Kwanini wanawake wengi wana mihemko ya Uzinzi miaka hii hata aliyeko kwenye ndoa anazini?

Kwanini wanawake wengi wana mihemko ya Uzinzi miaka hii hata aliyeko kwenye ndoa anazini?

Leo tu kuna mdau amesafiri kibiashara mke wake wa ndoa ameingiza mwanaume kwenye kitanda chake kwa ajili ya kuzini hivi hamuoni aibu???
Mnakera kwa kweli

mkuu huyo mwanaume ni wewe au? maana umejuaje yote hayo?
 
Mapi bana mie leo mzuka sina. ila mi huwa naona wanaume ndio balaa, ila si unajua mwanamke ndio mkosaji siku zote.
umekunywa nini kikakuharibia?? ye si ndio anaruhusu, akifich si tutakosa..hahahah
 
Last edited by a moderator:
Mimi nachomshauri ni akazane kula vyakula vya asili na mazoezi tutaenda sawa pia asivae boxer mbichi na zinazobana sana.Kitu kingine akiona mzigo unamuelemea uwanjani ajipe red card atafute size.Siyo kulalama.wanaume mjishughulishe haya matatizo yatakwisha
wengine kama katapila kwenye uchimbaji wa barabara ila ndio hivyo tena wenzetu
 
Jibu ni sisi wanaume tunatongoza sana nje ya mahusiano, ndoa zetu. Kuna mme wa mtu aliweka dau kabisa kwa demu wa mtu, anamwambia ntakupa 2m ukinivulia pants, sasa boyfriend pesa za mawazo, demu akakubali pesa inawekwa benki demu anaachia mchezo kwisha. Wanaume tukibadirika haya hayatakwepo
 
elezea na upande mwingine wa shilingi,vipi wanaume kwa uzinzi?
 
Maisha yamebadilika sana kwa hiki kizazi,ndoa hazimaanishi ndoa bali imekuwa ni kificho cha maovu,
watu hawajali tena viapo walivyoapa mbele za Mungu kuvuana nguo ovyo ovyo imekuwa kama fasheni,
huyu kavuana na huyu,mara yule yaani ni hatari kwa kweli.
Si bora mtembee uchi ieleweke moja?
 
wengi ni kwa hasira na kulipiza visasi kwa waume zao..unakuta mume ni mwenye mahusiano mengine nje ya ndoa yake,mwanamke anavumiliaa wee mwisho wa siku anachoka..na kutengana hataki labda anahurumia watoto wake...na hapo labda njia nyingine zote za kumtuliza mume zimeshindikana..basi wanaamua na wao kuzurura nje ya ndoa sasa..inakua ngoma droo tu
ndio njino kwa njino ee? au dawa ya moto ni moto?kunakitu kitabaki kweli?
 
Hakika siogopi kupigwa mawe kwa ukweli.. A true friend is one who doesn't make you happy with a lie but one who hurts you with the truth.nawasubirie
na ukadhani kila mtu anataka ukweli??
 
Kna dada nao washachoka kulia lia,manyanyaso na kumganda mwanaume,ukiongeza na economic independence ndo kabisaaa usinichoshe nisikuchoshe,tusichoshane
 
Sasa kulipiza siyo solutions unadhani anayeabika ni nani kati ya aliyetenda kwa kuhisiwa na huyu atakaye amua kuvua nguo zake kwa ajili ya kulipiza na kujiabisha..

Kama anayeaibika ni mwanamke wewe kama mwanaume inakuhusu nini? Piga kimya kwanza kuchapiwa ni siri ya ndani!
Isitoshe pengine shuuuli imekushinda!
 
Kwa kipindi cha mwaka mmoja nimefuatilia maada nyingi humu ndani hakika wanawake wamezidi kufanya ngono ndani ya mahusiano.
Yaani kuna matukio yanajitokeza mpaka unashindwa kuelewa kama wana moyo wa huruma au wameingiliwa na shetani gani..Mtu unaingia kwenye Ndoa kwa kusahau yote aliyoyapitia bado akiingia kwenye ndoa anaendelea kufanya uzinzi tu..Jaribu kusoma thread nyingi ndani ya MMU utaona nyingi zinaongelea kusalitiana, kufumaniana,kugongewa yaani shida tupu.
Je ni vyakula hivi ambavyo vimebadilisha mihemko ya miili yetu mpaka tunakuwa na hamu ya uzinzi hadi usoni kwetu...Tuwe wakweli humu ndani wadada wengi wanamatatizo kwenye mahusiano yapo ndio maana baadhi yao michango yao huwa ukiifikiria utadhani siyo mwanamke ..

Ebu wakati tunaelekea mwisho wa mwaka tujaribu kujiuliza nini tumemkosea mungu mpaka tunakuwa na hulka ya uzinzi kiasi hicho.
Leo tu kuna mdau amesafiri kibiashara mke wake wa ndoa ameingiza mwanaume kwenye kitanda chake kwa ajili ya kuzini hivi hamuoni aibu???
Mnakera kwa kweli

ndugu yangu sio vyakula wala nini!! zamani wanawake walikandamizwa wakaonekana hawawezi wala hawajui chochote lakini nadhani ilikuwa ni uongo tu sasa wanawake wana power ndio wanafanya the same kama wanaume wanavyofanya, so give them power they ll do the same as men. so usishangae hakuna cha vyakula wala nini, na tunapoenda ni kubaya zaidi, ila itabidi tukubali mi kijana nimekuwa nikimwambia kila siku wanawake wa siku hizi ni tofauti na kina sie, so asnione mimi ninavyioishi na babake wa kizamani akafikiri wanawake wa siku hizi wako no!! aombe Mungu sana ampe mke mwema na yeye mwenyewe ajue nafasi yake kama mwanaume. otherwise tutaona mengi sana kizazi hiki.
 
Ukweli upo mifano pia, kuna watu wamejitoa ufahamu wanakula vichwa kama vinyozi kwa ujira mdogo kupiga mizinga ikibuma hapa yule anatoa. Ni hatari, wanaume baadhi pia wanaangukia mkondo huu kwa kukomoa. Tujirekebishe tusiumize wasio na hatia.
 
Kama anayeaibika ni mwanamke wewe kama mwanaume inakuhusu nini? Piga kimya kwanza kuchapiwa ni siri ya ndani!
Isitoshe pengine shuuuli imekushinda!

Kula five Mkuu! Kuzini tuzini siye, aibu tuaibike siye, bastola washike wao! majangaaaa!!!
 
Jibu alishatoaga zahra white! Hatuna sababu ya kurudiarudia! Muulize babu Aspirin!!!
 
Bora wajitokeze wanawake wenyewe watueleze mambo yanayosababisha watoke nje ya ndoa
 
Back
Top Bottom