Kwanini Watanzania na Tanzania ni masikini pamoja na rasilimali (resources) tulizonazo?
Tanzania si maskini. Ni Watanzania ndio maskini. Wala sio maskini bali ni mafukara. Ni ufukara uliotokana na ujinga (kukosa Elimu) na uongozi mbaya. Hayo mawili yamezaa ufisadi, na huu ufisadi ukaleta ufukara zaidi (vicious circle)

Tanzania bila Watanzania si Tanzania kwa hiyo kama Watanzania ni maskini basi Tanzania nayo ni maskini.
 
Nadhani unge rephrase kichwa cha mada na kuwa "Kwa nini Afrika ni bara maskini?"

Ila mwisho wa siku, baada ya kufanya kila aina ya diagnosis na kudhani mmejua au tumejua sababu ya nini sisi kuwa maskini, ukweli unabaki palepale kuwa sisi Miafrika ni Ndivyo Tulivyo na hiyo ndiyo sababu kuu (underlying reason) ya umaskini wetu na yote yaliyowahi kutokea Afrika pamoja na utumwa na ukoloni.

Nadhani kuna ukweli kua waafrika hawana uwezo wa kujitawala na hii inatokana na ukweli kua ktk nchi za kiafrika serikali zimeshindwa kupanga na kusimamia mipango ya maendeleo kwa watu wao, hii ikwa na maana kuwa policies walizojiwekea zimeshindwa.

Mimi naamini sababu kubwa kutokua na uwezo kiutawala ni ubinafsi wetu na kutokua na uwezo wa kudhibiti watu wetu. Sitasema natoka wapi, lakini pale kwetu kabila fulani wapo radhi Mhindi atajirike kuliko kabila langu. Pia kabila langu ni hivyo hivyo. Hiyo inaendelea mpaka kwa mtu binafsi.
 
Nadhani unge rephrase kichwa cha mada na kuwa "Kwa nini Afrika ni bara maskini?"

Ila mwisho wa siku, baada ya kufanya kila aina ya diagnosis na kudhani mmejua au tumejua sababu ya nini sisi kuwa maskini, ukweli unabaki palepale kuwa sisi Miafrika ni Ndivyo Tulivyo na hiyo ndiyo sababu kuu (underlying reason) ya umaskini wetu na yote yaliyowahi kutokea Afrika pamoja na utumwa na ukoloni.

Hapana mkuu wangu sio Afrika yote maskini, maskini sisi na walalahoi wengine ambao hawafahamu pia ni maradhi gani yamewapata. Nasema hivi kwa sababu hata Ulaya kuna mataifa masikini tena maskini zaidi yetu na wao ni wazungu kuliko wazungu wa Uingereza maana Uingereza leo hii imejaa Machina, Wahindi, Wayahudi na mataifa mengi ambayo naweza kabisa kudai kwamba Mataifa tajiri duniani ni yale yenye mchanganyiko mkubwa wa wageni.

Hili neno Utumwa na Ukoloni ndilo nataka sana kuliewa vizuri sana maanake ikiwa kweli umaskini wetu umetokana na Utumwa na ukoloni hivi dawa yake nini haswa?..kuondoa viongozi wenye fikra za Ukoloni au sisi sote tujenge fikrazipi maanake kweli hadi leo hii nchi zote za Kiafrika zinategemea akili ya mzungu ktk kila strategy inayotumika.

Nitarudi ktk mfano wa WATU na MAZINGIRA, unajua toka mkoloni tulizoea ukienda Hospital unapewa dawa, sasa tabia hiyo imeendelea hadi leo kiasi kwamba daktari anayepokea mgonjwa akataka kufanya uchunguzi kwanza kabla ya kutoa dawa kuitwa sii daktari mzuri. Tunataka ukisha fika hospital dakati awe tayari na dawa mkononi iwe sindano au dawa ya kumeza..Na wakati mwingi dawa ya kumeza haiaminiki zaidi ya sindano, meaning sisi wenyewe tayari tumekwisha jenga fikra za kupona kwa sindano zaidi ya vidonge..Je, ni fikra hizi zinazotokana na utumwa kiasi kwamba tunaendeleza fikra hizo hata ktk dunia hii ya uchunguzi kabla ya kutibu?.

