2013.....
huo mwaka niliwahi kusafiri katika mkoa wa Arusha kwa ajili ya kutafuta fursa za kibiashara
wakati safari inaendelea nikiwa ndani ya mkoa wa Arusha huku mvua kubwa ikinyesha na milio ya radi ikipiga kwa kasi, wakati huo ni saa 9 usiku wa manane
kutokana na spidi ya gari kuwa 80 KpH aina ya Prado land cruiser TX mwangaza wa taa niliweza kumwona bibi akiwa na asili ya kimaasai, nilisimama na kumpa lifti bila kujali chochote, yule bibi alikubali na nikamfikisha Hadi anapo elekea ni porini Sana karibia na mbuga ya wanyama wakati huo saa 11:30 alfajiri yule bibi nimemfikisha kwake.
awali pindi tupo kwenye gari nilipata nafasi ya kuzungumza nae lakini hakutaka kueleza usiku ule na mvua zote zile alitokea wapi...? Haikuwa jukumu langu kulazimisha kuelewa yote hayo bali kumhakikishia usalama wake kwa wakati ule.
baada ya kumfikisha kwake alisihi nisubiri kwa muda kadhaa kisa aliingia katika boma lake na kuniletea mfuko mdogo ila una mawe wenye uzito ndani yake akaniambia hiyo ni zawadi yako majukumu wangu ubarikiwe kwa ukarimu wako nenda salama majukumu wangu.
nikaondoka zangu lakini kichwani Nina mawazo tele kwenye mfumo Kuna nini mbona Kuna uzito Sana kuangalia ni dhahabu alinipa. Kutoa ni moyo ndugu zangu Tena kwa ukunjufu.