Kwanini tunalazimishwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuwa tupo Awamu ya Sita wakati Kiuhalisia bado tupo Muhula wa Pili wa Awamu ya Tano?

Kwanini tunalazimishwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuwa tupo Awamu ya Sita wakati Kiuhalisia bado tupo Muhula wa Pili wa Awamu ya Tano?

Rais Mama Samia Suluhu Hassan nitakuwa wa mwisho Kukuamini kuwa tupo Awamu ya Sita kama unavyotulazimisha.

Ninachojua tu Generalist na naamini hata wale Waliobarikiwa vyema Akili ni kwamba tupo bado Awamu ya Tano ya Muhula wake wa Pili ( wa mwisho).

Rais Mama Samia Suluhu Hassan nitakubaliana nawe kuwa tupo Awamu ya Sita pale tu ukichukua Fomu na Kugombea Urais na ukashinda kuanzia mwaka 2025.

Rais wa Awamu ya Tano alikuwa ni Hayati Dkt. John Pombe Magufuli na Wewe kuwa Makamu wake na alipofariki Kikatiba ukaapishwa Wewe kuendelea ndani ya Awamu hii kstika Muhula wake wa mwisho.

Nasikitika tu kuona kuna waliomuamini.
Hajaapishwa kuendelea bali kutawala
Rais Mama Samia Suluhu Hassan nitakuwa wa mwisho Kukuamini kuwa tupo Awamu ya Sita kama unavyotulazimisha.

Ninachojua tu Generalist na naamini hata wale Waliobarikiwa vyema Akili ni kwamba tupo bado Awamu ya Tano ya Muhula wake wa Pili ( wa mwisho), ila Samia Suluhu Hassan ni Rais wa Sita.

Rais Mama Samia Suluhu Hassan nitakubaliana nawe kuwa tupo Awamu ya Sita pale tu ukichukua Fomu na Kugombea Urais na ukashinda kuanzia mwaka 2025.

Rais wa Awamu ya Tano alikuwa ni Hayati Dkt. John Pombe Magufuli na Wewe kuwa Makamu wake na alipofariki Kikatiba ukaapishwa Wewe kuendelea ndani ya Awamu hii kstika Muhula wake wa mwisho.

Nasikitika tu kuona kuna waliomuamini.
Ni vyema kutofautisha kati ya awamu na muhula ili usipate mkanganyiko;

1. Kuingia kwa serikali na Rais mpya madarakani ni awamu nyingine...

2. Awamu moja ina mihula miwili.

3. Ukomo wa awamu ya utawala unaenda sambamba na ukomo wa muhula.

Kwa mantiki hiyo, Rais anaweza akatawala kwa muhula mmoja awamu fulani ama mihula miwili, akishindwa kuendelea na muhula mwingine kwa sababu za kikatiba na serikali mpya ikaingia madarakani, basi itahesabika awamu nyingine.

Awamu ni ile ile tu kama Rais ni yule yule.

Ukomo wa muhula/mihula wa utawala ni mwisho wa awamu ya utawala na mwanzo wa awamu nyingine.

Yatosha kusema, ukomo wa muhula wa utawala wa Magufuli ndiyo mwisho wa awamu ya tano na mwanzo wa awamu ya sita ya Mama Samia.
 
So akitokea akafariki..ghafla..Mpango atakuwa Rais wa Saba katika awamu ya Saba sio!?
Ujinga mtupu ..Yani majitu nmnakomaa kwa kitu ambacho kipo wazi ..awamu Gani inakuwa na miaka minne..ama Tisa!?

Pole tu kwa Kuwaelimisha Wapumbavu.
 
ile ilani ni ya chama sio ya awamu bwege we. na sera za chama za awamu iliyopita ambazo hazijatekelezwa katika awamu husika huwa zinatekelezwa na rais ajae endapo atatokea chama hicho hicho kilichoongoza awamu iliyopita.

hapo chini ilani ya CCM inaonesha utekelezaji wa baadhi ya sera zake unaenda mpaka 2030 na nyingine mpaka 2050.

narudia tena ilani ni ya chama. BWEGE WE
View attachment 1756037

Sent from my SM-G570F using JamiiForums mobile app

Fanya upesi uwahi Mirembe ukatibiwe.
 
