Kwanini Ukristo na Uislam unashamiri kwenye nchi masikini na duni kielimu?

Kwanini Ukristo na Uislam unashamiri kwenye nchi masikini na duni kielimu?

Ninakubaliana na maelezo yako lakini bado pia hukutoa kilicho nyuma ya sababu ya dini za Kikristo na Kiislamu peke yake kushamili katika maeneo ya watu masikini na wasio na elimu ya juu ukilinganisha na imani za dini zingine?

Kwanza tuangalie: Kwani misingi ya hizi Dini kuu mbili ni ipi? Imani ni nini?

Kwa ufupi Msingi wa Hizi Dini ni kuishi kwa kufuata mafundisho yaliyojengwa juu taratibu maalum na zilizowekwa na Mungu (kwa mujibu wa mafundisho yao) i.e Kupendana, kujaliana, kushirikiana, uadilifu na kuonyana juu ya mienendo isiyofaa n.k (kwa mtazamo wao).

Na la pili ambalo ni kubwa ni kuwa na Imani, kuijenga Imani na kuishi kwa Imani. Na Imani kwa mtazamo wa Ukristo ni kuwa na matarajio juu ya mambo yajayo. Imani juu ya Maisha baada ya kifo, kwamba binadamu tunakufa hilo ni jambo linalojulikana, lakini baada ya hapo? ni Imani kwamba tukifuata misingi hiyo hapo juu tuna hakika ya kuishi baadaye.

Hapa lazima tukumbuke pia kwamba Ulaya Ukristo ulianza karne nyingi zilizopita. Huwezi kusema ustaarabu unaouona leo hauna muunganiko na Ukristo. Upo uhusiano mkubwa sana. Labda kinacholeta tofauti ni kimoja tu kwao, kwamba wanaona kwa sasa wanaweza kujenga Uadilifu, Utu, kuonyana n.k pasipo kukanyaga milango ya Kanisa!

Je Imani? kuijenga Imani na kuiishi Imani kila siku ni jambo linalohitaji muda na kujitoa (kwa mujibu wa Imani hizo).
Je Wazungu wana muda huo? wa kuamka saa 12 kwenda Kanisani, Je wana muda wa kumsikiliza Pastor au Padre?

Back to Waswahili:
Lazima tujue pia hakuna matumani nje ya mfumo wa Dini hizi mbili. Joto la Umasikini ni kubwa sana na mahali pekee ambapo tumaini linaweza kupatikana ni kuwa humo. Ndiyo maana ukuaji wa hizi Dini ni mkubwa, mahali ambapo Elimu ni Duni na umasikini upo juu ni rahisi watu kupokea mafundisho, kusikiliza na kujiunga.
 
cha kuchekesha ni mashariki ya mbali usitawi wa kiuchumi na mambo mengine unakuwa huku ukristu unakata mbuga,ulaya wanaanguka kadiri wanavyoukimbia ukristu.
 
Hili mkuu Kiranga kila mara hulizungumzia i.e umaskini na iman ya dini vinafungamana sana....kuna kipindi hata signature yake ilikuwa na ujumbe huo....kuna ukweli mkubwa sana lakn.

Soma signature yangu hapo chini. Sasa ukose yote hata imani au matumaini? Nawakubali watu ambao wana mali, elimu na bado wanamtegemea Mungu!
 
Ninavyofahamu,na kuona skorea,china na nchi nyingi za far east Ukristu unakuwa,na hii ni kwa sababu religion ni natural kwa mwanadamu.communinism ilikufa kwa vile ilikuwa na vacuum.

Hizo nchi hapo juu si masikikini kihivyo,.ukristo wa korea na uchina,hongkong,macau etc upo kwa matajiri,hata west watu wanaorudi ktk ukristu wapo.
North korea na china wanaangalia ukristu km tishio kwa tawala za kijamaa kuliko chombo cha mafanikio.ingawa raia wake wanafight kuufuata wakiamimini ndio ustaarabu wa mafanikio.

Ukristu korea si majority religion ila impact yake dunia inaona na hata wamisionary wao ni wengi sana dunian.

