Kwanini Waswahili hatuwezi kwenda na muda?

Kwanini Waswahili hatuwezi kwenda na muda?

TheChoji

JF-Expert Member
Joined
Apr 14, 2009
Posts
5,771
Reaction score
17,849
Tunakubaliana kabisa, jamani eeh kesho tukutane saa tatu kamili asubuhi. Watu wote wanaitikia "Sawa, saa tatu imekaa vizuri kabisa!"

Wewe unawahi saa tatu kasoro dakika 5 unafika eneo la tukio unakuta hakuna mtu hata mmoja. Unaanza kusubiri... saa tatu kamili, saa tatu na dakika 10, saa tatu na nusu.... saa nne!

Ndio watu wanaanza kujitokeza mmoja mmoja huku ikijichekesha chekesha "Ooh unajua bana mambo mengi asubuhi..." Sasa si mngesema tukutane saa nane?

Hivi kweli Waafrika tutaweza mambo serious kama swala la muda tu linatushinda!
 
Mbongo ukiwa una miadi nae SAA 3 basi wewe mwambie saa mbili....

Usimwambie muda kamili wa kukutana nae.

Kutokufata muda ni tatizo la utamaduni.

Kufuata muda na taratibu ni utamaduni
 
Mbongo ukiwa una miadi nae SAA 3 basi wewe mwambie saa mbili....

Usimwambie muda kamili wa kukutana nae.

Kutokufata muda ni tatizo la utamaduni.

Kufuata muda na taratibu ni utamaduni
Tatizo linapokua ni swala la watu wengi, ukisema saa 2 kuna watu watafika hiyo saa 2 kweli, halafu ndio wanaanza kukaa saa nzima wakiwasubiri wengine
 
Ukimwambia mkutane saa nne atakujaa saa Tano .wabongo na muda n vtu viwili tofauti hatuheshimu muda baadhi yetu
 
Wanajifariji na msemo wa 'There Is No Hurry In Africa' !!!
 
Tunakubaliana kabisa, jamani eeh kesho tukutane saa tatu kamili asubuhi. Watu wote wanaitikia "Sawa, saa tatu imekaa vizuri kabisa!"

Wewe unawahi saa tatu kasoro dakika 5 unafika eneo la tukio unakuta hakuna mtu hata mmoja. Unaanza kusubiri... saa tatu kamili, saa tatu na dakika 10, saa tatu na nusu.... saa nne!

Ndio watu wanaanza kujitokeza mmoja mmoja huku ikijichekesha chekesha "Ooh unajua bana mambo mengi asubuhi..." Sasa si mngesema tukutane saa nane?

Hivi kweli Waafrika tutaweza mambo serious kama swala la muda tu linatushinda!
Hakuna Haraka Afrika .tulia
 
Tunakubaliana kabisa, jamani eeh kesho tukutane saa tatu kamili asubuhi. Watu wote wanaitikia "Sawa, saa tatu imekaa vizuri kabisa!"

Wewe unawahi saa tatu kasoro dakika 5 unafika eneo la tukio unakuta hakuna mtu hata mmoja. Unaanza kusubiri... saa tatu kamili, saa tatu na dakika 10, saa tatu na nusu.... saa nne!

Ndio watu wanaanza kujitokeza mmoja mmoja huku ikijichekesha chekesha "Ooh unajua bana mambo mengi asubuhi..." Sasa si mngesema tukutane saa nane?

Hivi kweli Waafrika tutaweza mambo serious kama swala la muda tu linatushinda!
Wengi hawana usafiri bongo, miundo mbinu mibovu, maeneo wanayokaa wabongo wengi ni chokoromageni hayo ni baadhi ya matatizo makubwa mengine watajazia... halafu mtoa mada acha ushamba na uzumbukuku utafikiri ulizaliwa ulaya.. kwani ulizaliwa ndani ya muda?
 
Back
Top Bottom