Kwanini waliozaliwa katika familia maskini wana nafasi kubwa na wao kuwa maskini kuliko waliozaliwa katika familia tajiri?

Kwanini waliozaliwa katika familia maskini wana nafasi kubwa na wao kuwa maskini kuliko waliozaliwa katika familia tajiri?

SubTopic

Member
Joined
Sep 15, 2021
Posts
95
Reaction score
175
Ni swali fikirishi kidogo ukiangalia wengi wanaotokea familia maskini wengi huishia kuwa masikini ni wachache sana ambao hutoboa kimaisha. Au ndo tuseme umasikini mtu anaweza kuurithi?

Mfano: mawazo ya kimasikini kutoka kwa baba yanaweza kuhamia kwa mtoto kama baba hakuwa na vitega uchumi hawezi kukushauri kuhusu kuwa na vitega uchumi, kama alikuwa muoga katika kuwekeza itaweza kukufanya na wewe kuwa muoga.

Kwa kifupi falsafa ya baba ni rahisi sana kuhamia kwa mtoto mpaka ujipambanue sana ndo unaweza kuondokana nazo.
Tunatokaje katika hili? hebu tupeane mawazo zaidi

karibuni kwa mawazo wakuu
 
Kuzaliwa masikini ni bahati mbaya ila kufa masikini ni uzembe wako.

Wengine tumetoka familia za kimasikini sana japo sijawa tajiri ila sipo vibaya na bado nina nguvu za kupambana.

Japo hawa tunaowazaa sijui hata wanaelewa kitu,

Pambaneni vijana
 
1. Maskini hana urithi wa mali

2. Maskini hana wazazi wenye connections kwasababu watu wengi wanaojuana huwa katika level moja ya uchumi, mara nyingi matajiri circle zao ni za matajiri na wazazi wake wakiwa maskini, basi circle zao zimejaa maskini wenzao

Suluhisho.

1. Atengeneze connections zake kwa jasho lake yeye mwenyewe

2. apambane kwa bidii awe juu sana kwenye kitu anachofanya, kama ni shuleni basi afaulu mpaka vyuo vinambakiza awe lecturer, kama ni biashara inabidi ajibane kweli kweli ili mtaji uongezeke, n.k

3. atumie kipaji chake, hapa wenye vipaji wengi (sio wote) wanatokeaga maisha magumu kuanzia kina pele, maradona, messi, ronaldonho, michael jackson, n.k. tumia ulichojaaliwa kikunufaishe.

Vitu ambavyo havina msaada:

Tamaa - hapa atageuka kuwa kibaka anaweza kuishia kuchomwa moto, anaweza kuwa malaya akaishia kufubazwa kwa magonjwa na kujishusha utu.

Kulalamika kuzaliwa maskini - kuzaliwa maskini si uamuzi wako lakini kufa maskini kwa kiasi kikubwa ni uamuzi wako, kama nguvu unazo, akili unazo, n.k pambana mpaka kieleweke, hapa nikianza kuweka listi ya matajiri waliokuwa maskini tutakesha maana hata Mengi (r.i.p) alizaliwa familia ya kimaskini.

kuendekeza kauli za kimaskini - tumevikuta na tutaviacha, kulikuwa na matajiri flani ila leo wako wapi, cha muhimu kupumua, n.k achana na taka taka hizi aisee, umevukuta na utaviacha lakini hakikisha na wewe vikupitie hata kwa mbali, ukiendekeza hizi kauli za kijinga utateseka sana.

Kutafuta connection kwa kujishusha utu wako - tafuta connections bila kuondoa utu wako, kuwa chawa inapobidi kwa mbali lakini usiwe kupe ambae hata unapoona kabisa watu wanakuvumilia uwepo wako wewe unang'ang'ania, yani unalazimisha sana ukaribu lakini watu unaona kabisa wanakuvumilia tu kinafki wanatamani uondoke na hawana muda na wewe, mfano mzuri hapa nahisi pana Steve Nyerere, yani huyu hata kwa mwaka huu kuna semina ilikuwa ya viongozi wa kike pale Dodoma, jamaa alienda aisee, Pia huko kwa viongozi wengine analazimisha sana connection anabaki kituko tu maana washamkariri yupo kwa maslahi yake tu, matokeo yake hata michongo ama teuzi hapati kwa tabia hizi.

