Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Nionyeshe Status iliyoandikwa Employed au mtu aliyepata ajira kupitia notification ya status nikuonyeshe video ya Majaliwa akifungua mlango wa ndege na kasia.
Na nikwel mie nilimuuliza rafik angu mmoja kapata ajira na ana Kama wiki 3 kazini ,anitumie status yake kweny a/c yake kuona imebadilika au vp alivyonitumia haijabadilika chochote, imeandikwa tu SELECTED FOR ORAL bas na Yuko kazini ,mkeka wake ulitoka nomas sana kweny mambo ya status 😀😀
 

Kufuatilia Status baada ya Oral ni kitu ambacho mpaka sasa hakina maana yoyote ni kama kujitekenya tu.
 
Mimi jamani Nina barua mkononi narudia Tena ukishafika oral status hazina maana Tena Kuna wadau status zao zipo shortlisted wanabarua mie IPO selected for oral ninabarua haya pia hapa mdau kwenye huu Uzi aliyekosa kazi IPO shortlisted achana na status
 
Umemaliza mkuu. Acha vijana wasumbuane tu kwa mada sizizo na tija
 
Hii asali umelamba
 
Tuishi humu,tusubiri pdf
 
Kuna mambo mengi ya msingi ya kujadili. Hatuwezi kubadilisha hizi status kwa kuzijadili. Watu wanajifariji tu Kwa kuangalia hizi status lakini hazina maana au maana yake bado haijulikani.

Kwa Sasa tungejadili namna ya kufaulu written na oral interviews.

Nafasi nyingi zinakuwa re-advertized, shida nini? Watu wanafeli, watu wenye sifa hawapo au watu hawako interested kuomba kazi?

Hata watu wa utumishi (au wenye mamlaka) wakipitia hizi nyuzi, wataona vijana bado hawako vizuri na hawajui hata haki zao.

Kama tutaamua kuleta mijadala yenye kujenga, Kwa kutumia lugha safi na yenye staha (polite language), basi tunaweza kuwashawishi hao wenye mamlaka kututatulia shida zetu.

1. Kuna suala la interviews nyingi kufanyika Dodoma, kama tutajadili vizuri tunaweza kufikiriwa na interviews zikafanyika kikanda. Hii itasaidia kupunguza gharama.

2. Nafasi nyingi zinakuwa re-advertized. Nadhani ni Kwasababu watu wenye vigezo hawapo au watu wanafeli, je hatuwezi kulijadili hili ili kama watu hawapo wa kujaza nafasi hizo basi mamlaka waweke vigezo rahisi, mfano waajiri sana watu wenye degree za awali kuliko wa masters na PhD.

Uzuri wa jamiiforums sio kama groups za Whatsapp, ni forums ambazo kila mtu anaweza access, Rais, mawaziri, wakuu wa taasisi na watu wengine wakubwa. Mimi naamini kama tutaamua kuutumia vizuri huu mtandao, tunaweza kuchangia vitu vingi chanya katika mambo mengi na vikakubalika.
 
 

Interview bila placement haikubaliki,
 
Vitu vya maana ndio hivi sasa
 
Umasikini mbaya tuendelee kuukataa, jobless mwenzetu anatutukana!
Sawa sisi ni jobless Ila hayo mamabo ya status tuachane nayo yatawatia pressure na mkajinyonga Bure.. mbona watu wanapangiwa tu vituo hata kutoka kanzidata na hzo status hazionekanai Kam zina impact yoyote..
Humu tunataka tips za Interview, placements, maswali ya oral and written ili watu tufike Oral.. mambo za kupangiwa kituo bahati pia inahusika.. so Punguzeni Ushamba basi..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…