Hajaapishwa kuendelea bali kutawala

Ni vyema kutofautisha kati ya awamu na muhula ili usipate mkanganyiko;

1. Kuingia kwa serikali na Rais mpya madarakani ni awamu nyingine...

2. Awamu moja ina mihula miwili.

3. Ukomo wa awamu ya utawala unaenda sambamba na ukomo wa muhula.

Kwa mantiki hiyo, Rais anaweza akatawala kwa muhula mmoja awamu fulani ama mihula miwili, akishindwa kuendelea na muhula mwingine kwa sababu za kikatiba na serikali mpya ikaingia madarakani, basi itahesabika awamu nyingine.

Awamu ni ile ile tu kama Rais ni yule yule.

Ukomo wa muhula/mihula wa utawala ni mwisho wa awamu ya utawala na mwanzo wa awamu nyingine.

Yatosha kusema, ukomo wa muhula wa utawala wa Magufuli ndiyo mwisho wa awamu ya tano na mwanzo wa awamu ya sita ya Mama Samia.

Kichwani mwako zimetimia sawa sawa?
 
Rais Mama Samia Suluhu Hassan nitakuwa wa mwisho Kukuamini kuwa tupo Awamu ya Sita kama unavyotulazimisha.

Ninachojua tu Generalist na naamini hata wale Waliobarikiwa vyema Akili ni kwamba tupo bado Awamu ya Tano ya Muhula wake wa Pili ( wa mwisho), ila Samia Suluhu Hassan ni Rais wa Sita.

Rais Mama Samia Suluhu Hassan nitakubaliana nawe kuwa tupo Awamu ya Sita pale tu ukichukua Fomu na Kugombea Urais na ukashinda kuanzia mwaka 2025.

Rais wa Awamu ya Tano alikuwa ni Hayati Dkt. John Pombe Magufuli na Wewe kuwa Makamu wake na alipofariki Kikatiba ukaapishwa Wewe kuendelea ndani ya Awamu hii kstika Muhula wake wa mwisho.

Nasikitika tu kuona kuna waliomuamini.
Nyerere aliongoza awamu ngapi dogo?
 
Pengine tuzumzie awamu baada ya vyama vingi na uchaguzi wa kwanza wa kidemokrasia. Awamu inaweza kuwa ni kichwa au muda kutegemea na uchaguzi au anayeingia ofisi kuu.

Mtu yule yule anaporudi ofisini baada ya uchaguzi mkuu, awamu haibadiliki. Awamu inaweza kuwa ya miaka 5 au 10 kutegemeana na uchaguzi.

Raisi mteule, baada ya kuapishwa kikatiba, anapaswa kumteua waziri mkuu ndani ya siku zilizotajwa, waziri mkuu mteuliwa ataapishwa na raisi. Raisi atalihutubia bunge ishara ya kulifungua rasmi bunge.

Kuna tamko lolote kuhusu kwanini Majaliwa anaendelea kwa uteuzi ule ule wa JPM na kiapo kile kile cha JPM?

Waziri mkuu akifa, baraza linakuwa limekufa, vipi akifa Raisi, baraza aliloliteua linabaki?

Samia ni raisi wa 6 wa JMT.
Ok mkuu
 
We ni kilaza,hivi aufahamu kuwa kuna uchaguzi kila miaka mitano je kama magufuli angeshindwa na lisu tungesema lisu anaendeza awamu ya tano.

Hapo nafikiri aujaelewa,hebu fikiria kama membe angechukua fomu na magufuli kutokupitishwa alafu membe awe rais ingekuwa ni hawamu ya tano tena?.

Kwa ufupi hawamu ni vichwa vya marais ndio maana kila hawamu kunakuwa na rais bila kujali muda alioudumu kwa taarifa yako Samia ni rais wa sita wa tanzania .
Awamu ya Tano ya Muhula wake wa Pil
 
Yani wewe pamoja na huyo mnaisoma katiba bila kuitafakari...Samia anatumia Ilani ya awamu Gani katika kuongoza Serikali yake anayoiita ya awamu ya sita!? Ujiulizi why hana vipaumbele vyake zaidi ya kuviendeleza vya JPM !?

