Kwanini Ukristo na Uislam unashamiri kwenye nchi masikini na duni kielimu?

Kwanini Ukristo na Uislam unashamiri kwenye nchi masikini na duni kielimu?

Dini pia inatumika kama namna fulani ya kupunguza pressure za umasikini. Inatoa faraja na matumaini hata kama sio tangible, inaweka hofu fulani kwa wale wanaotaka kutenda maovu.

Kwa namna fulani zimesaidia kwa baadhi ya maeneo kupunguza vitendo vya kishenzi kama kufanya mauaji kwa Imani za kishirikina. Ukijaribu kupitia historia za makabila utaona kulikuwa na ukiukwaji mkubwa sana wa haki za Binaadamu hasa mauaji, Wanawake walinyanyaswa sana lakini ujio wa Dini angalau umepunguza hayo, na sababu moja kubwa.........Hofu ya Mungu.

Sikatai kwamba hata walio miongoni mwa Waumini kuna wenye tabia kama hizo lakini angalau wanajua si jambo linalokubalika kwa Mkuu wao kuliko wote - Mungu.

La nyongeza Dini imeziba ombwe la Uongozi hasa kwenye Umasikini. Tunajua kwa nchi masikini kama zetu mlipuko wa Kijamii kutokana na kukosa matumaini unaweza kutokea, lakini kwa mtazamo wangu Dini zimepunguza makali........Kuna matumaini fulani wameyajenga kwenye nyoyo za Watu.

Vipi kuhusu mapigano ya waislamu na wakristo mfano huko Nigeria? Au kwetu juzi tu huko Buselesele? Nadhani nadhani a yako kuwa dini hizi zimepunguza hivyo unavyoiita vitendo vya kishenzi haiko sahihi.
 
Mtazamo wangu ni kwamba umaskini tuliokuwa nao kwenye nchi zetu ni kwa sababu ya kutokufuata mafundisho ya nsing ya dini zetu. Tungekuwa tunafuata dini hizo mtoa mada alizozitaja, tusingekuwa na rushwa, mauaji, wizi, ukimwi etc. Yaani kwa kifupi uadilifu na ezalendo ungetawala na hatimaye tukapata maendeleo. Lakini kwa kuacha dini zetu, ndio maana leo tumebaki waumini wa majina na sio misingi ya dini. As a result tunaendelea kuwa maskini.
 
Vipi kuhusu mapigano ya waislamu na wakristo mfano huko Nigeria? Au kwetu juzi tu huko Buselesele? Nadhani nadhani a yako kuwa dini hizi zimepunguza hivyo unavyoiita vitendo vya kishenzi haiko sahihi.

Mapambano baina ya mifumo miwili yenye nguvu ndio itifaki ya kimaumbile,rejea vita vya kwanza vya dunia,vita vya pili vya dunia,vita baridi baina ya kambi ya mashariki na magharibi,na sasa vita vya marekani na kile wanacgokiita UGAIDI.
 
Labda uanze kujiuliza kwanini hizo nchi unazoziita zimeendelea ambazo hazifuati misingi ya dini zinatumia nguvu nyingi sana kuwekeza dini zao ambazo wao wenyewe hawazifuati katika nchi masikini?
 
Vipi kuhusu mapigano ya waislamu na wakristo mfano huko Nigeria? Au kwetu juzi tu huko Buselesele? Nadhani nadhani a yako kuwa dini hizi zimepunguza hivyo unavyoiita vitendo vya kishenzi haiko sahihi.

Ukila kiasi na kwa mpangilio (kama inavyopasa) utapata siha njema na kufanya kazi zako bila
tatizo. Ukila bila mpangilio tena kwa wingi bila nidhamu lazima utavimbiwa na afya yako haiwezi kuwa njema.

Ndivyo ilivyo Dini, na hapo kwenye bandiko langu nimeeleza kwamba wapo miongoni mwa waamini wakakengeuka
na kufanya yasiyokuwa hata kwenye mafundisho yao.