Tuwe waangalifu,east panakuwa huku wakipokea ukristu,west panaanguka jinsi wanaukataa ukristu.jamii isiyo na hope ni km mfu.Yesu ni hope.
Atheism haimpi mtu sababu ya kujenga kitu cha kudumu.islam inakimbiza watu wafe kuwahi pepo zaidi kuwekeza ktk elimu dunia .
Tuwe waangalifu na tafiti za propaganda km za redet.hata mashoga wana tafiti zao kuonyesha kuwa hata penguin mashoga wapo,nyani mashoga wapo na wanyama wengine halafu wakahitimisha kuwa ni natural.lakini nani kawauliza waliwapataje hao wanyama wachache mashoga?km si wao waliwaprogram ili potosha dunia.
Mkuu Nicholas , point yangu inabaki pale pale kwa sababu nchi hizo ulizozisema bado imani ya Kikristo na Kiislamu ni ndogo sana. Wakristo China wako 4% na Waislamu 2% ya wananchi. Nchini Korea ya kusini, wakristo wako 36% na Waislamu kama 1%.

Sipendi kugusia mambo ya imani kuhusiana na mapokeo ya dini, lakini pia ninashindwa kukuelewa unaposema watu wa nchi za magharibi wanaanguka kwa kukataa imani za dini za Kikristo na kiislamu.
 
Last edited by a moderator:
Dini zipo associated sana na moral development. Katika nchi zilizoendelea, watu wana maadili hata kama hawapractice dini. Rushwa, uzinzi, dhulma, uongo, wizi na mengine yanaitwa maovu katika jamii zilizoendelea lakini yanaitwa dhambi katika nchi zisizoendelea. Pengine hii inahusishwa pia na degree ya ustaarabu, ambapo mara nyingi ni kubwa katika jamii zilizo na elimu kuliko jamii ambazo hazijaelimika

Ushoga na ndoa za jinsia moja ni katika hayo maadili? Au ndio degree ya juu ya ustaarabu? Au ndio maendeleo yenyewe?
 
Hii maada nzuri sana!! ingawa kuna watu wanataka kuhusanisha kati ya maendeleo na aina ya dini, hilo litakuwa kosa. Chanzo cha dini zote, ni mashariki ya kati!! kwa hiyo pindi inapokuwepo nje ya maeneo hayo, na watu wakapata elimu ya kutosha juu ya chanzo cha dini hiyo, na jamii waliyoishi mitume, na manabii, wakaenda ndani zaidi kutaka kujibu swali la je kama hamna dini kuna nini? utafiti ukaonyesha hamna kitu!!! then nguvu na mvuto wa dini unapungua!!

Labda niiweke hivi, Mtanzania Mkristo/muislam akipata elimu ya kutosha, ndani na nje ya dini, angependa kwenda kuona kule dini ilikotokea wameendelea kwa sababu ya dini? wanaishije maisha yao? je ni kwa mfumo wa dini tu? au wanakopi mifumo mifumo mingine? hayo majibu huleta ama kuongeza kushika au kuiona dini siyo sehemu ya mafanikio.

Pili, Kwanini nchi maskini zinashika dini? kuna sababu ambazo zimesemwa nami nakubaliana nazo, matumaini, upendo na mshikamano katika jamii. Kiwango kidogo cha elimu, siyo ya dunia tu bali hata ya hiyo dini yenyewe. ( wanao sali na kuijua dini yao vizuri ni wachache sana may be 15% wengi wanahofu tu ya mungu). Kutokana na umaskini watu huitaji misaada si ya mali tu hata ya kiroho na kisha kujifariji, hiyo hufanya mtu kupata matumaini na kubobea kwenye dini.
Nje ya umaskini, ustaraabu, amani na kutokuwa na kazi dini zingedumaa na ushamiri wake usingekuwa huu wa leo.

Mwisho, ukinzani wa dini umeletwa na ukuaji wa uchumi na maendeleo ya technolojia. Viongozi wa dini wa leo imebidi waingie humo, mifano, miskitini/makanisan leo wanauza maji, wana maduka, hospitali, shule nk nazo lazima ulipie, hivyo wameanza kufanya biashara ili kujijenga kiuchumi.
My take kama dini zingetokea ulaya hakika zingebaki hadi kesho, maana wangejifunia maendeleo/mafanikio na dini, ila leo zilikotoka hapako salama, kama tulivyotegemea!!
Sp
 
Si Uislamu wala Ukristo unaowakataza Waumini wake kutafuta Elimi na Mali(Kuijenga Dunia).Mimi sio mjuzi wa Ukristo lakini nitanukuu kauli za Mtume Muhammad(S.A.W) ili kuthibtisha maneno yangu.

