Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Kariakoo usije, utachoka kabla hujafika. Sema bana leo ndo nmewaza ningekuwa na kazi aisee, Kariakoo hakupitiki na watu wanataka order zao. Yaan badala ya kugongwa na gari ama boda unagongwa na watu ama mizigo[emoji23][emoji23][emoji23]
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
bora ugongwe na hao watu/mizigo huwezi kuumia ukilinganisha na gari.
 
Kuna Mwl wangu fulani nilipokuwa Form 2 aliwahi kusema "Kufaulu mtihani sio kufaulu maisha", kwa kipindi hicho hiyo kauli sikuweza kuielewa ila nilikuja kuielewa tayari nikiwa nishapata elimu ngazi ya degree.

Mimi ni miongoni mwa Mwanafunzi pekee niliyebahatika kuchaguliwa shule ya Bweni kutoka kijijini kwetu, wengine walitupwa shule ya kata, wengine wakatupwa kitaa(hawakufaulu almaarufu kuPASS kwa enzi hizo).

Cha ajabu sasa ambao hawakuPASS wengi wao ndio wakawa wa kwanza kutoboa life.

Tuliong'ang'ania njia ya kalamu kama njia ya kutoboa ndio tumebaki wa mwisho kwenye hizi races za kutoboa, huku tunabaki kutojua kumbe tulipoteza sana muda ingawa tukipata mirija ya Asali tutaweza kufanya come back ya kibabe kama Mbappe juzi.

Takwimu zinaonesha kuwa, darasa letu Primary tuliofanikiwa kupata degree moja kwa moja ni 2 tu (Mimi na mwingine alisoma Ualimu). Wote na degree zetu bado tunapambana kusaka mirija ya Asali, yule wa Education ajira za moja kwa moja tunajua Mwendazake alizisimamisha ,juzi kwenye Interview za Bunge niliona kaitwa kwenye mkando(sijui kama alienda au la).

Kwa kifupi tuliokuwa wa kwanza zamani, sasa tumekuwa wa mwisho. Life halina formula.

Sifikirii kurudi shule, hii degree 1 inanitosha, sasa naisaka degree ya mtaani kwa mgongo wa mrija wa Asali.

Hahahahaha! Sawa Mkuu, kwa kifupi ulichomaanisha ni elimu ilichokufanyia umekoma, ni bora ufanye mambo mengine kwa sasa.

Japo haya mambo ndivyo yalivyo, kuna kusahau. Hata ukikutana na mwanamke aliyetoka kujifungua muda si mrefu anaweza kujiapiza kwamba kwa maumivu aliyoyapitia kubeba ujauzito mpaka zoezi la kujifungua hatorudia tena.

Lakini baada ya muda mfupi sana, kusahau na mambo mengine yakobaiolojia humfanya atamani kuongeza mtoto.

Ninachomaanisha, ukishaingia kwenye pipa la asali utajikuta ajira inakushape, unaanza kuwaza kupanda juu zaidi kwa kuongeza elimu.
 
Ndio hivyo mkuu, labda mzee wa flash atusurprise hizi siku chache zilizosalia

Hahahaha! Kwa mwenendo wa Mzee wa pdf huwa anatabia ya kufanya kazi nje ya muda wa kazi pamoja na sababu nyingine ni ili apate allowances kidogo.


Nadhani hizi weekends na sikukuu au hata jioni na usiku msizichukulie poa, hashindwi kufanya jambo.
 
Back
Top Bottom