Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Yaani hawa Kenge utumishi ,wamekuwa ni waalimu na manesi tu kila siku vipisi vipisi vya pdf ,bora wangewabakisha huko huko Tamisemi
Wanashindwa nini kutoa pdf moja na be done with it ,kuliko huu upuuzi wa kukata vipande visivyo na maana
mtu unaweza ukang'ata simu 🤣 🤣 🤣
 
Upo sahihi sana, lakini ulipaswa kuongezea kuwa wizara ya afya ina ngazi tofauti ya hospitali na pia ina taasisi na mamlaka zilizo chini yake.

Watumishi wote wa kada za Afya waliopo wizarani (makao makuu), hospitali za mikoa, na wale waliopo Tamisemi wanalipwa mishahara yao kwa ngazi za TGHS, wote wanafanana mishahara yao.

Watumishi wa kada za Afya waliopo katika hospitali za kanda, hospitali maalum za kitaifa (Mirembe, Kibong'oto etc), na hospitali ya taifa wanalipwa kwa ngazi za mshahara za PGMSS ambazo zipo juu kuliko zile za TGHS.

Watumishi wa kada za afya waliopo katika taasisi na mamalaka zilizo chini ya wizara ya afya (NHIF, TMDA, MSD, NIMR etc) wanalipwa kwa scale za mishahara maalum kutegemeana na taasisi ama mamlaka husika, mara nyingi zipo juu kuliko za hospitali za hapo juu.
Nimetumia neno serikali kuu kwa sababu. Taasisi zilizo chini ya wizara ya afya wanasimama kama waajiri kwa hiyo hawa hatuwajumuishi kwenye maelezo.

Naunga mkono hoja.
 
Awali yoyote nipende kuwashukuru wana jamiiforum kwa mawazo na hint mbalimbali toka mwanzo wa usahili na hatimae na mimi PDF zilizo toka jana jina langu limo hakika jamiiforum nisehem makini sana
Hongera Sana mkuu kila la kheri katika majukumu yako mapya, ukawe mtumishi mwema na mwadilifu ukachape kazi mkuu
 
Wakubwa namshukuru Mungu nami nimebahatika kulamba asali naamini Mungu ni mwema kwetu sote na kila mmoja kwa wakati wake naye atailamba asali

Sambamba na hilo nahitaji sana msaada wenu wakubwa kwani katika hizi harakati za kuendelea kusikilizia asali mimi niliona nichukue muda huo kuendelea na masomo kwa ngazi ya shahada ila hilo halikunizuia kujaribu bahati yangu nilipoona nafasi zimetangazwa na kwa bahati Mungu akajalia

Sasa mwaka huu ndio nimeingia mwaka wa mwisho wa masomo kwa ngazi hiyo ya shahada, nimesikia sikia story nyingi nyingi kuhusu uwezekano wa kuomba nafasi ya kumaliza masomo kisha kuingia kibaruani rasmi, ila sijaweza kupata maelezo yaliyonyooka kuhusu hilo ndipo nikaona ni vema niwaulize wataalamu humu ili mnisaidie mwongozo juu ya hilo au ufafanuzi zaidi ili nipate kuelewa, Natanguliza shukrani wakubwa
 
Habarini za asubuhi, tupeni mrejesho mliofanya written, wale wa TBC, TCRA, DATA ANALYST, Benjamini hospital etc.
Je maswali yalikua ya kuchagua (aptitude test) au kuna kada baadhi mlifanya written ya kuandika mfano explain, define, mention etc
 
Wakubwa namshukuru Mungu nami nimebahatika kulamba asali naamini Mungu ni mwema kwetu sote na kila mmoja kwa wakati wake naye atailamba asali

Sambamba na hilo nahitaji sana msaada wenu wakubwa kwani katika hizi harakati za kuendelea kusikilizia asali mimi niliona nichukue muda huo kuendelea na masomo kwa ngazi ya shahada ila hilo halikunizuia kujaribu bahati yangu nilipoona nafasi zimetangazwa na kwa bahati Mungu akajalia

Sasa mwaka huu ndio nimeingia mwaka wa mwisho wa masomo kwa ngazi hiyo ya shahada, nimesikia sikia story nyingi nyingi kuhusu uwezekano wa kuomba nafasi ya kumaliza masomo kisha kuingia kibaruani rasmi, ila sijaweza kupata maelezo yaliyonyooka kuhusu hilo ndipo nikaona ni vema niwaulize wataalamu humu ili mnisaidie mwongozo juu ya hilo au ufafanuzi zaidi ili nipate kuelewa, Natanguliza shukrani wakubwa
Inawezekana kama ukikutana na mkuu wa idara na afisa utumishi wazungu
 
Wakuu naomba kuuliza. Ukifanya written interview, je kama kuna practical wana shortlist majina au wote waliofanya written wanafanya practical?
Sasa maana ya mchujo(Written) ni nini..

Usahili uko hivi..

Kama mpo wachache mtaanzia Practical ( kwa sahili zenye Practical ) au Oral kwa sahili ambazo hazina Pratical.

Ila kama mpo wengi lazima mchujwe, muanzie Written then zitafuata hatua zingine (Practical, Oral)
 
Wakubwa namshukuru Mungu nami nimebahatika kulamba asali naamini Mungu ni mwema kwetu sote na kila mmoja kwa wakati wake naye atailamba asali

Sambamba na hilo nahitaji sana msaada wenu wakubwa kwani katika hizi harakati za kuendelea kusikilizia asali mimi niliona nichukue muda huo kuendelea na masomo kwa ngazi ya shahada ila hilo halikunizuia kujaribu bahati yangu nilipoona nafasi zimetangazwa na kwa bahati Mungu akajalia

Sasa mwaka huu ndio nimeingia mwaka wa mwisho wa masomo kwa ngazi hiyo ya shahada, nimesikia sikia story nyingi nyingi kuhusu uwezekano wa kuomba nafasi ya kumaliza masomo kisha kuingia kibaruani rasmi, ila sijaweza kupata maelezo yaliyonyooka kuhusu hilo ndipo nikaona ni vema niwaulize wataalamu humu ili mnisaidie mwongozo juu ya hilo au ufafanuzi zaidi ili nipate kuelewa, Natanguliza shukrani wakubwa
Ebu anzia kwa mwajiri kuuliza hili jambo atakupatia majibu sahihi
 
Habarini za asubuhi, tupeni mrejesho mliofanya written, wale wa TBC, TCRA, DATA ANALYST, Benjamini hospital etc.
Je maswali yalikua ya kuchagua (aptitude test) au kuna kada baadhi mlifanya written ya kuandika mfano explain, define, mention etc
wale wa online tumefanya kuchagua
 
Back
Top Bottom