasaidia hao watu kwani wanakusanya mapato kutoka kwao na si kwa huruma kam unavyosema

Raia wa kawaida zake ni huruma tu kwani vyanzo vya mapato yake havitokani na huyo mtu jua kutofautisha
 
Wazo zuri, ila nadhani mirembe ipo kwa kazi hiyo
 
Milembe vichaa wanatibiwa bure na kupewa huduma za chakula bure?
 
Dkt. Gwajima D anaweza kutupa jibu ya hili swali.
Hujambo? Heri ya Mwaka mpya.

Watu wengi bado wanazichanganya Wizara mbalimbali na Makundi yake maalumu. Haya maoni mazuri humu mngewasilisha moja kwa moja kwenye Wizara mahsusi ya kundi la watu wenye ulemavu ambayo inaitwa, Wizara ya Kazi Ajira Vijana na watu wenye Ulemavu, Iko ofisi ya Waziri Mkuu. Hivyo, maoni haya mazuri yangejumuishwa kwenye mikakati rasmi ya masuala ya wenye ulemavu kwenye Wizara hii mahsusi tafadhali.

Ahsante Sana
 
Na mimi nalisubiria kwa hamu!
Hujambo? Heri ya Mwaka mpya.

Watu wengi bado wanazichanganya Wizara mbalimbali na Makundi yake maalumu. Haya maoni mazuri humu mngewasilisha moja kwa moja kwenye Wizara mahsusi ya kundi la watu wenye ulemavu ambayo inaitwa, Wizara ya Kazi Ajira Vijana na watu wenye Ulemavu, Iko ofisi ya Waziri Mkuu. Hivyo, maoni haya mazuri yangejumuishwa kwenye mikakati rasmi ya masuala ya wenye ulemavu kwenye Wizara hii mahsusi tafadhali.

Ahsante
Sana
 
Ni kweli mama etu aje atupe matumaini kwa hawa watu hakika wanateseka wengi wao wametelekezwa na ndugu zao wanaishi kama wafu angali wako hai
Hujambo? Heri ya Mwaka mpya.

Watu wengi bado wanazichanganya Wizara mbalimbali na Makundi yake maalumu. Haya maoni mazuri humu mngewasilisha moja kwa moja kwenye Wizara mahsusi ya kundi la watu wenye ulemavu ambayo inaitwa, Wizara ya Kazi Ajira Vijana na watu wenye Ulemavu, Iko ofisi ya Waziri Mkuu. Hivyo, maoni haya mazuri yangejumuishwa kwenye mikakati rasmi ya masuala ya wenye ulemavu kwenye Wizara hii mahsusi tafadhali.

Ahsante Sana
 
Asante kwa ufafanuzi mheshimiwa. Tatizo hao wengine ni vigumu kuwapata sio kama wewe.
Tunapendekeza uwe waziri mkuu maana umekuwa mwepesi kurespond maoni ya wananchi kwa haraka. Mungu akulinde dada yangu.
 
Sijui Wizara ya Jinsia na Mandeleo ya Jamii inafanyaga kazi gani?
Maana hili lilipaswa kuwa moja ya majukumu yake. Hakukupaswa kuwa na wagonjwa wa akili mtaani, wala wazee, wala ombaomba wala watoto wa mtaani.
Wote wanapaswa kukusanywa na kuwekwa mahali pa kuishi.
Wale ambao wanaweza kufanya kazi, wafanye huku wakiwa hapo hapo kambini kama wakiamua kuwaweka kambini
 
Asante kwa ufafanuzi mheshimiwa. Tatizo hao wengine ni vigumu kuwapata sio kama wewe.
Tunapendekeza uwe waziri mkuu maana umekuwa mwepesi kurespond maoni ya wananchi kwa haraka. Mungu akulinde dada yangu.
Wanazo akaunti online wanapatikana,
Inafanya kazi nyingine nyingi tu ambazo hazifanywi na wizara zingine kwa mujibu wa instrument ya kuundwa kwake. Kwa uelewa zaidi, download hotuba yake ya bajeti bungeni Iko online. Kama una maoni, unawasilisha tu serikalini kwa kadri ya utakavyoona inafaa tafadhali.

Heri ya Mwaka mpya
 
Ahsante Mh. Kwa majibu haya mazuri natumaini Dr. Ndarichako waziri mwenye dhamana atalisikia hili

Lakini naimani hata wewe pia limekugusa kwa namna moja au nyingine tunaomba tufikishie ujumbe kwenye wizara husika kama mdau wa jamii forum tutashukuru sana hakika hawa watu hawana mtetezi zaidi ya kuteseka mitaani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…