Kwanini wanafunzi wasianze kidato cha kwanza na michepuo ya sayansi (Physics, Chemistry) au arts kwa kuzingatia matokeo ya Darasa la Saba?

Kama mambo ndio haya basi bado tuna safari ndefu sana mkuu...
 
Hizi multiple choice usidharau sana.....ukipata mtunzi mzuri wa mtihani, hutoboi! Kwani yale maswali ya aptitude tests na hata IQ tests mengi si huwa ni multiple choice tu?
 
Wale niliowakuta na A flat na wengine kupiga 100% kwa masomo 2 au 3 niliwaburuza.
Kigezo Cha matokeo ya la 7 hakina mashiko miaka hii . Kuna vijana walikuja form one na A flat but form four wakatoka na four.
Doooh basi kazi ipo mkuu
 
Ni uamuzi tu wa watunga sera...

Kuna uwezekano hata yakaanza fundishwa shule za msingi
 
Wapunguze miaka ya kusoma imekuwa mingi mno na haina maana yoyote zaidi ya kupoteza muda inakera sana unapoteza muda 18yrs unasoma hakuna ajira wala uwezo wa kujitegemea kwenye soko la ajira African we are not seriously
 
Hayo masomo sana ni lazima mwanafunzi wa kidato cha nne ayafanyie mtihani ndio maana nikasema ni ya msingi
Labda kwa sasa hivi. Miaka hiyo wale waliosoma sekondari za ufundi masomo kama History, Geography na Biology walikuwa hawasomi/haafanyii mtihani form four. Nafikiri hata kwa wale wa michepuo ya biashara kuna baadhi ya hayo mosomo unayoita ya "msingi" hayakuwa ya msingi kwao.

But nakiri kuwa huenda nimepitwa na wakati sana.....na labda mambo yameshabadirika kwa sasa.
 
Sikubaliani na hoja yako kwa sababu mimi binafsi shule ya msingi sikufanya vizuri masomo ya sayansi hata hisabati ila nilipopelekwa sekondari utoto uliponiisha nikapenda sayansi na hisabati na kufanya vizuri sayansi kuliko art kwenye matokeo ya O level. Hivyo nawaza mfumo wa sasa uendelee tu. Maana utafiti unaonyesha akili za watoto wa kiume zinaanza kutulia wakiwa kwenye advanced stage baada ya balehe ambayo ni huko O level. Watoto wa kike akili yao iko stable except kwa changamoto ndogondogo kama MP nk zingatia wao wanavunja ungo mapema wakiwa primary school wa kiume wanachelewa...kwa hiyo sekondari akili ya kijana wa kiume ndo inaanza kutulia....mimi wazo nalopendekeza miaka ya shule ya msingi ipunguzwe hadi miaka 6 au iongezwe hadi miaka 8 ya sekondari o level iwe 3 .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…