Amesema Mtume wa Allah Rehema na Amani ziwe Juu yake"Itafuteni Dunia kana kwamba mutaishi milele na itafuteni Akhera kana kwamba mutakufa kesho"

Amesema Mtume wa Allah Rehema na Amani ziwe Juu yake"Kutafuta Elimu ni lazima kwa Muislamu Mwanaume na Muislamu Mwanamke"

Falsafa ya Zakah(Kodi inayolipiwa mali ya muislamu kila mwaka ili wapewe masikini) na Sadaka ni kuondoa umasikini katika jamii.

Falsafa ya kukataza Riba katika Uislamu ni kupinga umasikini unaosababishwa na Riba(Riba uchukua mali kutoka kwa masikini na kuwaongezea mali matajiri,angalia nchi masikini zinavyodaiwa na nchi tajiri na kila siku deni linaongezeka kwa sababu ya Riba).

Hakuna uhusiano baina ya umasikini na Dini au kukosa elimu na dini na kama ikitokea hivyo huo udhaifu wa viongozi wa Dini na serikali(Uislamu hautenganishi baina ya Dini na Serikali,kiongozi wa Dini ndio kiongozi wa Serikili).

Katika Uislamu Dini ni mfumo wa Maisha ya mwanadamu tokea anaamka mpaka analala,kila analolifanya ni dini,hivyo basi si kweli kusema watu wa Magharibi hawana Dini,wana Dini na Dini yao inaitwa Matamanio ya Nafsi zao.
 
Utajiri na umaskini hausababishwi na dini ni sisi wenyewe hatufanyi kazi.
 
Falsafa ya Zakah(Kodi inayolipiwa mali ya muislamu kila mwaka ili wapewe masikini) na Sadaka ni kuondoa umasikini katika jamii.

Falsafa ya kukataza Riba katika Uislamu ni kupinga umasikini unaosababishwa na Riba(Riba uchukua mali kutoka kwa masikini na kuwaongezea mali matajiri,angalia nchi masikini zinavyodaiwa na nchi tajiri na kila siku deni linaongezeka kwa sababu ya Riba).

Hakuna uhusiano baina ya umasikini na Dini au kukosa elimu na dini na kama ikitokea hivyo huo udhaifu wa viongozi wa Dini na serikali(Uislamu hautenganishi baina ya Dini na Serikali,kiongozi wa Dini ndio kiongozi wa Serikili).

mkuu asante kwa maoni hayo!! hapo kwenye red kwa hiyo maskini watapenda dini ya uislam moja ya sababu inaweza kuwa ile sadaka wanayp patiwa pale msikitin, na kama ikiwa hivyo basi ni kweli umaskini una uhusiano na dini, kama mtoa mada anavyo jaribu kutanabaisha.

hapo kwenye blue, nilipitia kidogo islamic banking, "Mudharabah" "Wadiah" "Musharakah" "Murabahah", na "ijar" hii ni aina tofauti ya riba kwa benk, nadhani utakuwa unasifahamu. kwa hiyo riba inategemea imewekwa aje.

Mwisho, hapo kwenye kutokutofautisha dini na serikali, hapo ndo tunapo anzia umaskini wetu, ama kwa kupingana, kupigana, kutengana, nk. nadhani hii pia ilikuwa hivyo kipindi cha utawala wa roman Empire (Ukristo wa mwanza) ila baadaye ndo walibadili kama sikosei ilikuwa 1700, ( ndo maana Us $ ina neno "In God we Trust".

Nionavyo, kuna haja ya kuiona dini kwenye mlengo wake, chanzo na madhumuni yake bila kujiwekea hofu ya jambo lijalo baada ya kifo!!!

