Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?


Watu washaitwa kazini na oral imefanyika week ilopita duuh.
 
mmmh Inawezekana ikawa kweli lkn interview watu wa mwisho wamefanyw jumatano yan ndan ya siku 4 tu majibu yawe tayar daah
Huu ulimwengu bana mambo ni mengi sana unaweza ukachanganyikiwa ukisikiliza rumours za watu, usaili wa mwisho umefanyika J5 , usaili ulikuwa na idadi kubwa sana ya wasailiwa mfano tax management officer II oral ni 847, leo hii hata wiki haijaisha una ambiwa watu wameshaitwa kazini, any way sisi hatujui bana ila jambo la msingi ni kusubiria taarifa toka chanzo rasmi ambacho ni website ya TRA tu, amabako hayo majina lazima yatawekwa huko kwa kuwa toka mwanzo wa mchakato kila kitu kilikuwa kinapatikana huko, hata hao unaosema kuwa wamepata yawezekana ni story tu wanazungumza zisizokuwa na uhakika.
 
Hapa ndy nakosaga Nguvu watu tunasubiria matokeo nyie mna taarifa za watu kuitwa kazini
 
Hapa ndy nakosaga Nguvu watu tunasubiria matokeo nyie mna taarifa za watu kuitwa kazini

Ngoja nikushirikishe machache tu ambayo yanaendelea huku maofisini ujue jinsi Dunia ilivyokuwa haina USAWA....

Mimi binafsi ni mwaka wa 3 huu natafuta uhamisho (nishafanya Kazi miaka 10, kwahiyo Nina sifa zotee za kupata uhamisho) ila sasa...

Nikiwa na hustle na kutafuta uhamisho

1. Kuna watu wanapata Kazi (ajira mpya) wanakuja kureport, anarudi home kusubiri cheki namba.
Ile anaipata, hata hajaanza Kazi, anakuja na barua ya uhamisho kahamishiwa Taasisi fulani. Kwa halmashauri anatemana nayo kihivyo

UNADHANI HUYU HATA AJIRA ALIIPA NJIA KAMA YAKO?

2. Mmepata ajira mpya, wewe unawaza umfundishe Kazi ili umuachie ofisi uhame.
Na uhamisho hutoka baada ya mwaka wa ajira (ukishathibitishwa).
Ndani chini ya mwaka mtu anakuja na barua ya uhamisho na anasepa anakuacha wewe wa miaka hapohapo.

3. Siku umekaa unahili wala lile, unashangaa DED kamind. Kisa kapokea simu kutoka juuu huko "mtumishi fulani anatakiwa ahame haraka"

Braza hii Dunia japo Kuna Mungu, ila Kuna watu Wana WATU, sio watu ni WATU.

Mungu akujalie upate ajira, ipo siku UTANIELEWA.

Karibu kwenye Utumishi wa Umma.

#YNWA
 
Wameitwa lini kazini ili hali usaili wa oral toka ufanyike leo ni siku ya 6, na kwenye website ya TRA hakuna tangazo la watu kuitwa kazini mpaka sasa.
Hakuna aliyeitwa kazini.
Umenielewa, wao washajua wamepata.
Wamejuaje wanajua wenyewe.

Kama wewe unavyohangaikia kupata Kazi kimyakimya kwa kutumia njia zako unazozijua mwenyewe, Ndio hata sisi kwenye ajira tunavyohangaika na uhamisho kupitia njia zetu tunazozijua wenyewe.

#YNWA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…