Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Mm naonaga vile vijamaa kama vishamba Fulani muda wote kujichekesha kwa mademu pale asha migiro.

Wakiona msela wanakukazia
Ehhh ugonjwa wao ni wale watoto wa Kike, na waga vinawamega baada ya interview kwa sababu baadhi yao hujirahisi kwa kuhisi watapata kazi
 
Ngozi nyeusi na madaraka/nafasi waga tunaona Maisha tumeyapatia sana
Acha tu mzungu anajua kucare hawana longo longo za kikuda wala majivuno kama ma Hr wakibongo.Mbongo akiona mtu anataabika ndio roho yake inafurahi.

Sijawahi kufanya interview hata moja ila hii ya bomba la mafuta la east africa ndio imekuwa ya kwanza aloo mzungu mzungu tu.

Tulikuwa wengi tulioitwa kwenye interview almost 300 ila hata kama uko kijiji gani utalipiwa nauli hadi ufike dar kwenda na kurudi usafiri wowote utakaopenda ila usipande ndege tu[emoji3][emoji3].Hii ni kwa both oral and written.

Ukilala hotelini hata kama ni guest ya 5000 ,watakulipa 70,000 per night. Hotel tuliokuwa tukifanyia interview sasa ni seacliff [emoji3][emoji3]. Pesa ya kula 30,000

Na hapo Hotelin unakuta wamekuandalia Chai nzito vitafunwa vya kila aina, maji, chocolate,pipi yaani watakulazimisha ule hata kama hutaki utakula tu.

Hoteli ile ni kubwa ila kuanzia getini utakaribishwa kama mfalme. Kuna wale ambao kwa namna moja ama nyingine walikuwa wanashindwa kufika kwenye interview yaani utapigiwa simu wanakuuliza kama utaweza wakupangie siku nyingine. Kuna jamaa alisema siwezi kuja sababu sijajiandaa wakawa wanambebeleza njoo hivyo hivyo ujaribu bahati yako.

Maswala sijui ya kubeba mavyeti hawataki ni wewe na I'd yako yoyote. Ukimaliza interview unaenda kwa cashier anakulipa pesa zako zote ndio unasepa.

Kwenye oral interview kila mtu alikuwa amepewa saa moja kwenye venue uliopangiwa mfano ukachelewa wanam interview mwenzako aliewahi halafu wew watakuinterview baadae sio kama wabongo eti ukichelewa hata kwa bahati mbaya ndio imekula kwako na mabango juu.

Wakati wa interview sasa nilikuwa najiuliza nitaongea kizungu gani mimi na wazungu kwenye lisaa lizima wakati kizungu chenyewe sijui aloo wale jamaa wanajua kucare [emoji3][emoji3][emoji3]interview zote zingekuwa hivyo daa wakiona kuna swali unatapa tapa kujibu wanapredict unachojaribu kujibu wanakuolezea mpaka mwenyewe unasema yes yes yes ndio hiyo.

Au wakiona umechoka kidogo wanakwambia pumzika dakika tano kunywa maji Kisha tuendelee. Ambao tumepita oral interview last month tumeambiwa tutafute best private hospital yoyote iliyo kwenye mkoa uliopo Kisha tuwatumie ndio tunasubiri majibu yao twende kwenye medicals.



Sent from my SM-A025U using JamiiForums mobile app
 
si ndio hata mimi nashangaa yaani utumishi hata ubwabwa kutupikia wanashindwa jaman.yaani pale wengine wanafeli kwasababu ya njaa.. 🀣 🀣
 
si ndio hata mimi nashangaa yaani utumishi hata ubwabwa kutupikia wanashindwa jaman.yaani pale wengine wanafeli kwasababu ya njaa.. [emoji1787] [emoji1787]
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji1787][emoji1787][emoji1787]njaa znauma kweli,ila mm mbn hamu ya kula inakataga
 
Dahh wazungu ata ukikosa kazi unakosa ukiwa umeridhika kabisa maana kila kitu kilikuwa fair upande wako

ila sisi lazima tukupanikishe kwanza, tukufanye uonekane huna unachokijua na wala haustahili kupata hiyo kazi
 
Ilikuwa position gani mkuu?
 
Dahh wazungu ata ukikosa kazi unakosa ukiwa umeridhika kabisa maana kila kitu kilikuwa fair upande wako

ila sisi lazima tukupanikishe kwanza, tukufanye uonekane huna unachokijua na wala haustahili kupata hiyo kazi
Pale asha rose migiro, mkiwa wengi kada tofauti mnapelekeshwa kama watoto na kufokewa juu na walinzi wao. Mnapigwa jua na baridi la dom kabla ya kuingia kukandwa unawaza umaskini wako na familia yako unaona tu hamna namna nikuikubali tu system.
 
Hivi huwa wanapita humu kuna mengi sana wanatakiwa kujifunza, jamaa wanachofanya kwanza ni kukuogopesha toka wanaanza ukaguzi wa vyeti na vitu vingine, mpaka kuingia kwenye chumba cha interview unakua haupo katika utulivu.

Huwa nawaangalia najiuliza hawa watu nao walifanyiwa interview kama wanavyo tufanyia sisi au ni roho mbaya tuu na sifa zimewajaa....
 
Dahh wazungu ata ukikosa kazi unakosa ukiwa umeridhika kabisa maana kila kitu kilikuwa fair upande wako

ila sisi lazima tukupanikishe kwanza, tukufanye uonekane huna unachokijua na wala haustahili kupata hiyo kazi
Yaan ukweli kabisa..ndo maana maisha yetu yapo jinsi yalivyo ni huzuni sana
 
Mm mwaka jana niliitwa interview posta kufika tu.

Nikapokelewq kwa ukarimu sana na yule receptionist sijakaa sawa naambiwa muda wa Chai.

Nikaingia kwa panel ya interview ilikuwa ni org naulizwa relax dk 5 then wakaniuliza maji au juisi nikasema maji yakaletwa.

Tukaanza interview jaman private sector wako vzuri maana wanakucare mara utasikia jaribu basi mara kakuongezea point.

Nimemaliza interview na lunch nikala.

Nauli nikapata kazi nikakosa .

Feedback nikatumiwa kwa Email hadi marks zangu.

Jamani watu wako serious na kazi zao
 
Pale migiro full utishana.

Interview inaanza saa nne asubuhi saa 12 watu mpo mnapigwa na baridi.

Wakija saa 2 wanajiongelesha ongelesha.

Mara waanze kupanga logistics zao.

Haujakaa sawa mara wamechukua sjmu. Mara wakupeleke bondeni mara wakurudishe juu ni vurugu.

Hapo saa sita wanaanza kujitambulisha panelist mara mpelekwe pembeni.

Yaani ni vita Mpaka unamaliza interview watu hawacheki wala hawaongei hata kukutia moyo.

Kijana wa watu unajiondokea zako pale unapanda kabajaji kako CBE huyo dar es salaam
 
Unaanza kusubiri matokeo miezi mitatu oral hamna Malibu.

Siku unaangalia majibu unamuona jamaa aliyekuwa anajisifia ana mjomba utumishi jina lake la kwanza.

Unasema labda nikae nieendelee kusubiri mikeka mingine maskini.utumishi imekufa Haiti tena mikeka ihali in database kubwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…