Sp
 
KUNA WAKATI NILIFANYA KAZI NA MZUNGU MMOJA WA KIKE AMBAYE ALINIAMBIA WAZAZI WAKE TU NDIO WANAENDA KANISANI...YEYE SI SANA....ALIPOONA DISCUSSION INAPAMBA MOTO AKANIAMBIA..ALWAYS YOU STOP TO UNDERSTAND WHEN YOU START TO BELIEVE.......

nikainanisha kichwa nikaanza kurefer mstrari mmoja kwenye biblia kuwa kuamini ni kukubaliana na ambacho hujakiona.......nikakubaliana kabisa na neno la dada yule

hivyo basi ukichunguza vyema imani hizi ilikuwa namna ya kuimarisha morals za community at its introduction.......

but to the modest society....ni vema tukaa na morals zisizo za kuogofyana...ambazo zitakuwa sehemu ya tabia kama wenzetu wazungu.......japo tusiacche kwenda misikitini na makanisani kujiburudisha / kupumzisha vichwa na kujiwekea alawanzi ya what happens after death....

na ndio maana hata CCM IMEKUWA NI DINI KWA WATANZANIA WENGI WANAOAMINI KUWA IWE ISIWE CCM ITAWAKOMBOA WAKATI KILA SIKU INAWADIDIMIZA......WENGI WANAAMINI KUWA LAZIMA RAISI ATOKE CCM......CCM PIA NI DINI NA MAKUHANI WAKE NI KINA LAMECK MKUMBO AKA MWIGULU NCHEMBA.... ikiona karibu wanastuka ndio imeanza KUWABWETERE kwa kuwang'oa kucha na meno.....
 
Mkuu hatuwezi kuupata ukweli kama tukianza kutanguliza emotions katika ukweli unaogusa imani.

Kwa hiyo una maana nchi zilizoendelea zina mashetani wengi zaidi ya nchi masikini?.

Ole mhola hene ndogo wane?

Ni kweli ujinga na umasikini vinafanya dini ishamiri katika nchi zetu hizi. Ni kwa vile dini hizi zinajidai kutoa suluhisho la matatizo yetu hasa umasikini. Ulaya na America waligundua tangu zamani kwamba elimu na kufanya kazi ndio kuna-transform maisha ya mwanadamu. Huku kina Mwingira, Kakobe, Basaleh, Ilunga kazi kuwagombanisha waumini wao badala ya kuwafanya wasome na kufanya kazi. Ndio sababu unaona tu watu wanavyogombana kuchinja mnyama as if kunawaongezea chochote katika maisha.
 
Hii maada nzuri sana!! ingawa kuna watu wanataka kuhusanisha kati ya maendeleo na aina ya dini, hilo litakuwa kosa. Chanzo cha dini zote, ni mashariki ya kati!! kwa hiyo pindi inapokuwepo nje ya maeneo hayo, na watu wakapata elimu ya kutosha juu ya chanzo cha dini hiyo, na jamii waliyoishi mitume, na manabii, wakaenda ndani zaidi kutaka kujibu swali la je kama hamna dini kuna nini? utafiti ukaonyesha hamna kitu!!! then nguvu na mvuto wa dini unapungua!!

Labda niiweke hivi, Mtanzania Mkristo/muislam akipata elimu ya kutosha, ndani na nje ya dini, angependa kwenda kuona kule dini ilikotokea wameendelea kwa sababu ya dini? wanaishije maisha yao? je ni kwa mfumo wa dini tu? au wanakopi mifumo mifumo mingine? hayo majibu huleta ama kuongeza kushika au kuiona dini siyo sehemu ya mafanikio.

Pili, Kwanini nchi maskini zinashika dini? kuna sababu ambazo zimesemwa nami nakubaliana nazo, matumaini, upendo na mshikamano katika jamii. Kiwango kidogo cha elimu, siyo ya dunia tu bali hata ya hiyo dini yenyewe. ( wanao sali na kuijua dini yao vizuri ni wachache sana may be 15% wengi wanahofu tu ya mungu). Kutokana na umaskini watu huitaji misaada si ya mali tu hata ya kiroho na kisha kujifariji, hiyo hufanya mtu kupata matumaini na kubobea kwenye dini.
Nje ya umaskini, ustaraabu, amani na kutokuwa na kazi dini zingedumaa na ushamiri wake usingekuwa huu wa leo.

