Kwanini tunalazimishwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuwa tupo Awamu ya Sita wakati Kiuhalisia bado tupo Muhula wa Pili wa Awamu ya Tano?

Kwanini tunalazimishwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuwa tupo Awamu ya Sita wakati Kiuhalisia bado tupo Muhula wa Pili wa Awamu ya Tano?

Rais Mama Samia Suluhu Hassan nitakuwa wa mwisho Kukuamini kuwa tupo Awamu ya Sita kama unavyotulazimisha.

Ninachojua tu Generalist na naamini hata wale Waliobarikiwa vyema Akili ni kwamba tupo bado Awamu ya Tano ya Muhula wake wa Pili ( wa mwisho).

Rais Mama Samia Suluhu Hassan nitakubaliana nawe kuwa tupo Awamu ya Sita pale tu ukichukua Fomu na Kugombea Urais na ukashinda kuanzia mwaka 2025.

Rais wa Awamu ya Tano alikuwa ni Hayati Dkt. John Pombe Magufuli na Wewe kuwa Makamu wake na alipofariki Kikatiba ukaapishwa Wewe kuendelea ndani ya Awamu hii kstika Muhula wake wa mwisho.

Nasikitika tu kuona kuna waliomuamini.
Haiwezi kuwa AWAMU YA SITA. Kwa vigezo vipi?

Mkuu, haya ni matokeo ya kufanya mambo pasipokufuata taratibu, mama anaendeleza mle mle kwenye njia alizoziasisi mtangulizi wake.

Kwa hiyo mama na yeye sasa anatambua kwamba akijitangazia AWAMU YA SITA, hakuna atakayepingwa, kwa sababu yeye ndiyo rais!

Lakini hata akitangaza, historia itabaki kuwa vile vile, kwamba yeye anaendeleza awamu ya tano baada ya bosi wake kutoikamilisha awamu yao.
 
Hata JPM angeweza kutumia ya JK. Ni vipaumbele katika kuendeleza alipoishia aliyekuachia.

JPM akiamka leo, kipindi chake kitakuwa kimepita sababu tumeshaapisha raisi mwingine, ataitwa mstaafu badala ya marehemu.

UKISHAAPA WEWE NI RAISI, MARAISI WOTE WA CCM WANAENDELEZA WALIPOISHIA WALIOPITA.
Aende kwa wananchi, wamchague.

Hiyo itakuwa ni awamu yake bila ya kelele zozote.
 
Aende kwa wananchi, wamchague.

Hiyo itakuwa ni awamu yake bila ya kelele zozote.
Hii ni awamu yake. Kelele zinazopigwa hazibadili hilo. 2025 kuna uwezekano mkubwa akachaguliwa tena kumalizia awamu yake ya sita kwa kipindi cha mwisho kama chama kitampitisha.

Kama hii si awamu ya 6, ikitokea akapitishwa na chama akaanza awamu ya 6 yenye vipindi viwili, basi tupo naye for the next 14 years.
 
Kawaida imekuwa kwamba huko CCM lazima Rais mmoja aongoze vipindi viwili, naona hapo ndipo tatizo linapoanzia, kama akitokea Rais akaongoza muhula mmoja then amuachie mwingine naamini hii story ya awamu itabadilika.

Samia angekuwa Rais wa awamu ya sita kama angeanzia mwanzo baada ya kufanyika uchaguzi mkuu agombee na ashinde, lakini kama amekuja kumalizia kazi iliyoanzishwa na mwenzake yeye akiwa makamu basi yeye bado ni Rais wa awamu ya tano anaemalizia awamu waliyoianza na mwendazake.
Si kweli mnapotoshana awaamu inaambatana na Rais mpya awamu sio kikatiba ni mapendekezo ya chama
 
Rais Mama Samia Suluhu Hassan nitakuwa wa mwisho Kukuamini kuwa tupo Awamu ya Sita kama unavyotulazimisha.

Ninachojua tu Generalist na naamini hata wale Waliobarikiwa vyema Akili ni kwamba tupo bado Awamu ya Tano ya Muhula wake wa Pili ( wa mwisho).

Rais Mama Samia Suluhu Hassan nitakubaliana nawe kuwa tupo Awamu ya Sita pale tu ukichukua Fomu na Kugombea Urais na ukashinda kuanzia mwaka 2025.

Rais wa Awamu ya Tano alikuwa ni Hayati Dkt. John Pombe Magufuli na Wewe kuwa Makamu wake na alipofariki Kikatiba ukaapishwa Wewe kuendelea ndani ya Awamu hii kstika Muhula wake wa mwisho.

Nasikitika tu kuona kuna waliomuamini.
Awamu ni Raisi😂😂 Raisi akifa na awamu inaisha na hii ni kisheria maana awamu ni ya Raisi sio makamu. Hivyo hii ni awamu ya kwanza ya awamu ya 6 na anaweza kuhombea tena kisheria kwa muhula mmoja.
 
Rais Mama Samia Suluhu Hassan nitakuwa wa mwisho Kukuamini kuwa tupo Awamu ya Sita kama unavyotulazimisha.