Nimeandika kwenye bandiko linalofuata hivi:

Kwa ufupi Msingi wa Hizi Dini ni kuishi kwa kufuata mafundisho yaliyojengwa juu taratibu maalum na zilizowekwa na Mungu (kwa mujibu wa mafundisho yao) i.e Kupendana, kujaliana, kushirikiana, uadilifu na kuonyana juu ya mienendo isiyofaa n.k (kwa mtazamo wao).

Na la pili ambalo ni kubwa ni kuwa na Imani, kuijenga Imani na kuishi kwa Imani. Na Imani kwa mtazamo wa Ukristo ni kuwa na matarajio juu ya mambo yajayo. Imani juu ya Maisha baada ya kifo, kwamba binadamu tunakufa hilo ni jambo linalojulikana, lakini baada ya hapo? ni Imani kwamba tukifuata misingi hiyo hapo juu tuna hakika ya kuishi baadaye

Kwa hiyo utaona hiyo ndiyo misingi mikubwa inayofuatwa na kamwe haihusiani na Vurugu, Vita. Lakini kwa nini vita huja?
Kwa sababu mpangilio na uenezaji wa Dini umepindwa....hakuna utaratibu maalum, na kuna Watu kwa maslahi yao
wanatumia mwamvuli wa Dini kutia hisia kali za kuonewa n.k. Na kama mfumo wa kufundisha na kunyoosha Imani imepi
ndwa na hawa ni Watu matokeo yake ndiyo hayo unayaona.

Dini si kubatizwa au Kusilimishwa. Ni lazima pawepo na mfumo kamili wa kuwaandaa Waumini kujua misingi yenyewe
na kuiishi. Waaamini wafundishwe kuwa Waumini na siyo mashabiki wa Dini. Kuwa shabiki wa Dini hakuhitaji akili kubwa
au busara (Nafikiri umeshawaona mashabiki wa hivi Vilabu vyetu vikubwa wanavyokuwa kma wendawazimu wakati fulani).
 
Hili suala ni mtambuka, Dini hutoa watu kwenye giza na kuwaingiza kwenye mwanga!

Dini huwafanya watu wakaheshimiana na kujaliana kama alivyo amrisha Mwenyezi mungu.
Dini huleta usawa na haki miongoni mwa waumini!
Dini huondoa matabaka katika Jamii.
DINI HULEA UKARIMU na Maelewano kwani mwisho wa siku Binadamu wote ni WAJA wa Mwenyeezi Mungu...

Kwakuwa dini hugusa hisia za watu, Strategists wanatumia migongo ya dini kutugawa! Wanatumia migongo ya dini kunyonya Rasilimali zetu, Wanatumia migongo ya Dini kuonesha kuwa kuna watu wa imani inayopingana na yao kuwa wana wadhulumu na kuwa dharau! Kwa kutumia Dini wazungu walikuja kwetu kututawala...

The bottom-line ni kuwa Dini yaweza kuwa chachu ya maendelea kama ilivyo kwa baadhi ya nchi hususan za Kiislam na wenye kutumia Islamic Bond kwa maendeleo mfano nchi za Mashariki ya Mbali.

Kwa upande wa pili wa shilingi dini ni chanzo kikubwa cha machafuko miongoni mwa Jamii hususan pale ambapo Nchi Tajiri zinapotumia dini kukwapua rasilimali and in return wanarudisha vijimisaada kupitia kwenye dini! Jamii hukosa maelewana na matokeo yake kunakuwa na matabaka kati ya waliopata misaada ya shule, mahospitali nk Vs wale ambao wanahisi wanadharauliwa!

