Kwanini Tanzania Walimu wenye Masters hawatambuliwi kimasilahi?

Kwanini Tanzania Walimu wenye Masters hawatambuliwi kimasilahi?

Hivi kukagua shule ina vyoo vingapi,madarasa mangapi, mwalimu kafundisha vipindi vingapi diploma haitoshi?
Msilinganishe ualimu ns uinjinia, ili mtu adizaini daraja la fly over inabidi afanye mahesabu mazito. Ualimu unahitaji elimu ndogo tu hata digrii ni kubwa sana lsbda vyuoni huko.
Kweli network hapa ni not reachable

Sawa kiongozi umeeleweka
 
Nyie mnaosema Maafisa wanaogopa walimu wenye masters watawapora vyeo vyao... Mnitajie wapi huko Afisa elimu wilaya au hata Afisa taaluma amewahi pokonywa cheo na mwalimu mwenye Masters au PhD..?
Serikali karibia zote Duniani zinaajiri mtu na zinalipa mshahara na kutambua elimu kuanzia Certificate mpaka Degree...
Masters ni added advantage ikitokea nafasi fulani inahitaji mtu mwenye Masters ndipo anaangaliwa mtumish mwenye uwezo wa kuimudu nafas hiyo na elimu yake ya masters... Duniani kote Masters ni managerial course inayomuandaa mtu kuwa kiongoz...
 
Habari.

Kwasasa dunia inafanya mapitio ya mitaala ya kufundshia/kujifunza huko mashuleni, huku swala la elimu za walimu ambao ndio wadau wa mitaala hiyo likiwa gizani. Kwa mfano, kwa Tanzania muundo wa kiutumishi wa walimu wa shule za msingi na sekondari unaanzia elimu ya cheti hadi shahada ya kwanza tu, ambapo mwalimu akiwa na shahada ya pili (masters/PhD), mfumo haumtambui kimasilahi na kimuundo, tofauti na nchi zingine kama Kenya, South Africa, Nigeria, Zimbabwe na kwingineko.

Serikali ingelitazama hili swala kwa jicho la utatu kwa kuwaandalia muundo wa kiutumishi na kimasilahi walimu wenye shahada ya pili (masters/PhD) waliopo huko mashuleni. Ifikie kipindi sasa iwe ni kawaida kumwona mwalimu mwenye PhD anafundsha shule za msingi huko. Hii ishu italeta mapinduzi makubwa sana kwenye idara ya elimu na ualimu hasa huko mashuleni, tofauti na sasa ambapo mwalimu akishapata shahada ya pili tu huanza kuomba kuhamia idara zingine ambapo anaona atapata maslahi kulingana na elimu aliyonayo. Wakati huo elimu yake (masters/PhD) ingetambulika kimuundo na kimasilahi, angepata utulivu kituoni pale alipokuwa anafundisha bila kutafuta fursa mahali pengine.

Napenda kuwasilisha.
Masters inaongeza tija gani kwenye kufundisha shule ya msingi na sekondari.

Kwa kada zingine kama madaktari, inaongeza tija kwa kwa maana unaanza kutoa huduma za kibingwa (specialist).

So onyesheni tija kwanza sio makaratasi.
 
Habari.

Kwasasa dunia inafanya mapitio ya mitaala ya kufundshia/kujifunza huko mashuleni, huku swala la elimu za walimu ambao ndio wadau wa mitaala hiyo likiwa gizani. Kwa mfano, kwa Tanzania muundo wa kiutumishi wa walimu wa shule za msingi na sekondari unaanzia elimu ya cheti hadi shahada ya kwanza tu, ambapo mwalimu akiwa na shahada ya pili (masters/PhD), mfumo haumtambui kimasilahi na kimuundo, tofauti na nchi zingine kama Kenya, South Africa, Nigeria, Zimbabwe na kwingineko.

Serikali ingelitazama hili swala kwa jicho la utatu kwa kuwaandalia muundo wa kiutumishi na kimasilahi walimu wenye shahada ya pili (masters/PhD) waliopo huko mashuleni. Ifikie kipindi sasa iwe ni kawaida kumwona mwalimu mwenye PhD anafundsha shule za msingi huko. Hii ishu italeta mapinduzi makubwa sana kwenye idara ya elimu na ualimu hasa huko mashuleni, tofauti na sasa ambapo mwalimu akishapata shahada ya pili tu huanza kuomba kuhamia idara zingine ambapo anaona atapata maslahi kulingana na elimu aliyonayo. Wakati huo elimu yake (masters/PhD) ingetambulika kimuundo na kimasilahi, angepata utulivu kituoni pale alipokuwa anafundisha bila kutafuta fursa mahali pengine.

Napenda kuwasilisha.
Kwetu jambo hili haliko vizuri kabisa. Linawakatisha tamaa vijana wetu.
Mwalimu wa akihitimu master degree anaongezewa vidato viwili tu mf TGTS F1 TO TGTS F3; wakati muundo wa kazi unabaki ule ule.
Huu ni upuuzi kabisa.
Huenda walioko huko juu wanawaogopa hawa vijana wasomi.
 
Masters inaongeza tija gani kwenye kufundisha shule ya msingi na sekondari.

Kwa kada zingine kama madaktari, inaongeza tija kwa kwa maana unaanza kutoa huduma za kibingwa (specialist).

So onyesheni tija kwanza sio makaratasi.
Kwani degree inaongeza tija gani kwenye kufundsha msingi na sek. Tuanzie hapo ili tupate jibu la swali lako
 
Nyie mnaosema Maafisa wanaogopa walimu wenye masters watawapora vyeo vyao... Mnitajie wapi huko Afisa elimu wilaya au hata Afisa taaluma amewahi pokonywa cheo na mwalimu mwenye Masters au PhD..?
Serikali karibia zote Duniani zinaajiri mtu na zinalipa mshahara na kutambua elimu kuanzia Certificate mpaka Degree...
Masters ni added advantage ikitokea nafasi fulani inahitaji mtu mwenye Masters ndipo anaangaliwa mtumish mwenye uwezo wa kuimudu nafas hiyo na elimu yake ya masters... Duniani kote Masters ni managerial course inayomuandaa mtu kuwa kiongoz...
Unaongea tu hebu jaribu kujiridhisha na hoja zako usitumie uzoefu kujibu hoja hivi unajua miaka ya nyuma kidogo hapa Tz hata degree yenyewe ilikuwa haitambuliki, usiseme serikali zote Duniani hazitambui Masters si kweli hebu jaribu kugoogle nchi zifuatazo.. Uganda, Kenya, Zimbabwe, Nigeria, south Africa, zambia...huko mtu kuwa mwl ni Kama ilivyo Tz kwa mtu kuwa mhadhri, nafas zinatangazwa na watu Wana wafanyiwa interview na kila Elimu Ina Mshahara wake kasoro tu kwenye hzo nchi certificate haitambuliki
 
Chukua takwimu vyuoni.
Master za Ed pekee zinazidi 3000 kwa mwaka.
Mara miaka 5. Na wanaosoma ni vijana.
Wapo wengi value yao ishashuka.
Vijana watafute njia nyingine ya kutokea maisha
Wakati CPA Kwa Mwaka hazizidi 500, advocates Kwa mwaka 600
 
Back
Top Bottom