Ninachojua tu Generalist na naamini hata wale Waliobarikiwa vyema Akili ni kwamba tupo bado Awamu ya Tano ya Muhula wake wa Pili ( wa mwisho).

Rais Mama Samia Suluhu Hassan nitakubaliana nawe kuwa tupo Awamu ya Sita pale tu ukichukua Fomu na Kugombea Urais na ukashinda kuanzia mwaka 2025.

Rais wa Awamu ya Tano alikuwa ni Hayati Dkt. John Pombe Magufuli na Wewe kuwa Makamu wake na alipofariki Kikatiba ukaapishwa Wewe kuendelea ndani ya Awamu hii kstika Muhula wake wa mwisho.

Nasikitika tu kuona kuna waliomuamini.
Kwani awamu unaihesabu vp?NI kwa miaka? Au ?
Kama NI miaka je awamu Mona ina jumla ya miaka mingap? Labda wewe ndio utueleweshe kwa Nini unasema NI awamu ya tano muhula was pili
Basi hebu ona hizo awamu zilizo
pita
Nyerere miaka 20+
Mwinyi miaa 10
Mkapa 10
Jk miaka 10
Magu 5
Haya sisi tusiojua awamu tuambie awamu ina miaka mingapi?
 
Hii ni awamu yake. Kelele zinazopigwa hazibadili hilo. 2025 kuna uwezekano mkubwa akachaguliwa tena kumalizia awamu yake ya sita kwa kipindi cha mwisho kama chama kitampitisha.

Kama hii si awamu ya 6, ikitokea akapitishwa na chama akaanza awamu ya 6 yenye vipindi viwili, basi tupo naye for the next 14 years.
Eeenh Heee,
Hii ni awamu yake. Kelele zinazopigwa hazibadili hilo.

Mkuu, hii tabia ya mabavu mtaachana nayo lini? Tumia akili zaidi kuliko kulazimisha watu.

Hiyo habari ya "2025 yeye kugombea na kuchaguliwa kwa kipindi chake cha mwisho" umeitoa wapi?
Ndivyo katiba inavyosema?
 
Eeenh Heee,


Mkuu, hii tabia ya mabavu mtaachana nayo lini? Tumia akili zaidi kuliko kulazimisha watu.

Hiyo habari ya "2025 yeye kugombea na kuchaguliwa kwa kipindi chake cha mwisho" umeitoa wapi?
Ndivyo katiba inavyosema?
Boss sio mabavu ni uhalisia.

Ndiyo... katiba imetoa vipindi viwili vya miaka 5. Ccm wakavibatiza jina awamu. SSH akigombea 2025 anamalizia kipindi chake au awamu kama ccm wanavyoziita, katiba haimruhusu zaidi ya 2030.

Ila kama hii ni still awamu ya 5 kama unavyotaka na si awamu yake, basi inamaana ana vipindi vingine vya miaka 5 mara mbili vya awamu mpya.2025/30 - 2030/35. Hapa ataongoza kinyume na katiba inavyotaka miaka 10.

JPM lets say angefariki 2 years before uchaguzi basi hicho kipindi cha miaka 2 kisingekuwa awamu ya sita bali ya tano. Lakini 3 yrs na kuendelea ni awamu mpya.
 
Ila kama hii ni still awamu ya 5 kama unavyotaka na si awamu yake,
Nielewe, siyo kama ninavyotaka mimi; lakini hujaweka vigezo vyovyote vinavyoonyesha kuwa ni awamu ya sita.
Kama nilivyoandika hapo juu, kama anataka awe na awamu yake, aende kwa wananchi wampigie kura na aunde serikali yake ya awamu ya sita.
Huu uliopo sasa ni mwendelezo wa awamu ya tano.
 
Kalamu 1

"Ila kama hii ni still awamu ya 5 kama unavyotaka na si awamu yake, basi inamaana ana vipindi vingine vya miaka 5 mara mbili vya awamu mpya.2025/30 - 2030/35. Hapa ataongoza kinyume na katiba inavyotaka miaka 10."


Sentensi nimeandika imekamilika usiipunguze kubadili maana.
 
Kalamu 1

"Ila kama hii ni still awamu ya 5 kama unavyotaka na si awamu yake, basi inamaana ana vipindi vingine vya miaka 5 mara mbili vya awamu mpya.2025/30 - 2030/35. Hapa ataongoza kinyume na katiba inavyotaka miaka 10."


Sentensi nimeandika imekamilika usiipunguze kubadili maana.
Mimi sioni tatizo na hili, endapo kama ana ridhaa ya wananchi hapo 2025 na miaka mingine mitano baada ya hapo!

Maadam katiba iko kimya juu ya hilo, wewe unaona tatizo?

'Caviet' ni hiyo moja tu, kutimiza matakwa ya wananchi - yaani wampigie kura 2025 na hiyo mitano ya kumaliza awamu hiyo.
 