...Social GAP ni tatizo kubwa sana linalisababishwa na dini kwa nchi nyingi masikini duniani...
Ninapenda ufahamu pia hayo uliyoyaelezea (Haki, usawa, heshima,kujaliana etc) hata kwenye nchi zinazoikimbia imani ya dini za kikristo na kiislamu yanapatikana zaidi ya nchi hizi masikini na zenye elimu duni. hii haiwezi kuwa ni sababu ya imani ya hizi dini kushamili katika nchi masikini na zenye elimu duni.

Ninadhani hujaweza kubainisha sababu zake za msingi kama swali langu la msingi nilivyouliza.
 
Mkuu Ng'wamapalala natofautiana na wewe kidogo hasa kwenye kuhusianisha dini na umasikini kwa sababu zifuatazo:

(1) Dini zote huhimiza waumini wake wenye kipato kutoa zaka ambazo zingeweza kusaidia wale wenye maisha magumu kama zingekuwa zinatolewa ipasavyo, hili lingeweza angalau kuondoa tofauti kubwa iliyopo sasa kati ya walio nacho na wasionacho
(2) Mataifa ambayo tunaweza kuyaita Mataifa asisi ya dini hizi na yanapractice mafundisho ya dini husika yana hali nzuri kiuchumi hii inakwenda kinyume na hypothesis yako kwani tungetegemea hayo mataifa yawe na hali mbaya zaidi kulinganisha na haya yanayojaribu kupokea dini kwa sasa.

Nakubaliana na wewe kwa asilimia 100 kuwa kwa sasa Ulaya nyumba za ibada zimegeuzwa makumbusho. Lakini hawa wenzetu wana logic moja wanayoiamini ambayo pia sikubaliani nayo: Wanasema "If God is everywhere why should I go to the church while I can stay at home with my Bible and pray?"

Kwa maoni yangu: Kinachotusumbua sisi watu wa mataifa masikini ni kutokushika kwa usahihi mafundisho ya imani zetu. Kwa mfano imani nyingi zinasema utoe asilimia fulani ya kipato chako kwa kuwapa watu masikini, mayatima n.k. Lakini tujiulize ni wangapi wenye nacho ambao hutoa hiyo asilimia? Na kama wanatoa ni kweli kinachotolewa kinawafikia wahusika?

Sasa nije kwenye hoja ya msingi ya kwanini imani hizi husambaa kwa kasi kwenye jamii maskini na zisizo na elimu?
(1) Binadamu yeyote aliye na shida hushawishika kirahisi kukubali hoja yoyote na wakati mwingine bila hata kufikiri ili mradi tu shida yake ipatiwe ufumbuzi. Imani hizi husambaa kwa kasi kwenye maeneo yetu kwa kuwa watu wana shida na kwa kuwa kusambaa kwa imani hizi huambatana na misaada watu hushawishika kuzipokea kwa kuwa zitapunguza machungu ya maisha.
(2) Elimu ni nyenzo muhimu ya kumsaidia binadamu kufanya upembuzi yakinifu pasipo na elimu binadamu hukubaliana na kila aambiwalo ili mradi apate unafuu kimaisha

Kikubwa zaidi kwa mataifa yetu haya ni kwamba viongozi wengi walio na nafasi katika ngazi mbalimbali za uongozi hawana huruma kwa wananchi wanaowaongoza na hii ni kutokana na ukweli kuwa wamekosa chembe ya imani ya dini zao katika mioyo yao.

HITIMISHO:
Mafundisho ya Dini UISLAMU na UKRISTO huwataka waumini wake kuwa na moyo wa upendo na huruma kwa viumbe wenziwao. Yakishikwa ipasavyo humtoa binadamu katika lindi la ujinga na umasikini na kumuweka huru kwa ajili ya kumuabudu mungu wake kwa mujibu wa imani yake.
 
Last edited by a moderator:
Pamoja na madai kuwa lengo la dini ni kujenga na kuhimiza maadili lakini ni ukweli vile vile kuwa katika nchi hizo zinajojishamirisha kuwa na watu wenye dini viwango vya crime viko juu vile vile. Corruption katika nchi zinazodai kuwa na dini sana iko juu. Utajiuliza hivi kweli dini inapigania maadili ikiwa nchi zenye dini sana zimezongwa na ufisadi na makosa mengi ya kijinai?