Guys hili somo naona wengi wenu hapa ni maamuma ..na hamtaki kuujua ukweli..

Samia ni Rais wa Sita katika awamu ya tano..2025 akigombea atakuwa Rais wa Sita katika awamu yake mpya ya Sita.

Mzee..awamu ni term ya miaka...nakupa.mfano..kama Jiwe angekuwa hai..na MATAGA wakamuongezea miaka Kama walivyokuwa wanataka..bila kujali ingekuwa ni miaka mingap.simple angeendelea kuwa Rais wa Tano..katika awamu ya tano kulingana na miaka ambayo angetawala nayo mpaka ukomo wake. So Nyerere anabaki kuwa awamu ya kwanzA kwa sababu awamu yake ilikuwa na mingi miaka ambayo ikifika ukomo baada ya Mwinyi kuingia madarakani..hii ndio kusema Kama Mwl angekuwa hai mpaka leo ..na angeendelea kuwa Rais kwa namna yeyote iwe kushinda ama kuukalia madaraka kinguvu..sti angekuwa Rais wa kwanzA katika awamu ya kwanzA..mpaka ambapo angeingia Rais mwingine..
Sawa
 
Swali ambalo anatakiwa kujiuliza ni kuwa iwapo jpm angekuwa amesafiri au yuko kwenye matibabu ya muda mrefu automatically anayeongoza nchi ni yeye, je angesimama kwenye jukwaa na kusema hii ni serikali ya awamu ya sita? Then jpm akirudi anasema ni serikali ya awamu ya 5. Awamu za serikali zinatokana na UCHAGUZI sasa hapa hakuna uchaguzi mwingine uliofanyika.

Nikieleweka na Watu ( Members ) ambao ni Werevu ( Intelligent ) kama Wewe na Wenzako baadhi hapa huwa ninafurahi sana tu.

Nasikitika kuna baadhi ya Watu hapa wanajiita Wasomi lakini Jambo dogo tu hili wameshindwa Kulielewa na hata Kulichambua.

Kama Rais Samia ataendelea Kusema ( Kusisitiza ) Yeye ni Rais wa Awamu ya Sita nitaamini kuwa ana IQ Ndogo na nitamdharau pia.

Rais Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan ni Rais wa Sita katika Awamu ya Tano iliyo katika Muhula wake ( wa mwisho ) wa Pili.


Nimemaliza.
 
Mzee..hivi mnasomaga katiba kama.kitabu cha hadithi ama gazeti!? ..embu Rudi tena kasome katiba vyema kipengele cha endapo Rais atafia madarakani na namna ya kumsimika Makamu wake kuwa Rais ndipo utaelewa usiyojua..
Okey.
 
Rais wa Zanzibar wa sasa Dr Hussein Mwinyi ni Rais wa awamu ya nane kule Zanzibar. Sasa jiulize hao marais nane wa awamu zote nane walifanya uchaguzi ndio ikaanza kuhesabiwa upya au.....!!.

Simple logic ni kuwa anapoingia madarakani Rais mwengine unaanza kuhesabiwa awamu mpya rejea mfano wa Zanzibar
Zanzibari sio Nchi
Rejea Mzingo Pinda HUTUBA YAKE bungeni
 
Pole tu kwa Kuwaelimisha Wapumbavu.
Fanya upesi uwahi Mirembe ukatibiwe.
Ondoa Funza waliomo Kichwani mwako.
Inaonekana umeuliza swali ukiwa na jibu lako kichwani .

Hebu nikuulize awamu ya tatu ya A H Mwinyi - Zanzibar aliongoza kwa chini miaka miwili . Alirithi wabunge na mawaziri wa Alhaji Aboud Jumbe na wabunge 1984- 1985. Lakini si ni awamu ?!. Jumbe pia alirithi wabunge na mawaziri wa Sheikh Karume bila uchaguzi , lakini si ni awamu ya pili Zanzibar ?!.

Sasa kosa la Mama Samia kurithi Bunge na mawaziri wa awamu ya tano na kuhamia nao awamu ya sita Tanganyika iko wapi ?!
 
Back
Top Bottom