Mimi wa kwanza!
Ngoja nijaliwa kwa uelewa wangu.
Mbongo {African}siyo mweusi tu bali yeyote anaweza kuwa muafika.
Kuhusu rangi nyeusi isikupe shida ni Nature yenyewe ikumbukwe hili bara linapata jua kamili hivyo kuwa weusi nikwasababu ya ngozi iweze kuhimili miale mibaya ya jua {mawazo yangu}
Halafu bara letu ni zuri kuliko huko unakokusifia sisi hatuna mavimbunga sijui yakutisha, masunami,matetemeko,mavolcano hata kama yapo lakini siyo kama wao.
Pia kuhusu kutawaliwa na weupe ni sawa hii inaitwa kutesa kwa zamu hata sisi tulishawahi kuwatawala ila sema ilifichwa na hao hao kuogopa aibu,
Kuna mtu alikuwa anaitwa Malkia wa Sheba,kuna hawa jamaa Mafarau wa misri,inasemekana walikuwa weusi kabisa na hii ijulikana kupitia ugunduzi wa ile miili kufukuliwa kwenye makabuli huko Cairo na kukuta jamaa ni weusi tii.
Ngoja waje wataalam wakupe mkuu.