Kwanini Wakili Tundu Lissu anaiogopa sana Mahakama?

Kwanini Wakili Tundu Lissu anaiogopa sana Mahakama?

DATAZ

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2012
Posts
3,799
Reaction score
10,196
Huyu bwana kwa taaluma yake na kwa jinsi anavyojipambanua kama mwanasheria nguli, nilitaraji niwe nimemuona katika viunga vya mahakama mara kadhaa. Sababu kubwa ni kwa kujua na Lissu anajua sana, kuwa kwa mujibu wa Katiba yetu, mahakama ndio mhimili uliopewa mamlaka ya kusimamia na kutoa haki katika Nchi.

Lissu anadai kupitia katika matukio mazito, ambayo kisheria, yalipaswa kuwa yamefika Mahakamani ili sio tu kulinda na kutetea Haki yake Lakini pia kuweka msingi kwa haki za wengine.

1) Lissu alinusurika kuuawa na kupigwa risasi nyingi tu. Na alisema waliotaka kumuua anawafahamu. Aliwahi kukaririwa akisema "I have survived to tell a tale". Kilichotokea Hadi Leo ni kurusha tu tuhuma na lawama hadharani kwenye mikutano na vikao bila hatua yeyote ya kisheria

2) Lissu kaja na tuhuma za kuhongwa mamilioni na mtoto wa Rais bila shaka Ili ahujumu chama chake. Kuhongwa/Rushwa ni Kosa kubwa kisheria. Hapa napo hajaweza kuchukua hatua zozote za kisheria zaidi kumwaga tuhuma hizo hadharani Kila siku.

3) Lissu amedai na anadai kutishwa na amepokea Taarifa za kuaminika za kuuawa. The same story, hakuna hatua anazoonekana kuchukua zaidi ya maneno anayotamka hadharani.

Najiuliza ni hofu gani huwa anaipata Lissu ku initiate hatua za kisheria dhidi ya madhila haya anayodai kumpata ambayo pia ni kinyume kabisa na Sheria za Nchi? Kama mambo mazito kama haya yanashindikana kwa Lissu, vipi kwa Mtanzania wa kawaida?
 
Hahahaha kuna mahakama bongolendi kiongozi, au mfululizo wa threads tu ntoke vipi za simba? Wakili mkongwe huyu anaogopa mahakama? Majaji karibu wote majunior wake, na keshatetea watu maelfu bure mahakamani wakati unakua, hujajua kusoma na kuandika
 
Hivi kwa nini Majaji wengi huku Mikoani wanakufa sana vifo vya ajabu, tena vikiambatana na utata mwingi?.

Ni kwamba hawatendi haki na kujikuta KARMA ikiwaadhibu?, au ikoje wakuu hali hiyo?.

cc
Pascal Mayalla
 
Lissu ni mdau mzuri wa Mahakamani, hata huo unguli wa sheria uliupata baada ya kuudhihirisha mahakamani.

Isivyo bahati, baada ya kumiminiwa risasi 30+ akapona kimiujiza, inaonesha huenda ameacha/emepunguza kwenda Mahakamani.

Alipoteza leseni ya uwakili na keshairudisha tayari, wakati anamuita jiwe dikteta uchwara alikua mahakama ya kisutu hapo
 
  • Thanks
Reactions: K11
Yaani aogope Mahakama?

Lisu anaongea kwa mitego ili ninyi wahusika mjae then awaumbue ..

Unaweza kumfunga Lisu kwa mabavu tu Ila sio kwa Sheria..

Ni mjanja anajua ni kipi nikiongea kina madhara kisheria na kipi nikiongea hakina madhara kisheria ..
 
Suala la kisiasa shughulika nalo kisiasa. Garbage in, garbage out.
 
Huyu bwana kwa taaluma yake na kwa jinsi anavyojipambanua kama mwanasheria nguli, nilitaraji niwe nimemuona katika viunga vya mahakama mara kadhaa. Sababu kubwa ni kwa kujua na Lissu anajua sana, kuwa kwa mujibu wa Katiba yetu, mahakama ndio mhimili uliopewa mamlaka ya kusimamia na kutoa haki katika Nchi.

Lissu anadai kupitia katika matukio mazito, ambayo kisheria, yalipaswa kuwa yamefika Mahakamani ili sio tu kulinda na kutetea Haki yake Lakini pia kuweka msingi kwa haki za wengine.

1) Lissu alinusurika kuuawa na kupigwa risasi nyingi tu. Na alisema waliotaka kumuua anawafahamu. Aliwahi kukaririwa akisema "I have survived to tell a tale". Kilichotokea Hadi Leo ni kurusha tu tuhuma na lawama hadharani kwenye mikutano na vikao bila hatua yeyote ya kisheria

2) Lissu kaja na tuhuma za kuhongwa mamilioni na mtoto wa Rais bila shaka Ili ahujumu chama chake. Kuhongwa/Rushwa ni Kosa kubwa kisheria. Hapa napo hajaweza kuchukua hatua zozote za kisheria zaidi kumwaga tuhuma hizo hadharani Kila siku.

3) Lissu amedai na anadai kutishwa na amepokea Taarifa za kuaminika za kuuawa. The same story, hakuna hatua anazoonekana kuchukua zaidi ya maneno anayotamka hadharani.

Najiuliza ni hofu gani huwa anaipata Lissu ku initiate hatua za kisheria dhidi ya madhila haya anayodai kumpata ambayo pia ni kinyume kabisa na Sheria za Nchi? Kama mambo mazito kama haya yanashindikana kwa Lissu, vipi kwa Mtanzania wa kawaida?
hana ushahidi kabisa 🐒
 
Back
Top Bottom