Kwanini tuangaishane na michango ya harusi na tujitaabishe kwa kukusanya pesa za michango. Mbona shughuli ndogo kwa pesa yako mfukoni inawezekana

Eli Cohen

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2023
Posts
4,460
Reaction score
13,715
Africans, we are poor, lakini we are acting rich.

Kwamba unaogopa kusemwa?
Unaogopa kuitwa masikini?
Unaogopa lawama za kutoarika watu?
Unaogopa kutoendana na mila tulizozizoea?

Au ndio njia mbadala ya kupatia pesa za michango kujiboost maisha kidogo?

Muda mwingine hadi tunageuka kero pale tunapokuwa tunapigia simu ndugu na jamaa lakini bado tumo tu.

Labda nikitolea mfano wazungu utasema nimeenda mbali mno basi Siku moja uje ufungue TV uangalie harusi za ndugu zetu wakenya jinsi zilivyo simple.

 
Hujalazimishwa kutoa hiyo pesa.
 
Huu ni uharibifu wa pesa na muda na kutafuta lawama.Kama umependana na mwenzako nenda kwa viongozi wakufungishe ndoa.Sio lazima sherehe.Tunaendekeza mambo ya ajabu tunaacha ya msingi.Ndoa siyo sherehe,tuzingatie mambo ya muhimu kuwaza maisha baada kufunga ndoa.Ila kama una pesa waite wenye pesa wenzako wakuchangie sio unatuunga kwenye grouup kila anayekusalimia.
 
Hakika mkuu
 
Ni fasheni tu kuigana matumizi ya fedha. Tena umezuka mtindo mpya wa kufungashiwa vyakula na vinywaji ukumbini, utajua mwenyewe ule na unywe hapo hapo ukumbini au ukalie nyumbani. Kuna misosi ya awali na ya mwisho maarufu kama bufee. Kabla ya bufee unakuwa umeshiba vyakula vya awali hivyo basi itabidi uondoke ukumbini na fuko la chakula cha awali au uache kama mabaki. Ukipiga hesabu ya msosi na vinywaji inakaribiana na mchango uliotoa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…