Yapo mabadiliko makubwa ya yanayoashiria tupo awamu nyingine mkuu! Nakumbuka awamu ya tano Bashiru na mwenzake Chakubanga walikuwa wanaogopeka na kuheshimika kama simba wa porini ila ssa hivi wanapigana vikumbo na wakina Lusinde hata salamu hawapewi! Kweli zama Zimebadilika.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Sababu kubwa ni hii
Rais Mama Samia Suluhu Hassan nitakuwa wa mwisho Kukuamini kuwa tupo Awamu ya Sita kama unavyotulazimisha.

Ninachojua tu Generalist na naamini hata wale Waliobarikiwa vyema Akili ni kwamba tupo bado Awamu ya Tano ya Muhula wake wa Pili ( wa mwisho).

Rais Mama Samia Suluhu Hassan nitakubaliana nawe kuwa tupo Awamu ya Sita pale tu ukichukua Fomu na Kugombea Urais na ukashinda kuanzia mwaka 2025.

Rais wa Awamu ya Tano alikuwa ni Hayati Dkt. John Pombe Magufuli na Wewe kuwa Makamu wake na alipofariki Kikatiba ukaapishwa Wewe kuendelea ndani ya Awamu hii kstika Muhula wake wa mwisho.

Nasikitika tu kuona kuna waliomuamini.
 
Mimi sioni tatizo na hili, endapo kama ana ridhaa ya wananchi hapo 2025 na miaka mingine mitano baada ya hapo!

Maadam katiba iko kimya juu ya hilo, wewe unaona tatizo?

'Caviet' ni hiyo moja tu, kutimiza matakwa ya wananchi - yaani wampigie kura 2025 na hiyo mitano ya kumaliza awamu hiyo.
Tupo pamoja katika hili mkuu.

Wananchi ndo kila kitu.
 
Rais wa Zanzibar wa sasa Dr Hussein Mwinyi ni Rais wa awamu ya nane kule Zanzibar. Sasa jiulize hao marais nane wa awamu zote nane walifanya uchaguzi ndio ikaanza kuhesabiwa upya au.....!!.

Simple logic ni kuwa anapoingia madarakani Rais mwengine unaanza kuhesabiwa awamu mpya rejea mfano wa Zanzibar
Znz wana katiba yao ambayo ni tofauti na ya kwetu. Sijui kwanini unafananisha ila ni kwamba, Hayati JPM alishinda uchaguzi wa mwaka 2020 ili kukamilisha muhula wake wa pili wa awamu ya tano. Akahudumu kwenye muhula wa pili kwa miezi michache.

Katiba inasema, Makamu wake aapishwe kumalizia ngwe iliyobaki, na zaidi inasema kama kipindi kilichobaki ni chini ya miaka mitatu, Makamu huyo hatahesabiwa kuwa amehudumu kipindi kimoja cha awamu hiyo.

2020 angeshinda Lisu au CCM ingempitisha mtu tofauti na JPM, hapo tungekuwa tumeanza awamu ya 6.

Hivyo, Samia anamalizia muhula wa pili ulioachwa na JPM kwa uchaguzi wa 2020. Yeye ni raisi wa 6 wa JMT yenye mihula mitano mpaka sasa, ndo kusema, awamu ya tano imeshikwa na maraisi wawili.

Ni kama katika hali ya kawaida kuendelea kung'ang'ania kuwa Edward Lowasa ni waziri mkuu mstaafu, alistaafu lini?
 
Awamu ya tano kivipi? Hii ni awamu ya sita. Awamu inawakilisha mtu si miaka.

Nyerere awamu ya 1, miaka zaidi ya kumi...
Mwinyi awamu ya 2, miaka kumi
Mkapa awamu ya 3, mikaka kumi
Kikwete awamu ya 4, miaka kumi
JPM awamu ya 5, miaka 5 na miezi miwili
SSH awamu ya 6, haijulikani miaka.......

Still kama awamu ni miaka 10 na si mtu basi Nyerere hajatawala awamu moja hivyo hatukupaswa kuwa awamu ya tano.

Kama hutaki we mbishi tu.
Pengine tuzumzie awamu baada ya vyama vingi na uchaguzi wa kwanza wa kidemokrasia. Awamu inaweza kuwa ni kichwa au muda kutegemea na uchaguzi au anayeingia ofisi kuu.

Mtu yule yule anaporudi ofisini baada ya uchaguzi mkuu, awamu haibadiliki. Awamu inaweza kuwa ya miaka 5 au 10 kutegemeana na uchaguzi.

Raisi mteule, baada ya kuapishwa kikatiba, anapaswa kumteua waziri mkuu ndani ya siku zilizotajwa, waziri mkuu mteuliwa ataapishwa na raisi. Raisi atalihutubia bunge ishara ya kulifungua rasmi bunge.

Kuna tamko lolote kuhusu kwanini Majaliwa anaendelea kwa uteuzi ule ule wa JPM na kiapo kile kile cha JPM?

Waziri mkuu akifa, baraza linakuwa limekufa, vipi akifa Raisi, baraza aliloliteua linabaki?

Samia ni raisi wa 6 wa JMT.
 
Back
Top Bottom