Mwisho, ukinzani wa dini umeletwa na ukuaji wa uchumi na maendeleo ya technolojia. Viongozi wa dini wa leo imebidi waingie humo, mifano, miskitini/makanisan leo wanauza maji, wana maduka, hospitali, shule nk nazo lazima ulipie, hivyo wameanza kufanya biashara ili kujijenga kiuchumi.
My take kama dini zingetokea ulaya hakika zingebaki hadi kesho, maana wangejifunia maendeleo/mafanikio na dini, ila leo zilikotoka hapako salama, kama tulivyotegemea!!
Sp
Nimekusoma na nimekuelewa na kama sijakuelewa vizuri utanisahihisha.

Kwa mtazamo wako, dini za imani ya kikristo na kiislamu zina mafundisho ambayo hayatoi majibu wa wananchi zaidi ya kuwajenga hofu na kuwajengea imani kama kile ambacho hawana na hawakitegemei kukipata kuna nguvu fulani inaweza kuwapatia lakini wakati haujulikani. Kwa hiyo cha maana ni kuendelea kuomba na kusubiri. Na hata kama wataiacha hii dunia basi kuna nguvu fulani pia itawafariji kwa yale waliyoyakosa hapa duniani.

Kwa maana kuwa hata wanachokiomba hawakijui na wanaongozwa na matumaini. Kwa maana kuwa hizi imani za dini zinacheza na saikologia ya binadamu.

Pale jamii inapoanza kuelimika na kutagirika, nguvu za imani za dini nazo katika maisha yao zinaanza kupungua.
 
Falsafa ya Zakah(Kodi inayolipiwa mali ya muislamu kila mwaka ili wapewe masikini) na Sadaka ni kuondoa umasikini katika jamii.

Falsafa ya kukataza Riba katika Uislamu ni kupinga umasikini unaosababishwa na Riba(Riba uchukua mali kutoka kwa masikini na kuwaongezea mali matajiri,angalia nchi masikini zinavyodaiwa na nchi tajiri na kila siku deni linaongezeka kwa sababu ya Riba).

Hakuna uhusiano baina ya umasikini na Dini au kukosa elimu na dini na kama ikitokea hivyo huo udhaifu wa viongozi wa Dini na serikali(Uislamu hautenganishi baina ya Dini na Serikali,kiongozi wa Dini ndio kiongozi wa Serikili).

mkuu asante kwa maoni hayo!! hapo kwenye red kwa hiyo maskini watapenda dini ya uislam moja ya sababu inaweza kuwa ile sadaka wanayp patiwa pale msikitin, na kama ikiwa hivyo basi ni kweli umaskini una uhusiano na dini, kama mtoa mada anavyo jaribu kutanabaisha.
hapo kwenye blue, nilipitia kidogo islamic banking, "Mudharabah" "Wadiah" "Musharakah" "Murabahah", na "ijar" hii ni aina tofauti ya riba kwa benk, nadhani utakuwa unasifahamu. kwa hiyo riba inategemea imewekwa aje.
Mwisho, hapo kwenye kutokutofautisha dini na serikali, hapo ndo tunapo anzia umaskini wetu, ama kwa kupingana, kupigana, kutengana, nk. nadhani hii pia ilikuwa hivyo kipindi cha utawala wa roman Empire (Ukristo wa mwanza) ila baadaye ndo walibadili kama sikosei ilikuwa 1700, ( ndo maana Us $ ina neno "In God we Trust".
Nionavyo, kuna haja ya kuiona dini kwenye mlengo wake, chanzo na madhumuni yake bila kujiwekea hofu ya jambo lijalo baada ya kifo!!!
Sp

Kwanza kabisa Mkuu tambua nini maana ya zakah

Zakah ni kodi inayolipiwa mali ya Muislamu ili wapewe maskini lengo ni kujiendelza kiuchumi ili mwaka unaofuta na wao waweze kulipa zakah watakayopewa maskini wengine ili wajiendeleze kuichumi.Mtu akishapewa Zakah anatakiwa afiatiliwe anaifanyia nini hiyo zakah pia apewe elimu ya matumizi wa hiyo zaka,sio kwenda kwenda kununua kuku na mchele ufaidi siku moja ili keshoukachukue zakah nyingine.