Kwa hiyo pamoja na kuwepo kwa dini bado binadamu tunahitaji mfumo bora zaidi wa kuongozana na kutawalana. Dini si tofauti sana na mifumo ya mila na desturi za makabila na jamii mbali mbali. Zinatofautiana tu mipaka kwa maana dini na hasa hizi mbili za ukristo na uislam ni mfumo wa mila (udhanifu) iliyofanikiwa kuvuka mipaka ya jamii ilikoanzia. Hata hivyo kadri binadamu anavyozidi kuendelea ukweli unazidi kujidhihirisha basi na dini zinazidi kufifia.

Ndo maana kiwango cha ustaarabu na maendeleo ya kiuchumi na kisayansi vinapozidi kujikita katika jamii, dini huanza kufifia na kutoweka. Tunaelekea kwenye dunia isiyo na dini. Dunia ambayo ustaarabu na maendeleo vinatokana na kushamiri kwa maarifa kuhusu mazingira, dunia na vilivyomo. Maarifa ya kisayansi na maendeleo ya kiuchumi yanayotokea hapo hufanya dini ibaki kama silaha iliyozeeka na isiyo na matumizi tena. Ndo maana kwa nchi maskini ambazo kiwango cha maarifa na maendeleo kiko chini dini bado inaendelea kutumika kujaribu kuleta utangamano katika jamii.

Dini ni chombo cha kuleta utangamano katika jamii, ila ni chombo ambacho hakijafanikiwa sana. Hata hivyo bado inafaa pale ambapo bado hakujawa na mbadala.
 
Hakuna uhusiono,research za kuimarisha dini zao za ukahaba na ushoga hizo wapelekee wenyewe.

UsSR ilianguka kwani ilichanganya Dini na Serikiali,Marekani nayo ipo ukingoni karibu itaanguka kwani imechanganya Dini na Serikali.

Kila Dola lenye nguvu linasimama na kuanguka,wale ambao Dola zao zilianguka sasa wanajipanga kuzirudisha.wewe kaa na kuwasifia wamagharibi tu kwa sababu wamekufadhili.
Nilipenda tu ufahamu kama kunijadili mimi hakuwezi kutoa jibu au kufuta ukweli ambao unabainishwa na research zilizofanyika. Hata kama nimefadhiliwa, hakuondoi pia ukweli wa mada iliyo mezani.

Wapi nimehusisha kuanguka kwa dola kumeshababishwa na kuchanganya dini.

Swali langu la msingi ni kutaka kubainisha sababu zinazofanya dini za imani ya kikristo na kiislamu kupata mafanikio sana katika nchi zilizo masikini na zenye jamii iliyo na elimu ndogo wakati huo huo zikidoda katika nchi zilizoendelea.
 
Wanataka kutuambia na hivyo viresearch vyao sisi sote tuwe watembea Uchi,Makahaba na Mashoga kama wao,hiyo ndio Dini yao,na huo ndio ustaarabu wa hali ya juu(From west is Best!).

Bora kuishi zama za mawe za kwanza kuliko kuwa na Maendeleo ya ain hii

Dini zinatufundisha tutafute maendeleo na tuwe na Maadili mema( inawezekena kwa wamagharibi kutembea Uchi barabarani,ukahaba na Ushoga ndio maadili mema acha waendelee nayo sisi hatuyataki).

Kwa ujinga hawa wamagharibi ndio hivi sasa utamkuta anampelka mtoto wa miaka miwili shule Bweni kukimbia kulea,wazazi hawana muda wa kulea watoto wao.Shame up on western culture.

I hate western Culture and they are Development,go to hell with them,you look shameless.
 
