uwezo wa kuyachimba mnao?,technology mnayo ili myachimbe wenyewe.
unadhani mtu aje na vyote hivyo,awekeze mabilioni ya dola kisha nyie mchukue hela?,,,,

kwa hiyo wachimbe bure sio?

Ndoooooorobo we,si afadhali madini hayo tuyaache wajukuu zetu wakiwa na technologia na mitaji waje wachimbe. Madini hayaozi umenielewa eehee.
 
Habari ya leo wanajukwaa?

Leo ningependa tushirikishane kidogo au tupeane uelewa juu ya kwa nini uchumi wa Tanzania unakua lakini bado wananchi wengi wanaishi katika dimbwi la umasikini.

Kitu vitu viwili ambavyo ningependa wanajukwaa wenzangu mvielewe.

Kuna kitu kinaitwa KUKUA KWA UCHUMI, kwa tafri isyo rasmi wanaitwa ''ECONOMIC GROWTH''. Economic Growth au kukua kwa uchumi (kwa tafsiri isiyo rasmi na nitaendelea kitumia) ni ile hali ya kuongezeka kwa HUDUMA na BIDHAA zinazozalishwa nchini kwa kipindi fulani.(Hii mjumuiko wa tafsiri mbili za Charles P. Kindleberger na Simon Kuznet.

Kumbe tunaposema kukua kwa uchumi tunazungumzia ile hali ya kukua/kuongezeka kwa uzalishaji wa bidhaa na huduma katika nchi.

Hali hii hupimwa kwa takwimu, kwa mfano uchumi wa pato la ndani la Taifa kwa mwaka 2013 ni trilioni 19.8, mwaka 2014 trilioni 21.2 (kwa robo tatu za mwaka) na mwaka 2015 (robo ya kwanza) ni trilioni 21.9. Ukiangalia takwimu hizo utaona ni kweli kuwa pato la ndani linakuwa siku hadi siku.

KWANINI BADO WATANZANIA NI MASIKINI?
Katika uchumi kuna kitu kingine (ambacho ndio cha pili) kinaitwa ''Economic Development'', kukua kwa uchumi(sio pato la taifa, ingawa lenyewe ni sehemu). Hapa unazungumizia maisha ya watu, ubora wa maisha watu wanayoishi, wanapata mahitaji ya muhimu (Chakula, Mavazi, Malazi, Afya na Ulinzi), Je, binadamu huyo anaheshimika na wengine, anathaminika? Ana uhuru wa kweli juu ya kujiamulia mambo yake?(Ili mradi havunji sheria)?

Kwa hiyo kama mwanadamu ana vitu vitatu yaani

1. Anapata huduma za muhimu kama nilivyoeleza hapo juu

2. Anathaminika na kuheshimika na wengine

3. Ana uhuru wa kweli juu ya kujiamulia mambo yake. Kama haya yote yapo, ndipo tunasema MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA (Msome mwandishi Todaro).

Kwa hiyo, watanzania wanapewa takwimu za kukua kwa uchumi (Pato la Tiafa) sio maisha yao.Kukua kwa uchumi wa kweli ni kuwepo kwa nafasi za ajira, kupungua kwa umasikini na kuwepo kwa usawa.

Yaani wanaelezwa ECONOMIC GROWTH na sio ECONOMIC DEVELOPMENT.

Asanteni.
 
Watanzania pamoja na nani, wema ana rangerover, shilole ana Mercedes Benz, diamond BMW X5, masikini tumebaki wachache sana.
 
Mimi nashangaa tunanadi kuwa tuna madini ya kila aina, bahari, misitu, mbuga za wanyama na ardhi kubwa ya kilimo lakini nchi imekithiri umaskini na mabingwa wa kuombaomba kwa wazungu na wakati huohuo serikali inafukuza ombaomba mjini lkn wao kuomba kwa wazungu hakuna anayewafukuza sasa tatizo ni viongozi, wananchi au Chama tawala
 
Tatizo ni wote hapo kila mtu hawajibiki kwa nafac yake ndio maana tuko hivi ila sasa viongozi ndo vinara kwa ubinafsi na uroho wa Mali kujilimbikizia.
 
Mkuu tatizo kubwa ni viongozi waliopita ikiwemo magufuli na yeye hakwepi lawama yeye na chama chake
 
Tunawajibika ila kodi zetu hazituletei maendeleo wala kupunguza deni la taifa. Tatizo ni chama tawala hakina mikakati ya kuleta maendeleo bali kuchukua ushindi kwa gharama zozote na kufaidi rasilimali za nchi.
 
kwa sababu wengi zenu ni wapumbavu na malofa.
 
Huu mwimbo unachekesha sana.
Watunge beat tu sasa.

Kwanini Tz ni masikini,
Tuna nini nini nini nini nini

Hahaha
 
Tatizo la TANZANIA NI UPIGAJI NA KUJILIMBIKIZIA MALI. Kila mtu anawaza kupiga tu. Imefikia hatua mpaka vijana wanaosoma vyuoni wanawaza kununa BMW na NDINGA ZINGINE kwa pesa ya dili. ETHICS imeshuka kwa kiwango kikubwa mpaka aibu. Sio wazee sio vijana. Hili taifa limekuwa la ajabu ajabu tu
 
Kwanini masikini hupenda sifa na matanuzi? Naangalia bunge la UK ukumbi wao ni wa kawaida sana, hauna mbwembwe licha ya utajiri wao.Inakuwaje pale Dodoma ukumbi wa bunge mi wa kifahari as if sisi tuna uwezo mkubwa kiuchumi?
 
Kwanini masikini hupenda sifa na matanuzi? Naangalia bunge la UK ukumbi wao ni wa kawaida sana, hauna mbwembwe licha ya utajiri wao.Inakuwaje pale Dodoma ukumbi wa bunge mi wa kifahari as if sisi tuna uwezo mkubwa kiuchumi?
Nikajua nimeona mwenyewe na kuwaza mwenyewe lakin hizo ndo tabia za maskini too much spending.
 
mimi mwenyewe nimejiuliza sijapata jibu, yani inaonekana wenzetu wazungu wanatuona kama vichaa tuu sema wanashindwa kutuambia because of their economic interest in africa
 
Ni ulimbuke Mkuu. Jamii yetu ina matatizo yafuatayo. Ubinafsi, kupenda sifa ili waonekane, Kutojali, kutopendana, kutokuwa serious na maisha. Hata huyu anayejipambanua kuwa yeye ni wawanyonge, hakuna kitu hizo ni geresha tu, nakutumia ukali sana ili walio naye wamuogope ili baadaye apige deal za kufa mtu. Ubinafsi kwa jamii yetu ni tatizo sugu. Hatutaki kuishi kwa kuogopa kesho. Ukipata tumia kesho itajijua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…