Kwanini Wajita hawaui nyoka aina ya kifutu? Bado wanaamini katika nyoka hao?

Kwanini Wajita hawaui nyoka aina ya kifutu? Bado wanaamini katika nyoka hao?

Phdum

JF-Expert Member
Joined
Apr 15, 2019
Posts
1,322
Reaction score
3,278
Kuna mila na imani nyingi saana potofu. Niliishi kwa wajita huko kijiji fulani karibu na kibara. Kuna siku nyoka mkubwa aina ya kifutu alionekana cha kushangaza badala ya watu kuanza kumshambulia walianza kukimbia kila mtu kutafuta njia yake.

Baadae wakaja na mfuko eti wanambembeleza aingie ndani ya mfuko wampeleke porini. Ikabidi niulize ndio naambiwa wanaamini huyo nyoka wakimuua ni mikosi na balaa itawaandama na sio kumua tu hata yeyote atakaye muona akiuwawa nae nuksi na mikosi itamuandama.

Lakini pia wengine wanasema huyo nyoka wanamsujudi kama sehemu ya mizimu yao. Nilibaki nacheka tu maana mimi ninachojua ukimuona nyoka ni kuwahiana tu kummaliza.

Je, huko kwenu vipi mkimwona nyoka mnapiga naye picha au mnawaita Maliasili.

images.jpeg
 
Abhajita bhejasu bha Rusori,mungwako amasango ge chimumu bhabhabhwiriye?

Yegoooooo!,siga okwamba nitegelesye amasango kuchalo kunu!
 
Niliishi kijiji kimoja kinaitwa Busambara...siku moja niliona wenyeji wamemkata chatu aliyemeza mbuzi wakamchapa tu viboko na kumweka kwenye gunia na kwenda kumtupa mtoni!!
 
Back
Top Bottom