Nilipenda tu ufahamu kama kunijadili mimi hakuwezi kutoa jibu au kufuta ukweli ambao unabainishwa na research zilizofanyika. Hata kama nimefadhiliwa, hakuondoi pia ukweli wa mada iliyo mezani.

Wapi nimehusisha kuanguka kwa dola kumeshababishwa na kuchanganya dini.

Swali langu la msingi ni kutaka kubainisha sababu zinazofanya dini za imani ya kikristo na kiislamu kupata mafanikio sana katika nchi zilizo masikini na zenye jamii iliyo na elimu ndogo wakati huo huo zikidoda katika nchi zilizoendelea.

Umetumwa kuleta Dini za Kutembea Uchi barabarani,Ukahaba na Ushoga ili uendelee kupata ufadhili huko magharibi,haya ujumbe umefika nenda kachukue posho yako kwa mabwana zako mashoga na wasagaji ndio maendeleo yanu hayo
 
nguvukazi mikono, hebu jibu kuhusu hizo aina ya tozo (Riba in relative) nilizoweka kwenye bandiko langu, kabla hujatoa vifungu vya kukataza RIBA, ingawa unajua Islamic countries na Islamic banks zinatoza hizo kwa msingi wa Profit -Loss Sharing "PLS" Je hizo aya za quaran tukufu hawazijui?

Ng'wamapalala!! umeni elewa, na hii ni kwa sababu tuongea lugha moja, yaana tunalinganisha dini na maendeleo kufikia ustaraabu wenye utii wa sheria bila shuruti, ( maana dini yaweza kuwa shuruti, mfano toa 1/10 au sehemu ya faida wape maskini hiyo ni shuruti).

Hebu Hapa tusemezane kuwa kuna serikali inayo endeshwa kwa misingi ya vitabu vya dini, ambayo imeweza kutumia aya ( biblia/quaran) kuweza kuwa mfano mkuu wa mafanikio ya kutoka hatua moja hadi nyingine kuelekea ustarabuni.

Narudia sema wafuasi wa dini nyingi hawajui historia za dini, viongozi wao wachache wanajua na hawataweza kuwambia kamwe!!!
Mwisho, naomba Mtoa maada endelea kulinda watu wasiende kwenye dini, tujikente hapa, je Nchi yenye waumini wengi inaweza kuwa maskini au kwanini raia wake wawe maskini?.

Kuna mchangiaji anasema, Dini na umaskini usilinganishwe, mimi nasema la hasha!!! Labda mtu aseme kwanini unaenda kuomba Mungu? unataka akupe nini?

My Take:
Waumini wamejazwa hofu ya je ukifa utaenda wapi? MOTONI/JEHANAM. Je Kuliko toka hizo dini wanaishi vipi?
SP
 
Ng'wamapalala,,
Thanks kwa mada yako njema mkuu,

Lakini kwa maono yangu mimi ni kwamba zipo nchi ambazo zimeamua kuuchukua mfumo wa kisecular kama ndio suluhisho kuu na msingi mkuu wa maisha yao na kuzifanya dini kama fashion tu, au kitu cha kutumika kwenye matukio kama ya misiba, sherehe za ndo na n,k.,

Pia sijafaham vyema hapo kuhusu nchi hizo maskin umeangalia kitu gani hasa, zipo nchi kama Iran, Qatar, Saudi Arabia etc ambazo si maskini kwa kias hicho, kwa ufupi ni watu wenye per capital icomes kubwa lakini wana iman zao thabiti tu za kikristo na kiislam.

Thanks..
 
Last edited by a moderator:
Nimekusoma na nimekuelewa na kama sijakuelewa vizuri utanisahihisha.

Kwa mtazamo wako, dini za imani ya kikristo na kiislamu zina mafundisho ambayo hayatoi majibu wa wananchi zaidi ya kuwajenga hofu na kuwajengea imani kama kile ambacho hawana na hawakitegemei kukipata kuna nguvu fulani inaweza kuwapatia lakini wakati haujulikani. Kwa hiyo cha maana ni kuendelea kuomba na kusubiri. Na hata kama wataiacha hii dunia basi kuna nguvu fulani pia itawafariji kwa yale waliyoyakosa hapa duniani.

