Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Guys mue na moyo mgumu wa chuma ukikosa placement kuna kanzi data na wengi wamepata.....just imagine wengine tunasubiri matokeo ya placement kwa miezi saba! Sometimes tunahisi labda matokeo yamefutwa lakini tunajipa tu moyo
Mmmh acha masikhara mkuu,, miezi Saba Ina maana ulifanya Usaili lini na ni kada gani hyo...?
 
Uzi umepooza na kila mtu kushikwa na butwaa kihusu mwenzetu Wizy kutikuja amepatwa na nini kama ni kukosa mrija hilo ni jambo la kawaida na huenda mungu amempangia sehemu njema zaidi ya ile,,,huko uliko wizy kama umefanikiwa hongera kama hakuna basi tunaamini siyo mwisho wa mapambano
@wizy popote ulipo tunakuomba urudi.

Riziki ipo, kila mmoja wetu amekadiriwa riziki yake na muumba wake na hauwezi kuondoka juu ya mgongo wa ardhi kabla haujaichakata riziki yako.

Mtihani tulioachiwa ni njia za namna ya kuichuma hiyo riziki na kila mmoja atatumia njia yeyote ile ili aweze kuchuma riziki yake.

Wengi wetu kwenye uzi tumeona njia bora ya kuiendea riziki ni kupambana na PSRS ingawa kuna njia lukuki ambazo tunaweza kupita nazo na tukafanikiwa.

Katika hizi njia kuna mabonde, miinuko, tambarare, visiki, matope, utelezi[emoji3][emoji3](sio ule lakini) ambavyo vinafanya pawe na changamoto mbalimbali tunazopaswa kuzikabili ili tuweze kupita.

Mtu unakandwa mara kadhaa, hapo umekumbana na miinuko, matope, visiki. Ili uweze kupita lazima ukae chini ubuni mbinu za kuzitumia mwishowe unapita (unafika oral)

Mwingine anapitia njia ya utelezi/mserereko(written 1 tu kawakanda, oral 1 tu kawakanda).

Tunapitishwa katika hizo njia zote na mgawa riziki huku akiwa na maana yake yeye pekee(kama maana ya mabadiliko ya status baada ya oral kutokana na programming kama anavyosemaga wizy ).

Hivyo basi tunapaswa kushukuru kwa jambo lolote lile maana kila jambo hutokea likiwa na sababu yake kwani unaweza kulalamika kuhusu kitu fulani kumbe umeepushwa na shari.

Tuwe na subira, tumtangulize Muumba/mgawa riziki.
 
Ety wadau(hv physical appearance pia Ina mchango wowote wa marks ..?
Yaana the way ulivyovaa na muonekano wako wote kwa ujumla.. Nazungumzia kwenye Oral interview

Nipeni tips hapo wakulungwa

Ndio mkuu kuna baadhi ya kazi na hasa hizi "White Collar Jobs" mwonekano wako wa nje unachangia sna, hapa na maanisha unadhifu au umaridadi.

Kuwa nadhifu ni muhimu sana na ni moja kati ya maadili ya kazi. Mnaweza kuwa mmepata alama sawa ktk usaili, hapo huwa wanaangalia kitu cha ziada ambacho unacho na wenzio hawana ( added advantages).

Kwa hyo kupitia unadhifu wako unaweza pata nafasi ya kusonga mbele.
 
Ety wadau(hv physical appearance pia Ina mchango wowote wa marks ..?
Yaana the way ulivyovaa na muonekano wako wote kwa ujumla.. Nazungumzia kwenye Oral interview

Nipeni tips hapo wakulungwa
Kuvaa kiheshima hasa kiutumishi ni muhimu sana.

Hivi ukivaa kama msanii, macheni kama yote, jinsi umetoboka toboka, chini raba kubwa, masikioni hereni si watakuona kituko!!

Kila sehemu kuna dressing code yake, PSRS nenda na dressing code ya kiutumishi, ikiwezekana tumia sample ya mavazi yaliyokwenye muongozo wa mawazi ya watumishi wa umma(kuna picha zimebandikwa kwenye ofisi mbalimbali za umma)

Akina Prok walipigilia dressing code ya kiuanasheria, walitokelezea vizuri sana
 
@wizy popote ulipo tunakuomba urudi.

Riziki ipo, kila mmoja wetu amekadiriwa riziki yake na muumba wake na hauwezi kuondoka juu ya mgongo wa ardhi kabla haujaichakata riziki yako.

Mtihani tulioachiwa ni njia za namna ya kuichuma hiyo riziki na kila mmoja atatumia njia yeyote ile ili aweze kuchuma riziki yake.

Wengi wetu kwenye uzi tumeona njia bora ya kuiendea riziki ni kupambana na PSRS ingawa kuna njia lukuki ambazo tunaweza kupita nazo na tukafanikiwa.

Katika hizi njia kuna mabonde, miinuko, tambarare, visiki, matope, utelezi[emoji3][emoji3](sio ule lakini) ambavyo vinafanya pawe na changamoto mbalimbali tunazopaswa kuzikabili ili tuweze kupita.

Mtu unakandwa mara kadhaa, hapo umekumbana na miinuko, matope, visiki. Ili uweze kupita lazima ukae chini ubuni mbinu za kuzitumia mwishowe unapita (unafika oral)

Mwingine anapitia njia ya utelezi/mserereko(written 1 tu kawakanda, oral 1 tu kawakanda).

Tunapitishwa katika hizo njia zote na mgawa riziki huku akiwa na maana yake yeye pekee(kama maana ya mabadiliko ya status baada ya oral kutokana na programming kama anavyosemaga wizy ).

Hivyo basi tunapaswa kushukuru kwa jambo lolote lile maana kila jambo hutokea likiwa na sababu yake kwani unaweza kulalamika kuhusu kitu fulani kumbe umeepushwa na shari.

Tuwe na subira, tumtangulize Muumba/mgawa riziki.
U said it All man👊
 
Kuvaa kiheshima hasa kiutumishi ni muhimu sana.

Hivi ukivaa kama msanii, macheni kama yote, jinsi umetoboka toboka, chini raba kubwa, masikioni hereni si watakuona kituko!!

Kila sehemu kuna dressing code yake, PSRS nenda na dressing code ya kiutumishi, ikiwezekana tumia sample ya mavazi yaliyokwenye muongozo wa mawazi ya watumishi wa umma(kuna picha zimebandikwa kwenye ofisi mbalimbali za umma)

Akina Prok wakipigilia dressing code ya kiuanasheria, walitokelezea vizuri sana
Kwa kujazia hiyo hasa uvae kwenye Oral
 
Vaa casual
Epuka kuvaa tofauti na watumishi wa Umma , vaaa shati , suruali kiatu Cha kamba kizuri
Chana nywele , au vaa baragashia
Ety wadau(hv physical appearance pia Ina mchango wowote wa marks ..?
Yaana the way ulivyovaa na muonekano wako wote kwa ujumla.. Nazungumzia kwenye Oral interview

Nipeni tips hapo wakulungwa
 
Back
Top Bottom