Ama Sadaka anapewa mtu yoyote yule maskini au tajiri(maskini anastahiki zaidi kuliko tajiri),sadaka anatoa mtu yoyote yule.

Hao matajiri wanaowapangisha watu foleni misikitini wanawadhalilisha maskini tu,hawataki kulipa zakah

Allah Mtukufu amesema katika Qurani Tukufu"Allah ameharamisha Riba na Amehalalisha Biashara"
Akasema tena"Akika ya Allah anaipa baraka mali ya biashara na inaipungizia baraka mali ya Riba"
Akasema tena"Anayekula Riba ametangaza vita na Allah"

Katika uislamu Riba ni haramu hata uipake rangi gani.
 
Nimekusoma na nimekuelewa na kama sijakuelewa vizuri utanisahihisha.

Kwa mtazamo wako, dini za imani ya kikristo na kiislamu zina mafundisho ambayo hayatoi majibu wa wananchi zaidi ya kuwajenga hofu na kuwajengea imani kama kile ambacho hawana na hawakitegemei kukipata kuna nguvu fulani inaweza kuwapatia lakini wakati haujulikani. Kwa hiyo cha maana ni kuendelea kuomba na kusubiri. Na hata kama wataiacha hii dunia basi kuna nguvu fulani pia itawafariji kwa yale waliyoyakosa hapa duniani.

Kwa maana kuwa hata wanachokiomba hawakijui na wanaongozwa na matumaini. Kwa maana kuwa hizi imani za dini zinacheza na saikologia ya binadamu.

Pale jamii inapoanza kuelimika na kutagirika, nguvu za imani za dini nazo katika maisha yao zinaanza kupungua.

Imani yangu ya Kiislamu inanifundisha mafanikio ya Duniani na Akhera yanapatika kwa kufanya juhudi za kweli kisha Allah utia taufiki yake katika juhudi zangu.

Kama kuna Waislamu wanaamini wataipata Dunia na Akhera kwa kubweteka tu late them go to the hell
 
Si Uislamu wala Ukristo unaowakataza Waumini wake kutafuta Elimi na Mali(Kuijenga Dunia).Mimi sio mjuzi wa Ukristo lakini nitanukuu kauli za Mtume Muhammad(S.A.W) ili kuthibtisha maneno yangu.

Amesema Mtume wa Allah Rehema na Amani ziwe Juu yake"Itafuteni Dunia kana kwamba mutaishi milele na itafuteni Akhera kana kwamba mutakufa kesho"

Amesema Mtume wa Allah Rehema na Amani ziwe Juu yake"Kutafuta Elimu ni lazima kwa Muislamu Mwanaume na Muislamu Mwanamke"

Falsafa ya Zakah(Kodi inayolipiwa mali ya muislamu kila mwaka ili wapewe masikini) na Sadaka ni kuondoa umasikini katika jamii.

Falsafa ya kukataza Riba katika Uislamu ni kupinga umasikini unaosababishwa na Riba(Riba uchukua mali kutoka kwa masikini na kuwaongezea mali matajiri,angalia nchi masikini zinavyodaiwa na nchi tajiri na kila siku deni linaongezeka kwa sababu ya Riba).

Hakuna uhusiano baina ya umasikini na Dini au kukosa elimu na dini na kama ikitokea hivyo huo udhaifu wa viongozi wa Dini na serikali(Uislamu hautenganishi baina ya Dini na Serikali,kiongozi wa Dini ndio kiongozi wa Serikili).

Katika Uislamu Dini ni mfumo wa Maisha ya mwanadamu tokea anaamka mpaka analala,kila analolifanya ni dini,hivyo basi si kweli kusema watu wa Magharibi hawana Dini,wana Dini na Dini yao inaitwa Matamanio ya Nafsi zao.
Hapo kwenye RED.
Ninashinbdwa kukuelewa unaposema hakuna usiano wa imani ya dini za kikristo na kiislamu wakati reseach imefanyika na ikabainisha hivyo.