Kwa maana kuwa hata wanachokiomba hawakijui na wanaongozwa na matumaini. Kwa maana kuwa hizi imani za dini zinacheza na saikologia ya binadamu.

Pale jamii inapoanza kuelimika na kutagirika, nguvu za imani za dini nazo katika maisha yao zinaanza kupungua.
hapo uko sawa kabisa!!! watu hawajaenda mbali kujua historia za dini!! Amin wanao enda mskitini /kanisani na wanajua historia za dini hawafiki15%
Umetumwa kuleta Dini za Kutembea Uchi barabarani,Ukahaba na Ushoga ili uendelee kupata ufadhili huko magharibi,haya ujumbe umefika nenda kachukue posho yako kwa mabwana zako mashoga na wasagaji ndio maendeleo yanu hayo

mkuu mbona umekuwa mkali sana!!! mkanasha huu ndo unanoga punguza mukali.
Je wingi wa waumini haufanyi mvua inyeshe sana, mbegu (bila mahabara) zizae sana? sasa kwanini inchi ina waumini wengi, kuna mafuriko, njaa, magonjwa na umaskini mkubwa?
Twende taratibu, anaweza kesho akajiunga na dini yako akielewa. Unadhani mtume angekuwa na hasira wewe ndini ingekufikia?
Sp
 
Nguvukazi Mikono, hebu jibu kuhusu hizo aina ya tozo (Riba in relative) nilizoweka kwenye bandiko langu, kabla hujatoa vifungu vya kukataza RIBA, ingawa unajua Islamic countries na Islamic banks zinatoza hizo kwa msingi wa Profit -Loss Sharing "PLS" Je hizo aya za quaran tukufu hawazijui?

Mkuu unajua nini maana ya RIBA?
 
Mkuu kwa kiasi kikubwa dini inaendana na Saikoloji ya watu. Mara ningi binadamu akiwa na shida ndipo uhamua kumlilia Mungu. Watu masikini wanapenda kuwa karibu na Mungu ili kujipa Moyo . Mfano Makanisa ya Kilokole wao wanaubiri kuwa ukiomba utajiri Mungu anakupa, ndiyo maana utaona siku hizi Watu wanahama kanisa la Roma na kwenda kwa walokole ili wapate utajiri au hali yao ya kiuchumi iwe sawa.

Cha ajabu ni kwamba binadamu yuleyule alikuwa mcha mungu siku akipata pesa utaona hata kanisa analisahau. Ndiyo Maana hata kwenye bible inaonesha tajiri itakuwa ngumu kuuona ufalme wa mbinguni, kwa hiyo mara nyingi binadamu ujiweka karibu na mungu pale wanapokuwa na shida.

Kwa maelezo hayo ndiyo maana nchi masikini zinakuwa na dini sana kwani kisaikolojia binadamu uwa karibu na dini pale anapokuwa na shida. Hivyo nchi za ulaya kwa kuwa hawana shida sana wao wamehamua kuhasi, hawaoni nini Mungu atawasaidia, lakini ole wao.