Mkuu, mimi bado nipo palepale, NDIVYO TULIVYO ni somo kubwa sana ambalo linaweza kujaza vitabu volume 10 kwa urahisi kabisa, lakini pamoja na hayo yote ni lazima kuna tofauti ya maradhi ya Umaskini kama vile Zimbabwe wanakwisha kwa sababu ya gonjwa la Ukimwi na Tanzania inaongoza kwa vifo kutokana na Maleria.. yote ni maradhi lakini imani yangu inanituma kwamba dawa ya Zimbabwe kuondokana na Umaskini (ukimwi) haiwezi kuwa sawa na dawa itakayotumika Tanzania kuondokana na Umaskini wetu (Maleria)..Pia maradhi ya Tanzania yanatibika tofauti na Ukimwi wa Zimbabwe ambao hata wataalam wanapendekeza kinga.

Halafu kwa kuongezea tu, ni jinsi gani maradhi hutibiwa?... Je, inapotokea pendamic ni muhimu kuzuia maradhi kusambaa au kinachotangulia ni kuweka karantini waathirika ili maradhi hayo yasisambae.. mfano huu unahusu scandal kama za mafisadi. je, kinachotakiwa ni kuweka sheria kinga ya Ufisadi (chanjo) kwa wananchi wote au kuwasweka mafisadi wote ndani lupango (karantini) hao mafisadi waathirika.

Mkuu najaribu kutafuta jibu aloshindwa kulijibu JK.. nikiwa na maana kuwa hapa JF wapo wasomi wanaoweza kunifunulia..kwa sababu ikiwa sote hapa tuliweza kumbeza JK kwa majibu yale ina maana wapo watu hapa wanaelewa vizuri kwa nini Tanzania ni nchi maskini.. Na kama jibu la Watanzania wengi wasomi hapa JF ni sawa na lako, sasa kweli unaweza kumlaumu JK kwa kushindwa kujibu hoja ile? yaani tulitegemea JK aseme Sio Tanzania tu, Afrika nzima ni maskini kwa sababu NDIVYO TULIVYO!

Ingeleta maana kweli kwa kiongozi wa nchi kutoa majibu kwamba kushindwa kwetu kunatokana na laana a Curse, kama alivyohitimisha mkuu Son of Alaska!
 
Last edited:
ukilinganisha na wapi? ili tupate hoja yenyewe vizuri maana inawezekana tunajiona masikini kwa kulinganisha na mataifa yenye miaka 200 kwenye uhuru na ambayo hoja kama hizi zilijadiliwa miaka 155 iliyopita na wakapata majibu ndo maana leo wapo kama walivyo!!otherwise hilo swali uliza the other way round ili tujue tunaweza kuendelea baada ya muda gani??
Mkuu hatuhitaji kubishana wala kulinganisha na nchi yoyote ile.. sisi ni Maskini na ndio ukweli wenyewe hata ukitumia takwimu au mwenye macho na aone!..

Nitarudia kusema Umri na miaka mingi sii sababu ya Utajiri hata kidogo. Kupata Uhuru kwa nchi kama Marekani sii sababu hata kidogo kwani kupima umri ni sawa na kupima umri wa binadamu kupima au kutafuta mafanikio yake.. Marekani walikuwa matajiri hata kabla ya uhuru wao ukilinganisha au kutolinganisha na nchi yoyote.. Huwezi kunambia unatakiwa uwe umri fulani ndipo unaweza kutajirika, hapana hata kidogo hili sio hitimisho zuri.. Wataliani walikuwa huru lini, wareno, Romania, Greece, Haiti na kadhalika mbona wao bado maskini iweje wao wasiwe matajiri kuliko hata Marekani ikiwa tutafuata umri. South Afrika wamejitawala majuizi tu na matajiri je, utajiri wao unatokana na kutawaliwa?. Au umri wa nchi unauchukua vipi mwenzangu maanake dunia hii ina umri sawa kabisa..tunaanza wapi kuhesabu umri wa nchi!..

