Kwanini sijaonekana kwenye picha za Iftar ya Ikulu siku ya Jana. Nimechukia sana

Kwanini sijaonekana kwenye picha za Iftar ya Ikulu siku ya Jana. Nimechukia sana

Hata mimi roho imeniuma sana
Picha zote za jana sijaonekana kabisa.
Labda pozi nililokaa ndio lenye utata
 
Kwema Wakuu!

Sisi wengine ni Watu wa misifa, Watu wa mitandaoni, Watu wa kujionyesha, Watu wa kujimwambafai tukio kama la jana kwangu lingeniongezea Credit muhimu sana.

Kutokuonekana inamaamisha sikuwepo ama? Kutokuonekana kwenye picha yoyote au video yoyote ya tukio inamaanisha sikuhudhuria ama! Wachukua Kamera mnieleze kwa nini hamkunichukua kwenye Rekodi? Why? Kwamba hamkuniona Ama! Kwamba hamkutaka Watu ambao hawakuhudhuria wasijue nilialikwa Ama!

Kwa ambao hamkuwepo, nilivalia Kanzu yangu safi kabisa ambayo niliinunua Pale Magomeni, mahususi kwaajili ya mwaliko wa heshima wa Iftar. Ilikuwa Kanzu ya Kahawia yenye udarizi mweusi kwenye Kola na sehemu ya vifungo ingawaje haikuwa na vifungo.

Nilinunua pia Sendo nzuri ambazo muuzaji alinijuza zimetokea Uturuki. Kichwani nikanyoa vizuri. Ni kweli nilipendeza na nilifanania mwaliko wa Ikulu.

Nisingepanda Daladala kwa namna ile. Nilikuwa nimependeza na ninanukia marashi mazuri na manukato ya mafuta aghali. Nikachukua Bolt, huyo mpaka kwenye mwaliko.

Kukata Stori isiwe ndefu kwani bado nina Kwikwi za hasira. Vile nimependeza, vile nilivyokuwa natembea kitasha, vile nilivyokuwa nimebeba chakula na ninakula chakula kidizaini na kistaa hivi hakuna mchukua kamera yeyote aliyenibahatisha kuniona?

Humu mtandaoni Watu watahitaji ushahidi. Kule nako sikuruhusiwa kuchukua Kamera. Sasa nitatamba vipi ndugu zanguni? Inamaana hapa sina tofauti na mtu ambaye hakupata Mwaliko.

Mwenye picha yangu nikiwa kwenye mwaliko tafadhali ninaomba. Masuala ya kusema tulikutana wenye uwezo kwenye Iftar na iftar inatakiwa Watu wasio na uwezo hayo tuachane nayo kwanza.

Taikon wa Fasihi
Dar es Salaam
Kwanza Twambie Yale Magari ulishapeleka Ripoti?
 
Mi pia nilikuwepo ila watu wote walikua hawanijui nikiwasogelea wananiona naharibu stori zao nikaenda kukaa karibu na jokoni
Harafu hii huwa inatokea ukienda Sherehe za watu wazito ukiamini na wewe unajulikana.

Maajabu sasa unaona watu hawakupi umuhimu wowote.
 
Wewe !!

Haukua mwaliko ule, Bali walikua na mambo yao ambayo uwepo wenu nyie ungesaidia plan kufanikiwa!

Shukuru mungu hukuonekana kwa video shukuru sana! hujui motive behind ya mwaliko wenyewe!!

Mialiko kama hii ndio huzua vilio vya kudumu Kwa baadhi ya watu!!

Nikuulize, Mzee wa kutabasamu alikuwepo!!?
 
Kwema Wakuu!

Sisi wengine ni Watu wa misifa, Watu wa mitandaoni, Watu wa kujionyesha, Watu wa kujimwambafai tukio kama la jana kwangu lingeniongezea Credit muhimu sana.

Kutokuonekana inamaamisha sikuwepo ama? Kutokuonekana kwenye picha yoyote au video yoyote ya tukio inamaanisha sikuhudhuria ama! Wachukua Kamera mnieleze kwa nini hamkunichukua kwenye Rekodi? Why? Kwamba hamkuniona Ama! Kwamba hamkutaka Watu ambao hawakuhudhuria wasijue nilialikwa Ama!

Kwa ambao hamkuwepo, nilivalia Kanzu yangu safi kabisa ambayo niliinunua Pale Magomeni, mahususi kwaajili ya mwaliko wa heshima wa Iftar. Ilikuwa Kanzu ya Kahawia yenye udarizi mweusi kwenye Kola na sehemu ya vifungo ingawaje haikuwa na vifungo.

Nilinunua pia Sendo nzuri ambazo muuzaji alinijuza zimetokea Uturuki. Kichwani nikanyoa vizuri. Ni kweli nilipendeza na nilifanania mwaliko wa Ikulu.

Nisingepanda Daladala kwa namna ile. Nilikuwa nimependeza na ninanukia marashi mazuri na manukato ya mafuta aghali. Nikachukua Bolt, huyo mpaka kwenye mwaliko.

Kukata Stori isiwe ndefu kwani bado nina Kwikwi za hasira. Vile nimependeza, vile nilivyokuwa natembea kitasha, vile nilivyokuwa nimebeba chakula na ninakula chakula kidizaini na kistaa hivi hakuna mchukua kamera yeyote aliyenibahatisha kuniona?

Humu mtandaoni Watu watahitaji ushahidi. Kule nako sikuruhusiwa kuchukua Kamera. Sasa nitatamba vipi ndugu zanguni? Inamaana hapa sina tofauti na mtu ambaye hakupata Mwaliko.

Mwenye picha yangu nikiwa kwenye mwaliko tafadhali ninaomba. Masuala ya kusema tulikutana wenye uwezo kwenye Iftar na iftar inatakiwa Watu wasio na uwezo hayo tuachane nayo kwanza.

Taikon wa Fasihi
Dar es Salaam
Ukiona hivyo ujue huna umuhimu, huna "impact"!
 
Amkaaa
FB_IMG_1700191791808.jpg
 
Nimemuelewa mwandishi hasa ni paragraph ya mwisho ndio iliyobeba ujumbe , any way pengine hao watu ambao wengi tulitegemea kualikwa wakaalikwa mwisho bado siku 29
 
Hongera kwa mualiko ulioupata wa iftar ikulu....Nyinyi ni watoto wa mama kizimkazi ,na hapa ipo ,ukihitajika utaitwa tena.
 
🤣🤣🤣kwani we ni chawa wa mama?
Wameonekana mainfluenza 🤣wanaomuhakikishia kizmkaz kushinda uchaguz 2025
We walikuona kama maskini wengine ambao hawakualikwa AU
Walidhani umepewa kadi ya mwalikwa aliyepata udhuru🤣🤣
Ongeza kulamba maka.li.o utaonekana soon
 
🤣🤣🤣kwani we ni chawa wa mama?
Wameonekana mainfluenza 🤣wanaomuhakikishia kizmkaz kushinda uchaguz 2025
We walikuona kama maskini wengine ambao hawakualikwa AU
Walidhani umepewa kadi ya mwalikwa aliyepata udhuru🤣🤣
Ongeza kulamba maka.li.o utaonekana soon

😂😂
Daah! Walimwengu bhana.
 
Back
Top Bottom