Nikwambie tu kwamba. Historia inaonyesha kuwa dola zilizochanganya dini katika uendeshaji wake zilijikuta zikipata matatizo makubwa.

Huoni kama huo mfumo wa maisha unachangia au unastawisha umasikini na ukosefu wa elimu ya kiwango cha juu kama jedwali hapo juu linavyobainisha?.
 
KUNA WAKATI NILIFANYA KAZI NA MZUNGU MMOJA WA KIKE AMBAYE ALINIAMBIA WAZAZI WAKE TU NDIO WANAENDA KANISANI...YEYE SI SANA....ALIPOONA DISCUSSION INAPAMBA MOTO AKANIAMBIA..ALWAYS YOU STOP TO UNDERSTAND WHEN YOU START TO BELIEVE.......

nikainanisha kichwa nikaanza kurefer mstrari mmoja kwenye biblia kuwa kuamini ni kukubaliana na ambacho hujakiona.......nikakubaliana kabisa na neno la dada yule

hivyo basi ukichunguza vyema imani hizi ilikuwa namna ya kuimarisha morals za community at its introduction.......

but to the modest society....ni vema tukaa na morals zisizo za kuogofyana...ambazo zitakuwa sehemu ya tabia kama wenzetu wazungu.......japo tusiacche kwenda misikitini na makanisani kujiburudisha / kupumzisha vichwa na kujiwekea alawanzi ya what happens after death....

na ndio maana hata CCM IMEKUWA NI DINI KWA WATANZANIA WENGI WANAOAMINI KUWA IWE ISIWE CCM ITAWAKOMBOA WAKATI KILA SIKU INAWADIDIMIZA......WENGI WANAAMINI KUWA LAZIMA RAISI ATOKE CCM......CCM PIA NI DINI NA MAKUHANI WAKE NI KINA LAMECK MKUMBO AKA MWIGULU NCHEMBA.... ikiona karibu wanastuka ndio imeanza KUWABWETERE kwa kuwang'oa kucha na meno.....

Kaka hii ndio Dini yako,endelea kuamini hivyo kama unaona hiyo ndio njia ya mafanikio yako,si unajua ukifa hapa utazwaliwa tena ulaya ukiwa Mbwa,safi san.
 
Hili suala ni mtambuka, Dini hutoa watu kwenye giza na kuwaingiza kwenye mwanga!

Dini huwafanya watu wakaheshimiana na kujaliana kama alivyo amrisha Mwenyezi mungu.
Dini huleta usawa na haki miongoni mwa waumini!
Dini huondoa matabaka katika Jamii.
DINI HULEA UKARIMU na Maelewano kwani mwisho wa siku Binadamu wote ni WAJA wa Mwenyeezi Mungu...

Kwakuwa dini hugusa hisia za watu, Strategists wanatumia migongo ya dini kutugawa! Wanatumia migongo ya dini kunyonya Rasilimali zetu, Wanatumia migongo ya Dini kuonesha kuwa kuna watu wa imani inayopingana na yao kuwa wana wadhulumu na kuwa dharau! Kwa kutumia Dini wazungu walikuja kwetu kututawala...

The bottom-line ni kuwa Dini yaweza kuwa chachu ya maendelea kama ilivyo kwa baadhi ya nchi hususan za Kiislam na wenye kutumia Islamic Bond kwa maendeleo mfano nchi za Mashariki ya Mbali.

Kwa upande wa pili wa shilingi dini ni chanzo kikubwa cha machafuko miongoni mwa Jamii hususan pale ambapo Nchi Tajiri zinapotumia dini kukwapua rasilimali and in return wanarudisha vijimisaada kupitia kwenye dini! Jamii hukosa maelewana na matokeo yake kunakuwa na matabaka kati ya waliopata misaada ya shule, mahospitali nk Vs wale ambao wanahisi wanadharauliwa!

...Social GAP ni tatizo kubwa sana linalisababishwa na dini kwa nchi nyingi masikini duniani...
 
Hapo kwenye RED.
Ninashinbdwa kukuelewa unaposema hakuna usiano wa imani ya dini za kikristo na kiislamu wakati reseach imefanyika na ikabainisha hivyo.