Wivu na chuki kwa wenye navyo - Wivu hautakusaidia chochote zaidi ya kukuumiza tu na mwishowe kuwa mshirikina tu na ushirikina haunaga maendeleo, wivu wako na chuki kwa waliofanikiwa utakuumiza sana hii dunia, kutwa nzima utawaombea mabaya wenzako na utazidi kuumia wanavyozidi kutoboa.

kuwekeza muda mwingi kwenye anasa - Sio tatizo ukiwa na ratiba maalum lakini ni tatizo ukizidisha,,,,iwe ni pombe, ngono, sigara, bangi, n.k hivi vitu vitakufanya usahau kabisa malengo yako huku afya yako ikizidi kuzorota.
 
ukiuliza swali katikakati ya halaiki ya watu ya kwamba wangapi wanapenda kuwa masikini hakuna atakayenyoosha mkono. Ni dhahiri kuwa watu hawapendi kuwa masikini ila namna ya kuchukua hatua ndo inakuwa ngumu. Maana asilimia kubwa ya watu wengi sio watu wa kujiuliza natokaje hapa,
 
1. Maskini hana urithi wa mali

2. Maskini hana wazazi wenye connections kwasababu watu wengi wanaojuana huwa katika level moja ya uchumi, mara nyingi matajiri circle zao ni za matajiri na maskini circle zao za maskoni wenzao

Suluhisho.

1. Atengeneze connectiona zake kwa jasho lake yeye mwenyewe

2. apambane kwa bidii awe juu sana kwenye kitu anachifanya, kama ni shuleni basi afaulu mpaka vyuo vinambakiza awe lecturer, kama ni biashara inabidi ajibane kweli kweli ili mtaji uongezeke, n.k

3. atumie kipaji chake, hapa wenye vipaji wengi (sio wote) wanatokeaga maisha magumu kuanzia kina pele, maradona, messi, ronaldonho, michael jackson, n.k. tumua ulichojaaliwa kikunufaishe.
Asante kwa mchango wako mkuu. Mawazo yako yanamsaidia mtu mahali fulani muda huu
 
Nafikiri pia masikini anakosa mpango wa muda mrefu (long term plan) atatafuta chakula cha leo tu hajali kuhusu kesho. Ni sawa na kupanda mti ili upate matunda na ufaidike nayo. Siyo kitu rahisi kuusubiri mti mpaka ukue na kupata matunda. Lakini mtu akiweza hapo ana nafasi ya kutoboa. Nimetoa huo kama mfano
 
ukiuliza swali katikakati ya halaiki ya watu ya kwamba wangapi wanapenda kuwa masikini hakuna atakayenyoosha mkono. Ni dhahiri kuwa watu hawapendi kuwa masikini ila namna ya kuchukua hatua ndo inakuwa ngumu. Maana asilimia kubwa ya watu wengi sio watu wa kujiuliza natokaje hapa,
Muda mwingine watu tumekuwa wazembe wakutafakari vizur ni hatua gani sahihi uchukue zinazoweza kukufikisha kule unapotaka
 
Muda mwingine watu tumekuwa wazembe wakutafakari vizur ni hatua gani sahihi uchukue zinazoweza kukufikisha kule unapotaka
hakika ndugu! .yaani tunatumia muda mwingi kulalamika kuliko kuchukua hatua
 
ukiuliza swali katikakati ya halaiki ya watu ya kwamba wangapi wanapenda kuwa masikini hakuna atakayenyoosha mkono. Ni dhahiri kuwa watu hawapendi kuwa masikini ila namna ya kuchukua hatua ndo inakuwa ngumu. Maana asilimia kubwa ya watu wengi sio watu wa kujiuliza natokaje hapa,
Umasikini ni upeo Mdogo kuhusu mazingira yanayokuzunguka na kushindwa kuziona fursa.
 
umezaliwa uswahilini, shule ukasoma uswahilini, ukaendelea kukaa uswahilini, Vijiwe vyako ni vilabuni, vijiwe vya bao na solo au drafti, mpira unaangalizia vibanda umiza, utakuwa tajiri saa ngapi na hao matajiri utawaona wapi?

Sasa mwenzio kkazaliwa uzunguni, kakulia uzunguni, kasoma IST, huko kakutana na
"wenye dunia" sasa kwanini asije kuwa tajiri?

Mazingira yana nafasi kubwa sana ya kumfanya mtu kuwa tajiri au kuendelea kuwa masikini.
 
Ogopa kilichoandikwa hadi ndani ya Biblia.
Mathayo 13:12
[12]Kwa maana ye yote mwenye kitu atapewa, naye atazidishiwa tele; lakini ye yote asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyang’anywa.
For whosoever hath, to him shall be given, and he shall have more abundance: but whosoever hath not, from him shall be taken away even that he hath.
 
Back
Top Bottom