Kwanini wanataka kuzuia Rais Samia Suluhu asiende kinyume na Hayati Magufuli?

Kwanini wanataka kuzuia Rais Samia Suluhu asiende kinyume na Hayati Magufuli?

Kwani tatizo nini? Mbona mnaonekana hamjaridhika samia kushika nchi? Mlitakaje labda ? Aapishwe majaliwa?
Samia Suluhu Hassan ndio Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania
Samia Suluhu Hassan ndio mweyekiti wa chama kubwa CCM
Samia Suluhu Hassan ndio mama wa kwanza wa taifa

Kazi iendelee
 
Mimi naamini Rais yuko kipindi cha mpito anajipa mda,hata Magu aliwateua Wana JK lakini alipojipa mda hawakuchukua round akawatema wote ko hata hao hawana miaka 2 alishasema wataachwa njiani
 
Kwa maoni yangu ni kuwa Mama samia Amerithi serikali ambayo yeye alikuwa sehemu yake na ilikuwa na malengo kulingana na ilani ya uchaguzi iliyowaweka madarakani pale, kwa hiyo swala ni ukamilishaji wa ilani ile.

Ni maoni yangu tu, siyo kuwa kwa vile karithi serikali na yeye ndiyo bosi basi ilani yao haina maana tena ila yeye ataleta ya kwa kwake tofauti; sidhani kama kweli mambo yanatakiwa yawe hivyo. Wenzetu husema elections have consequences, ambazo yeye atatakiwa azisimamie siyo kuwa azifute.

Mkuu uko sahihi lakini sidhani Mama anataka kufuta matokeo ya ilani. Nadhani anataka kutumia njia nyingine na ni njia hizo ndio wengi bungeni hawataki zibadilishwe.

Kufunga shughuli za siasa ilikuwa na faida kwa CCM kwa sababu marehemu alitumia nafasi yake kama mwenyekiti kufanya siasa!! CCM haitaki uhuru wa habari, inataka Polisi ifanye kazi kwa mabavu badala ya sheria. CCM inataka kushika hatamu na huenda mama anadhani taasisi ya uRais ndio ishike hatamu.

Matokeo hayana shida, shida ziko kwenye njia. Na ni bahati mbaya njia za marehemu zinaanikwa na Mama kama hazikuwa sahihi na zikome. Anataka haki, jambo gumu sana kufanywa na CCM.
 
Ni ukweli usiofichika kuwa kuna mkakati wa ndani ya Bunge na baadhi ya Mawaziri wakiongozwa na PM mwenyewe kum pre empty Rais Mama Samia ili ajikute anafanya kazi bila kwenda kinyume na mtangulizi wake JPM.

Mkakati huo unaoendeshwa kimahesabu sina hakika kama Rais ameshaushtukia au kwa vile timu ya wasaidizi wake ni ileile anaweza kuwa anafunikwa na blanketi na halioni hilo?

Je, ni kwa nini mbinu hizo chafu zinafanywa? Je, mama haoni kuwa kuendelea na wasaidizi wasio kubaliana kifikra kuwa yeye ni Rais kwa sasa itakwamisha mipango yake?
Nadhani shida kubwa kwake itakuwa ni katiba,hivi mkiangalia mle bungeni kuna watu wengine zaidi hao wanaomzunguka?
 
Kamanda hivi mnafikiri kwa upuuzi mnaweza kuifitinisha serikali? Muda unakuja, hamtapata mnayoyata mrudie kazi yenu ya ramli na matusi
Hakuna Ramli za matusi labda kama neno tusi lina maana tofauti.yaani mnadharau mpaka ripoti ya CAG kulinda kivuli cha huo mzoga wenu? Mnamshangilia mpumbavu kibajaji kuua hoja za wasomi wa nchi hii???
Ukiwa ccm unakuwa mpumbavu tu
 
Ni ukweli usiofichika kuwa kuna mkakati wa ndani ya Bunge na baadhi ya Mawaziri wakiongozwa na PM mwenyewe kum pre empty Rais Mama Samia ili ajikute anafanya kazi bila kwenda kinyume na mtangulizi wake JPM.

