Kwanini wanawake Waislamu hawaruhusiwi kwenda makaburini kuzika wapendwa wao?

Kwanini wanawake Waislamu hawaruhusiwi kwenda makaburini kuzika wapendwa wao?

Waislamu Wameanza lini kuaga maiti?
Mwili kupelekwa nyumbani kwake kuswaliwa na kutolewa kwenda malaloni ndio maana halisi ya kuagwa na watu wake ikiwemo ndugu marafiki na majirani na si kwamba atawekwa na kufunuliwa la hasha.

Kwahiyo wanawake wataishia nyumbani na ndio inatafsiriwa kua wameaga na kuzika.baada ya hapo ni shughuli ya wanaume ili kuondoa mchanganyano wa jinsia kwakua huenda ukaleta athari hasi na zikasababisha watu kupata dhambi.

Ndio maana ata kwenye nyumba zetu za ibada wanawake hatuchangamani nao kabisa , kwahiyo kuondoa usumbufu huo mafundisho yetu yanasema ni bora wabakie nyumbani
 
Ni kwanini Wakristo mnalazimisha Waislam wafanya mfanyavyo? Waislam na Qur An Yao imewaambia kwamba '...hawatokuwa radhi nanyi mayahudi na manaswara(Wakristo) mpaka mfuate Mila zao....'

....'Ninyi mna Dini yenu na wao Wana Dini yao'.

Kila mtu atekeleze maelekezo ya Dini yake
Unachoandika na nilichokujibu ni vitu tofauti. Sijasema sitaki mfanye mnayotaka kufanya. Mm sijawaambia mpande daladala pamoja na wanawake. Ni nyie wenye ndio mmesema hamtaki kuchangama na wanawake ikiwa kila siku mnachangamana nao. Ndio nawauliza mnapokua kwenye daladala, au huko maofisini au huko masokoni huo uislamu mnauweka pembeni?
 
Huyo Sheikh alimaindi baada ya majirani wa Dida kugoma kwenda kuagia makaburini wakisema kwamba kwa nini hajapelekwa nyumbani kwake alikokuwa anaishi akaagwe kwa mara ya mwisho?

Walichofanya hao majirani, na wao wakaenda huko huko makaburini, wanaume kwa wanawake.

Sasa kama wao waliweka ratiba ya kuagia iwe makaburini walitegemea mashoga zake wasiende makaburini kwenda kuaga?

Badala ya kubwata na wanawake walioenda makaburini kuaga, wangedili na walioandaa ratiba ya mazishi.

View attachment 3118369

View attachment 3118370
hawa majirani sjawaelewa kabisa hoja yao ipi?
 
Saudi Arabia ni nchi ya kiislamu, inafuata sharia.

Israel mara nyingi hapa nimesoma na nasoma kuwa hawaupendi ukristo, wanaupiga marufuku ukristo, hairuhusiwi kumtaja kristo. Pia mara nyingi tumekubaliana Israel wakristo ni wachache kuliko hata waislamu na ipo hivyo.
Saudi Arabia siyo islamic state.
 
Kwani wakienda kuna hatari/physical consequences or to put it in a religious perspective, moral consequences gani zitatokea?

Uislam uko very conservative, extremely conservative! Unawaona wanawake as OBJECTS of men!

(nitakao wakwaza naomba radhi for my observation)
Dini ya Uislam imekamilika! Haifanyiwi review kwa matakwa ya nafsi za binadamu!
Ukianza kuhoji hivyo utajiuliza maswali yote, kwanini tuoe, kwanini tuswali rakaa nee mbili zina shida gani. Na maswali mengine ya kipuuzi!

Zipo dini zinaruhusu review za imani zao, nenda hizo usilazimishe usilamu uefuate matakwa ya nafsi zenu!
 
