Kwanini ukienda hospitali idadi kubwa ya wanaotibiwa ni wanawake?

Kwanini ukienda hospitali idadi kubwa ya wanaotibiwa ni wanawake?

Nipo Muhimbili hapa...idadi kubwa ya wagonjwa na wapendwa wao ni wamama ... ni kwamba men hawaumwi!?

No wonder men ndo sababu tunakufa fasta hatuna muda wa kupokea tiba
Wanaume ni wagumu by nature, ni risk takers than women, and they tend not to seek medical help until it is complicated (wagumu)
 
Kuna mambo mengi kaka yanayochangia wanawake kwenda hospitali ndio maana kuna wodi ya wazazi wanawake lakini hakuna wodi ya wazazi wanaume.
Kuna magonjwa ya mfumo wa kizazi kwa wanawake hii hata kwa wanaume pia ipo ila wanaume huwa hatupendi kujikubali kwamba mfumo wote wa kizazi haufanyi kazi au hadi umshawishi akubali kwamba yeye hana nguvu za kiume itachukua miaka 10 ndio aende hospitali plus gharama mtu akiwaza alivyotoka jasho kuipata laki 1 halafu aipeleke hospitali kirahisi kwa magonjwa ya kuambiwa tu na mdomo inakuwa ngumu ila wanawake wao pesa zao zinapatikana kiurahisi kwa kupewa tu
Wamama ndiyo wanawapeleka hospitality watoto wao ndiyo maana wanaoneka wapo wengi ni mara chache sana kukuta Baba kampeleka mtoto wake Hospital
 
Kwa hiyo watakuwa wengi mbinguni eti?
Inaweza kuwa hivyo. Wanaume mara nyingi hatupendi ibada mungu atusaidie sana utatukuta kwa wingi kwenye mabanda ya mpira, kwenye vyumba vya kubeti, uwanjani , kwenye matamasha ya wasanii n.k.

Hata hivyo sababu zinazoweza kuwafanya wanawake kuwa wengi katika mikusanyiko ya injili
1. Wanawake wana matatizo kuliko wanaume , mfano , umaskini, magonjwa n.k
2. Wanawake wanafikiwa na matangazo kwa haraka na kwa urahisi
3. Kwa mtazamo wangu wahudhuriaji ibada wazuri ni over 60 years na katika huo umri wanawake wanatuzidi
 
Mleta mada ameingia wodi ya akina mama na wanaojifungua sijui anatazamia atapata atawapata wanaume humo?
Wakina Mama ndiyo wanaongoza kwenda kuwatembelea wagonjwa hospitali na kuwapelekea chakula kwahiyo lazima waonekane wapi wengi
 
Nipo Muhimbili hapa...idadi kubwa ya wagonjwa na wapendwa wao ni wamama ... ni kwamba men hawaumwi!?

No wonder men ndo sababu tunakufa fasta hatuna muda wa kupokea tiba
Hahaha, huu uchunguzi wako nimeukubali...kina mama kila sehemu wao wapo wengi, sio kupiga kura, na vinginevyo..wao ni rahisi kupokea jambo na kuanza nalo kupambana nalo..sisi wengine tuna ugumu sanaa..ndio maana tunakufa sana mkuu
 
Nipo Muhimbili hapa...idadi kubwa ya wagonjwa na wapendwa wao ni wamama ... ni kwamba men hawaumwi!?

No wonder men ndo sababu tunakufa fasta hatuna muda wa kupokea tiba
Wanawake ni waoga kuugua yaani kifogo tuu anakimbilia hospital tofauti na mwanaume.
 
Watu wanaotoa hoja tunaumwa ila tunajikaza kiume haina ukweli.
Sababu za kweli hizi hapa
1. Wanawake wanapokea magonjwa kirahisi kuliko wanaume . Mfano mwanamke ni rahisi kupata HIV kuliko mwanaume kulingana na maumbile yao
2. Ulaji wao , wanawake wanakula hovyo kuliko wanaume hasa junk food
3. Uzazi na Malezi mwanamke anahusika zaidi ya 95%
4. Magonjwa kama fangasi , magonjwa ya ngozi, kansa ya matiti, kansa ya kizazi yanashambulia zaidi wanawake
5. Wanawake waishi zaidi kuliko wanaume yani ukifanya sensa ya kuhesabu watu wenye zaidi ya miaka 60+ utakuta kundi kubwa la wanawake kuliko wanaume na umri huo ndio magonjwa ya uzeeni .

NB
Ukienda hosptiali kubwa waambie wakuoneshe idara ya Urolojia utakuta wanaume wamejaa
Ngoja niongezee. Kwenye suala la UZAZI tu peke yake mwanamke anaweza kupata kansa ya shingo ya uzazi, uvimbe katika ovaries (sometimes hata kansa ya ovaries), fibroids, kansa ya matiti (breast cancer), kifafa cha mimba, upungufu wa damu wakati wa ujauzito, hata kama hana ujauzito kutoka damu bila mpangilio , kutoshika ujauzito n.k. Wakati mwanaume kwenye uzazi labda apate Tezi dume tu!!!!
 
Nipo Muhimbili hapa...idadi kubwa ya wagonjwa na wapendwa wao ni wamama ... ni kwamba men hawaumwi!?