Mkakati huo unaoendeshwa kimahesabu sina hakika kama Rais ameshaushtukia au kwa vile timu ya wasaidizi wake ni ileile anaweza kuwa anafunikwa na blanketi na halioni hilo?

Je, ni kwa nini mbinu hizo chafu zinafanywa? Je, mama haoni kuwa kuendelea na wasaidizi wasio kubaliana kifikra kuwa yeye ni Rais kwa sasa itakwamisha mipango yake?
Kwa sababu 1. Mambo aliyotekeleza magufuli chini ya usaidizi wake ni mazuri sana kwa watanzania. 2. Yeye anafuata ilani ya CCM hivyo ni muendelezo tu nothing else. Asituletee mapaya hatuyataki. Mapya ataanzisha akigombea na kushinda 2025 alete maono yake na azitafute pesa za maono yake!
 
Kwa mtu yeyote aliyefanya kazi kama makamu atakubaliana nami kuwa wakubwa hukera na pia hufurahisha.
Ikitokea unashika madaraka kuna utakayoyatupilia mbali na utakayoyaendeleza.
Tusilazimishe hiyo ndiyo hali haalisi
 
Nanaamini kila mmoja anahitaji kufanya kitakachomjenga kiutendaji na kihistoria.

Kwa uelewa au matendo asilazimishwe mtu kuyaridhi kwani sio kila cha kuridhi ni hekima kama sio hivyo hakuna haja ya kuufuata mfumo wa mwenye mamuzi yake.

Rais hatekelezi majukumu yake kwa sababu ya kutaka kujijengea historia nzuri, bali anatekeleza majukumu yake kwa mujibu wa kanuni za kisheria na kikatiba zilizopo wakati huu. Historia itamfuata yenyewe baadaye. In fact viongozi ambao hujiaribu kufurahisha historia, huwa wanakuja kuumbuliwa sana na historia hiyo kwani historia huwa haiandikwi na watu unawafurahisha sasa hivi bali huandikwa kwa ujumla wake kuangaliajinsi mtu alivyotekeleza majukumu yake kwa mujibu wa kanuni zilizokuwapo.
 
"Kodi ya dhuluma, hapana"! Hii ni moja kati ya departure nzuri sana. Naamini na ule uozo na unyang'anyi wa DPP kwenye kesi za kubumba za uhujumu uchumi na money laundering hawezi kuendelea nao.

Ilani ya uchaguzi ya ccm haina shida. Shida ilikuwa ni namna inavyotekelezwa.

Unaweza kupambana na ufisadi bila kuonea watu. Unaweza kukusanya kodi bila kuonea watu. Kuwapa watu uhuru wa maoni, habari na kufanya siasa ni haki za kikatiba.....kunyima haki Hizi haikuwahi kuwa ilani ya ccm.

Sasa mama aki depart kwenye hayo mambo ya hovyo hovyo ya JPM kuna shida gani?

JPM alikuwa ana abuse sana madaraka yake makubwa kama Rais, hakuwa na staha pia unazotegemea Rais wa nchi awe nazo (e.g. Rais anawezaje kumwambia mwananchi wake kuwa " abaki na mavi yake nyumbani" ....tena hadharani! Alikuwa anatia aibu tu)
Magufuli hakustahili kuwa Rais wa nchi hii, sema tu mifumo yetu ya mibovu ndiyo ilimfikisha pale.
 
Ni kazi sana kujua jinsi mambo yanavyofanyika bongo
 
Na mandumi la kuwili yamejaa 'mjengoni'!
Mama yetu Raisi Samia (Iron lady) kuwa makini sana na hawa wanafiki wakubwa!
 
Back
Top Bottom