Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Waajiri wanatofautiana.

Wengine wanaharakisha michakato yote na kukamilika kwa wakati.

Wengine miyeyusho pia, wanachelewesha michakato.

Mshahara unaweza kupata hata kama bado upo nyumbani unasubiri kuitwa/kupigiwa simu endapo huyo mwajiri amekamilisha taratibu zako za ajira(yaani umeungwa kwenye system ya payrol)

Hela za kujikimu ndio inategemeana na Mwajiri, kama yuko poa atalipa kwa wakati, kama ni miyeyusho basi mtajua mtiti wake
 
Kama ni halmashauri subiri mshahara uingie ndio uende kuanza kazi, Ukitegemea pesa ya kujikimu utateseka mkuu.

Kuna watu wanaenda kustafu hizo pesa za kujikimu hawajawahi kupewa.
 
sawa sawa nimeelewa 🙏
 
Nafasi inaweza ikawepo na isiwepo, kama watapata mtu ambaye haihitaji hizo process zote au ameshazikamilisha kwanini wamuache waendelee kukusubiri wewe??? Hii ndo Ile "Hoping for the best but expecting the worst"
Ikitokea wamepata mtu, hapo inakuwaje?
Tujaribu kushauriana
 
Hapo kwenye kupush barua ndio changamoto kama huna mtu wa ndani utumishi. Simu wanapokea ila majibu ni yale yale kuwa mvumilivu inashughulikiwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…