Ulaya wanaamini sana sana katika juhudi na technolojia kuliko miujiza

Ni UWONGO mkubwa!kudai biblia inasema ni vigumu tajiri kuuona ufalme wa MUNGU na ni rahisi kwa maskini!badala yake unahitaji kutafuta ukweli wa kauli hiyo ya Yesu na utashangaa kukuta hata umaskini ni laana!kuna uhusiano mkubwa sana katika kuwaza utajiri na kuupata utajiri wenyewe ama kuuwaza umaskini na kuumiliki umaskini huo!(Mf msemo wa aliye juu mgoje chini ni wa maskini tuu!)Huwezi kutoka kwa mawazo kama hayo!'When one is truly ready for a thing,it puts in its appearance' Wazungu wanaamini hivyo na miujiza hutokea!Wacheni maneno maneno ya kiswhili hapa!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Mkuu Ng'wamapalala natofautiana na wewe kidogo hasa kwenye kuhusianisha dini na umasikini kwa sababu zifuatazo: (1) Dini zote huhimiza waumini wake wenye kipato kutoa zaka ambazo zingeweza kusaidia wale wenye maisha magumu kama zingekuwa zinatolewa ipasavyo, hili lingeweza angalau kuondoa tofauti kubwa iliyopo sasa kati ya walio nacho na wasionacho (2) Mataifa ambayo tunaweza kuyaita Mataifa asisi ya dini hizi na yanapractice mafundisho ya dini husika yana hali nzuri kiuchumi hii inakwenda kinyume na hypothesis yako kwani tungetegemea hayo mataifa yawe na hali mbaya zaidi kulinganisha na haya yanayojaribu kupokea dini kwa sasa.
Nakubaliana na wewe kwa asilimia 100 kuwa kwa sasa Ulaya nyumba za ibada zimegeuzwa makumbusho. Lakini hawa wenzetu wana logic moja wanayoiamini ambayo pia sikubaliani nayo: Wanasema "If God is everywhere why should I go to the church while I can stay at home with my Bible and pray?"
Kwa maoni yangu: Kinachotusumbua sisi watu wa mataifa masikini ni kutokushika kwa usahihi mafundisho ya imani zetu. Kwa mfano imani nyingi zinasema utoe asilimia fulani ya kipato chako kwa kuwapa watu masikini, mayatima n.k. Lakini tujiulize ni wangapi wenye nacho ambao hutoa hiyo asilimia? Na kama wanatoa ni kweli kinachotolewa kinawafikia wahusika?
Mkuu hayo unayoyasema yameandikwa kwenye misahafu ya dini lakini ni nani anayesimamia?. Kama ndiyo nguzo zake kuu, huoni kama kuna uwalakini katika mafundisho yake.

Angalia utajiri wa viongozi wa madhehebu ya Kikristo na Kiislamu ulinganishe na waumini wake duniani.

Ninafikiri hutofautishi au unachanganya nation inherited wealth na nation self made wealth. Nchi tajiri na ambazo dini hizi mbili zinashamili itakuwa ni nchi yenye utajiri wa kuridhi kama mafuta.

Hili halina ubishi hasa kutokana na mazingira na nguvu za kisaikologia kuwa kwenye kitovu cha hizi dini lazima tu wananchi waliopo pembeni watakuwa wako active na hizi dini ikichukuliwa kuwa, sheria za nchi hizo zimetungwa kulingana na mafundisho yaliyomo kwenye misahafu.

Sasa nije kwenye hoja ya msingi ya kwanini imani hizi husambaa kwa kasi kwenye jamii maskini na zisizo na elimu?
(1) Binadamu yeyote aliye na shida hushawishika kirahisi kukubali hoja yoyote na wakati mwingine bila hata kufikiri ili mradi tu shida yake ipatiwe ufumbuzi. Imani hizi husambaa kwa kasi kwenye maeneo yetu kwa kuwa watu wana shida na kwa kuwa kusambaa kwa imani hizi huambatana na misaada watu hushawishika kuzipokea kwa kuwa zitapunguza machungu ya maisha.
(2) Elimu ni nyenzo muhimu ya kumsaidia binadamu kufanya upembuzi yakinifu pasipo na elimu binadamu hukubaliana na kila aambiwalo ili mradi apate unafuu kimaisha
Kikubwa zaidi kwa mataifa yetu haya ni kwamba viongozi wengi walio na nafasi katika ngazi mbalimbali za uongozi hawana huruma kwa wananchi wanaowaongoza na hii ni kutokana na ukweli kuwa wamekosa chembe ya imani ya dini zao katika mioyo yao.
HITIMISHO:
Mafundisho ya Dini UISLAMU na UKRISTO huwataka waumini wake kuwa na moyo wa upendo na huruma kwa viumbe wenziwao. Yakishikwa ipasavyo humtoa binadamu katika lindi la ujinga na umasikini na kumuweka huru kwa ajili ya kumuabudu mungu wake kwa mujibu wa imani yake.
Kwa hiyo nikisema kama hizi dini zinashamili sehemu ambazo ni masikini na zenye elimu duni kwa sababu zinatumia madhaifu ya wananchi kujipenyeza na kukubalika zaidi.

