Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Wakuu naulizia je baada ya kufanya Oral inaweza kuchukua muda gani mpaka kuitwa kazini lakini pia kwa uzoefu ikishapita baada ya muda gani basi itakuwa inamaanisha kuwa hata kwenye database haupo? Mwenye ufahamu juu ya hili naomba anijuze.

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
 
Inategemea na taasisi ila sio chini ya miezi 2 mpaka 3. Na database ni haizidi mwaka mmoja
 
Panels zinakuwa kati ya 5-10 so Muda unatosha.
Wanagawa wanaokandwa kwa grupu za watu 20 Kila grupu.
 
Kuitwa kazini inategemeana na uharaka wa taasisi yako unaweza kuchukua mwezi,miezi miwili,mitatu ,minne au hata mwaka😂
Na kukaa data base hesabu miezi sita baada ya placement kutoka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…