Nikwambie tu kwamba. Historia inaonyesha kuwa dola zilizochanganya dini katika uendeshaji wake zilijikuta zikipata matatizo makubwa.

Huoni kama huo mfumo wa maisha unachangia au unastawisha umasikini na ukosefu wa elimu ya kiwango cha juu kama jedwali hapo juu linavyobainisha?.

Hakuna uhusiono,research za kuimarisha dini zao za ukahaba na ushoga hizo wapelekee wenyewe.

UsSR ilianguka kwani ilichanganya Dini na Serikiali,Marekani nayo ipo ukingoni karibu itaanguka kwani imechanganya Dini na Serikali.

Kila Dola lenye nguvu linasimama na kuanguka,wale ambao Dola zao zilianguka sasa wanajipanga kuzirudisha.wewe kaa na kuwasifia wamagharibi tu kwa sababu wamekufadhili.
 
KUNA WAKATI NILIFANYA KAZI NA MZUNGU MMOJA WA KIKE AMBAYE ALINIAMBIA WAZAZI WAKE TU NDIO WANAENDA KANISANI...YEYE SI SANA....ALIPOONA DISCUSSION INAPAMBA MOTO AKANIAMBIA..ALWAYS YOU STOP TO UNDERSTAND WHEN YOU START TO BELIEVE.......

nikainanisha kichwa nikaanza kurefer mstrari mmoja kwenye biblia kuwa kuamini ni kukubaliana na ambacho hujakiona.......nikakubaliana kabisa na neno la dada yule

hivyo basi ukichunguza vyema imani hizi ilikuwa namna ya kuimarisha morals za community at its introduction.......

but to the modest society....ni vema tukaa na morals zisizo za kuogofyana...ambazo zitakuwa sehemu ya tabia kama wenzetu wazungu.......japo tusiacche kwenda misikitini na makanisani kujiburudisha / kupumzisha vichwa na kujiwekea alawanzi ya what happens after death....

na ndio maana hata CCM IMEKUWA NI DINI KWA WATANZANIA WENGI WANAOAMINI KUWA IWE ISIWE CCM ITAWAKOMBOA WAKATI KILA SIKU INAWADIDIMIZA......WENGI WANAAMINI KUWA LAZIMA RAISI ATOKE CCM......CCM PIA NI DINI NA MAKUHANI WAKE NI KINA LAMECK MKUMBO AKA MWIGULU NCHEMBA.... ikiona karibu wanastuka ndio imeanza KUWABWETERE kwa kuwang'oa kucha na meno.....
Ni kweli kama unavyosema. Kwanza jamii ambayo ni masikini na haina elimu ya kutosha inakuwa na mapungufu katika maangalizo kwa kina. Naona kama hizi imani za dini zinawajengea wananchi mazingira ya kuishi kwa kuhofia kisichojulikana (Fear for unknown)
 
Ole mhola hene ndogo wane?

Ni kweli ujinga na umasikini vinafanya dini ishamiri katika nchi zetu hizi. Ni kwa vile dini hizi zinajidai kutoa suluhisho la matatizo yetu hasa umasikini. Ulaya na America waligundua tangu zamani kwamba elimu na kufanya kazi ndio kuna-transform maisha ya mwanadamu. Huku kina Mwingira, Kakobe, Basaleh, Ilunga kazi kuwagombanisha waumini wao badala ya kuwafanya wasome na kufanya kazi. Ndio sababu unaona tu watu wanavyogombana kuchinja mnyama as if kunawaongezea chochote katika maisha.
Ginehe nkoi,
Hata mzee wa Loliondo alipata sana kwa jina la Mungu.

Kwanza ni swala la kujiuliza, kwa nini viongozi wa hizi dini wanajikita sana katika kujua kwanza saikologia?.

kwa nini msisitizo wa mafundisho yao unakuwa umejisimika kwenye maisha ya baadaye yasiyojulikana kwa mwanadamu?.

Ninafikiri imani hizi za dini zimetawala fikra za watu masikini kiasi kwamba hawapati hata muda wa kutafakari kilichoko nje ya imani hizi za dini. Waumini wake wanajazwa hofu kwa yasiyojulikana.
 
Back
Top Bottom