1.Saudia Arabia ni nchi yenye waislamu wengi kwa maana ya wakazi sio nchi ya kiislamu kwa maana ya kuongozwa na Quran na Sunan, ile ni nchi ya kifalme tu ilio amua kufanya uislamu kuwa dini rasmi na kiarabu kuwa lugha rasmi hakuna la ziada pale , ndio maana wanarithishana tu babu, baba na watoto ile nchi

2. Waisrael wanasoma kitabu BIBLIA asa agano lake, lakini kila mwaka serikali ina ruhusu paredi la mashoga, huwezi kusema hii nchi inaongozwa na Biblia ni nchi ya kipagani hiyo hata kama wayahudi ndio wengi
Wewe ndio mtu pekee ambae nimewahi kumsikia akisema Saudi Arabia sio nchi ya kiislamu.

Israel nimekujibu kuwa hata hao wakristo ni population ndogo kuliko hata waislamu walioko huko. Haiwezi kuwa nchi ya kikristo
 
Wamevaa vibandiko vichwani lakini hata dini hawaijui halafu wanajinasibu mitaani kama wanazuoni.
Uislam haukatazi mwanamke kwenda kuzika, bali imeshauriea tu. Swala hilo la mwanamke kwenda au kutikwenda kuzika limepelekea hata wanazuoni kugawanyika.
Sababu zilizopelekea ishauriwe wanawake kutokwenda kuzika ni;

1. Wanawake wapo too emotional na hawawezi kujizuia, hivyo wakati wa kushuhudia safari ya mwishi ya mpendwa wao hupelekea wengi kushindwa kujizuia na kuanza kulia kwa sauti na hivyo kuingilia na kuvuruga ibada.

2. Kwa maumbile yao, na kama ilivyozoeleka uwepo wa wanawake makaburini husababisha fitna (majaribu/ushawishi), hivyo kupelekea msoma mawaiza/dua pamoja na wengine badala ya kujikita kwenye kumuomba marehemu kwenye safari yake ya mwisho, badala yake fitna ya wanawake inaweza ikapelekea wahame katika dua na mawaiza na kuanza kufikiria mengine.

Hivyo, ieleweke kwamba swala la wanawake kutotakiwa kwenda kuzika siyoamri, yaani siyo katazo bali ni ushauri tu.
kwani mkuu yale si mavazi tu anavaa yeyote?
 
Wewe ndio mtu pekee ambae nimewahi kumsikia akisema Saudi Arabia sio nchi ya kiislamu.

Israel nimekujibu kuwa hata hao wakristo ni population ndogo kuliko hata waislamu walioko huko. Haiwezi kuwa nchi ya kikristo
Huo ndio ukweli ile sio nchi ya kiislamu, ila ni nchi yenye waislamu wakaazi wengi,
Kuhusu Israel sijataja ukristo mimi nimetaja Biblia ya wayahudi, inakataza ushoga lakini kila mwaka ile serikali ya Netanyahu inaruhusu paredi la mashoga, huwezi kusema hii nchi ni ya kibiblia ni nchi ya watu wameamua tu iende watakavyo sawa na Saudi Arabia
 
Wamevaa vibandiko vichwani lakini hata dini hawaijui halafu wanajinasibu mitaani kama wanazuoni.
Uislam haukatazi mwanamke kwenda kuzika, bali imeshauriea tu. Swala hilo la mwanamke kwenda au kutikwenda kuzika limepelekea hata wanazuoni kugawanyika.
Sababu zilizopelekea ishauriwe wanawake kutokwenda kuzika ni;

1. Wanawake wapo too emotional na hawawezi kujizuia, hivyo wakati wa kushuhudia safari ya mwishi ya mpendwa wao hupelekea wengi kushindwa kujizuia na kuanza kulia kwa sauti na hivyo kuingilia na kuvuruga ibada.

2. Kwa maumbile yao, na kama ilivyozoeleka uwepo wa wanawake makaburini husababisha fitna (majaribu/ushawishi), hivyo kupelekea msoma mawaiza/dua pamoja na wengine badala ya kujikita kwenye kumuomba marehemu kwenye safari yake ya mwisho, badala yake fitna ya wanawake inaweza ikapelekea wahame katika dua na mawaiza na kuanza kufikiria mengine.