Mkuu omiath , kwa hiyo ina maana hizi dini zinakuwa na ajenga za siri siyo kama zinavyobainisha kwenye mafundisho yake ya kumkomboa mnyonge na masikini?.
 
Last edited by a moderator:
Hebu tuangalie, ni kweli nchi zenye waumini wa dini hizi mbili ni maskini,hebu angalia nchi gani hasa ambazo zinaongoza kwa wanachi wake kuwa na kipato cha zaidi ya dola 5 kwa siku? Utakuta ni nchi za kiislamu na ni nchi hizo uislamu bado upo.

Pia ukiangalia nchi za ulaya kwanini hasa wametupa dini? Utakuta wao wanapenda sana kuongozwa na nafsi inavyota na si kwa mashart ya dini pia hata tabia na ubinaadamu haupo ktk nchi hizo,mfano wakuta mtu mazazi wake kafikia uzee badala ya kumlea anampeleka kwenye makambi, ngono kuwa kitu cha kawaida,hivyo haya ni madhara ya kuacha dini.

Tukija ktk suala la waumumi kuwa masikini(si wote)hili linatokana na dinni kukataza machumo ambayo ni haramu, kuiba, kudhulumu, kutapeli, ufisadi, riba, biashara za mihadarati, haya yote hufanywa na watu wasio na dinni na ndio unakuta matajiri, ila utajiri huo una madhara makubwa sana katika jamii.

Riba humfanya tajiri aendelee kuwa tajiri na kunyonya maskini, hapo huwezi kupata jamii yenye usawa kuiba. Hii inafanya yule menye kuhangaika na kipato chake mwizi aje achuku pasina kufanya kazi, lakini kama angefuata dinni asinge fanya hivyo.

Ufisadi, viongozi hawana dini, madhara yake unakuta wananchi wanakuwa hoi viongozi wapo juu,lakinikm dinni ingefuatwa haya yasingekuwapo.

La mwisho, mtu anaona bora asifanye hayo kwa ajili ya utajiri wa hapa bora apate kidogo cha halali lakini siku ya mwisho aishi ktk maisha mazuri peponi.

Hivyo, umasikini hausababishwi na watu kuwa maskini, bali kutofuata dini ndio kunasababisha watu kuwa maskini.
 
Mkuu unajua nini maana ya RIBA?

mkuu naomba nijibu bila kutafuta angalizo, yaani nitoe maana kwa mazingira.
Riba ni rejesho la ziada kwenye Amana, yaani ni ziada ya mali/dhamani ya kitu ulichopewa na mtu/tasisi.
hii inafidia mtu kuacha kutumia amana yake leo akaukupa wewe nguvukazi mikono utumie leo halafu mrudishie siku za mbeleni.
kwanini nimeihusisha na ijir, murakhabar etc, kwenye mfumo wa benki za kislam, mfanya biashara aliyekopa akipata faida tunagawana( benk na mteja) hivyo benki inapata fedha zilizokopwa jumlisha faida ya hiyo biashara ya mteja!!! kwa kifupi inapata principle plus share of profit!!!
Traditional banks, haziangalii faida, ila zinategemea utapata faida na utalipa kiasi ulicho kopa jumlisha ziada ( toka kwenye faida ya bishara/shughuli yako)
wewe unajua je mkuu? nipe darasa
SP
 
Back
Top Bottom