No wonder men ndo sababu tunakufa fasta hatuna muda wa kupokea tiba
Kiasi wanawake wanasumbuliwa na maradhi mengi kwa nature ya miili yao, ukozingatia ndio wenye jukumu kubwa la uzazi na niwetu wenye shughuli nyingi za hapa na pale.
WANAWAKE WOTE MUNGU AWABARIKI SANA
 
U
Ukienda kanisani ni hivyo hivyo,kwa waganga pia wanawake ndio wengi
Kwa ufupi hawakubali kufa kizembe
Au tuseme ni uoga wao tu
Uwoga wa wanawake unafanya wafike hospitalini mara kwa mara na matatizo yao kigundulika na kutibiwa mapema. Uwoga wa kobe, unasababisha aishi miaka mingi hadi zaidi ya 100. Ujasiri wa wanaume unasababisha kinyume chake, ni kama Simba wa porini, miaka 15 tu anarudisha namba kwa muumba.
 
Nipo Muhimbili hapa...idadi kubwa ya wagonjwa na wapendwa wao ni wamama ... ni kwamba men hawaumwi!?

No wonder men ndo sababu tunakufa fasta hatuna muda wa kupokea tiba

Pamoja kuzingatia aina huduma itolewayo kwenye vituo vya afya, bado tafiti zimeonyesha kuwa jinsi(mwanamke au mwanaume) imekuwa ni moja ya sababu ya utofauti wa mahudhurio kwenye vituo vya afya.

Wanawake wanao mwitikio mkubwa wa kwenda kituo cha afya kwa dalili yoyote anayojisikia au kutokuwa sawa.

Utofauti huu huweza kutokana na:

1: Matarajio kutoka kwenye huduma
Kuna huduma maalumu kwa makundi maalumu ya huduma husika. Hii huweza kuwaleta watu husika kwa wingi. Mfano: huduma za mpango wa uzazi. Hapa mwanamke ndiye mnufaika zaidi kwa mantiki ya mwanaume. Kulingana na malezi ya jamii na tamaduni, wababa hujihusiaha kwa uchache. Nso maana hapa kuna wamama hujiunga na huduma hii hata kwa siri bila kuhuaisha wenzi wao.

2: Malezi
Malezi yetu humjenga kijana wa kiume kuwa mkakamavu/musculinity. Hii humjenha kisaikolojia kutokuwa mwepesi kutoa ishara au kujongea kwa kila kiyu hasi kinachotokea kwenye mwili wake.

2: Unyanyapaa
Unaweza kuwa kwa huduma inavyotolewa inamwonyesha kila anaenda pale hospitalini ni kama anaonyesha unyoge wake/kwa tafsiri ya mwanaume au misingi ya jinsi huduma inavyotolewa huweza kumtweza kifikra mwanaume.
Pia kwenye baadhi ya huduma husika kama kliniki za watoto, ambapo baba huona kama ni jukumu la mama zaidi.

3: Tamaduni
Kwa tamaduni zetu, zinamtaka mwanaume asiwe mtu wa kuonyesha kulalamika kwa sababu ndogondogo. Hii hupelekea hata upande wa ugonjwa kuchukuliwa kiwepesi mpaka dalili zinapokuwa kubwa.

4: Utafutaji/kipato
Baba nso mtafutaji mkuu wa familia/social reaponsibility. Huwa kwenye harakati nyingi za kutafuta kipato , hivyo akibadili ratiba vitu hukwama/husimama pia.

5: Umri
Pia kuna magonjwa yanaathiri zaidi kulingana na jinsi. Mfano: maambukizi ya njia ya mkojo yapo zaidi kwa watoto wa kike. Wakari umri wa kati, watoto wa kike ni wahanga wa kupungukiwa damu sababu ya hedhi pia kuwa ni wahanga wa magonjwa ya ngono, umri mkubwa kuambatana na madhira yake kama menstrual syndrome na kansa aina mbalimbali kutokana na mabadiliko makubwa ya vichocheo/homoni mwilini.

Hizi ni baadhi tu ya sababu zinazofanya mahudhurio ya wamama kwenye vituo vya afua kuwa juu zaidi ya wanaume
 
uume na unaulizwa helaya sabuni sukari imeisha na ada ... lazima maumivu ya magonjwa yawe sugu na kufa mapema
 
Wanawake huwa hawanata tabia ya kusubiri mpaka ugonjwa ukolee
 
Nipo Muhimbili hapa...idadi kubwa ya wagonjwa na wapendwa wao ni wamama ... ni kwamba men hawaumwi!?

No wonder men ndo sababu tunakufa fasta hatuna muda wa kupokea tiba
Kwa idadi wanawake ni wengi kuliko wanaume

Pia wanawake Wanaumwa sana na Wana magonjwa mengi
 
Sasa wanawake wajawazito wanaenda clinic sasa ulitegemea kuona wanaume huko
 
Nipo Muhimbili hapa...idadi kubwa ya wagonjwa na wapendwa wao ni wamama ... ni kwamba men hawaumwi!?

No wonder men ndo sababu tunakufa fasta hatuna muda wa kupokea tiba
Wanapitia machungu mengi sana
 
Back
Top Bottom