Hivyo, ieleweke kwamba swala la wanawake kutotakiwa kwenda kuzika siyoamri, yaani siyo katazo bali ni ushauri tu.
so maana yake kama ni ushauri tu majirani hawana kosa. mstari wako wa kwanza ni vema ukauondoa
 
sasa magari yana husika vip na Uislamu?muwe mnaelewa kuwa Saudi Arabia sio utawala wa kiislamu ule, ni tawala za watu tu walizo jiamulia
Kwa hiyo wewe Muislamu wa Buza na Makangarawe unaujua Uislamu kuliko wenye Mecca ma Madina yao?? Nyambaaaaaf
 
Saudi Arabia siyo islamic state.
Screenshot_20241008-125726_1.jpg
 
Huo ndio ukweli ile sio nchi ya kiislamu, ila ni nchi yenye waislamu wakaazi wengi,
Kuhusu Israel sijataja ukristo mimi nimetaja Biblia ya wayahudi, inakataza ushoga lakini kila mwaka ile serikali ya Netanyahu inaruhusu paredi la mashoga, huwezi kusema hii nchi ni ya kibiblia ni nchi ya watu wameamua tu iende watakavyo sawa na Saudi Arabia
Kusema Saudi Arabia sio nchi ya kiislamu ni kujitoa akili. Sifa za nchi ya kiislamu ni zipi?
Saudi Arabia inafuata sharia laws, katiba inafuata Quran na sunna. Bado unassma io nchi ya kiislamu?
Screenshot_20241008-125726_1.jpg
 
Kwa hiyo wewe Muislamu wa Buza na Makangarawe unaujua Uislamu kuliko wenye Mecca ma Madina yao?? Nyambaaaaaf
Uislamu sio Mecca na Madina ni maandiko wewe, kila mmoja yuko huru kusoma na kujifunza, kama ulikuwa ufahamu hao makafiri wengi walio msumbua Mtume walikuwa ni wakazi wa hapo hapo Saudi Arabia
 
Kusema Saudi Arabia sio nchi ya kiislamu ni kujitoa akili. Sifa za nchi ya kiislamu ni zipi?
Saudi Arabia inafuata sharia laws, katiba inafuata Quran na sunna. Bado unassma io nchi ya kiislamu?
View attachment 3118685
Utachukua muda kuelewa sana hata ISIS walijitangaza ni Dola la kiislamu kule Iraq na Syria, kusema ni moja na kufanya ni mbili, hiyo nchi ni ya kifalme hakuna uhusiano na Dola ya kiislamu
 
Wanawake katika uislam hawaruhusiwi kwenda kuzika ila wanaruhusiwa kwenda kutembelea makaburi.

Hawaruhusiwi kwenda kuzika kwasababu wengi wao huwa wanalia kupitiliza na hata wakiona maiti anafukiwa huwazidishia uchungu na mara nyingine wanaongea maneno yanayopelekea kukufuru mfano "Mungu kwanini umemchukua"

Kuzika katika uislam ni ibada na kila ibada ina utaratibu wake hivyo utaratibu wa ibada hii ya kuzika ni mwanamke kubaki nyumbani akimuombea dua maiti wake na mwanaume ni kwenda makaburini kuzika.
Heri wewe umeeleza sababu
Kuliko wengine wamekuja na matusi tu wanatukanana badala ya kujadili mada.
 
Utachukua muda kuelewa sana hata ISIS walijitangaza ni Dola la kiislamu kule Iraq na Syria, kusema ni moja na kufanya ni mbili, hiyo nchi ni ya kifalme hakuna uhusiano na Dola ya kiislamu
Nimekuuliza sifa ya nchi ya kiislamu ni zipi? Kipi kifanyike ili ujue hii nchi ni ya kiislamu na ipi sio ya kiislamu?
Saudi Arabia wanatumia sharia laws, katiba yao inafuata Quran na sunna. Lipi tena lifanyike?
 
Back
Top Bottom