Binafsi naamini kabisa umri has nothing ktk kuchangia umaskini au Utajiri wa nchi au binadamu. na makuzi ya mtu au nchi hayawezi kutafsirika kama ndio maendeleo.. Unapokuwa mtoto mdogo utavaa nguo zinayokutosha kwa umri na kimo chako, hivyo tofauti ya ukubwa wa nguo isiwe sababu hata kidogo ya kutafsiori utajiri wa mtu kama vile majengo na kadhalika..

Pili, siwezi kusema kwa udogo wetu wa umri ndio maana sisi maskini, ukifananisha na mtoto ambaye hajafikia umri wa kujitegemea.. Hii itahalalisha ukweli kwamba Tanzania ni taifa changa hivyo tulihitaji bado malezi ya mama yaani ukoloni... Maadam sisi wenyewe tumechagua kuingia ktk maisha ya kujitegemea hatuwezi kabisa kusingizi umri kwani kijana wa miaka 18 anaweza kabisa kuwa successful kuliko mzee wa miaka 50..umri haujengi sababu ya umaskini mkuu wangu.
 
Last edited:
Hili neno Utumwa na Ukoloni ndilo nataka sana kuliewa vizuri sana maanake ikiwa kweli umaskini wetu umetokana na Utumwa na ukoloni hivi dawa yake nini haswa?..kuondoa viongozi wenye fikra za Ukoloni au sisi sote tujenge fikrazipi maanake kweli hadi leo hii nchi zote za Kiafrika zinategemea akili ya mzungu ktk kila strategy inayotumika.

Mkandara...
Hili la kuhususha utumwa na ukoloni na umaskini wa sisi Waafrika ni kisingizio kisicho na kichwa wala miguu. Yako mataifa yaliyoathirika sana na ukoloni lakini yameweza kupiga hatua. Na... beside that... mtu unaweza kujiuliza ilikuwaje mtu atoke mbali aje akamate mababu zetu nyumbani kwao? Huoni Mwafrika alishashikuwa dhaifu kabla ya hata huo utumwa wenyewe?
 
Mkandara...
Hili la kuhususha utumwa na ukoloni na umaskini wa sisi Waafrika ni kisingizio kisicho na kichwa wala miguu. Yako mataifa yaliyoathirika sana na ukoloni lakini yameweza kupiga hatua. Na... beside that... mtu unaweza kujiuliza ilikuwaje mtu atoke mbali aje akamate mababu zetu nyumbani kwao? Huoni Mwafrika alishashikuwa dhaifu kabla ya hata huo utumwa wenyewe?
nakusikia mkuu wangu lakini bado sijapata jibu...
Mwalimu Augustine Moshji kagusia vitu lakini ila hakunipa kwa kirefu vitu hivyo vinaweza vipi kubadilisha matokeo maanake kama ni maradhi tunaona wasomi wetu wakitoa watu miguu huku wanaumwa kichwa!..idadi ya vifo nchini inazidi kuwa kubwa kuliko wakati wowote ule hali wasomi tunao wengi zaidi.. Ni elimu gani inayotakiwa haswa. na viongozi wa aina gani wanatakiwa maanake kama wazungu (wasomi) bila shaka walitutawala kwa muda mrefu kuliko hata sisi wenyewe na uhuru wetu na wakatuacha maskini...
 
Nadhani jibu lipo kwenye nukuu hii:

Unfortunately”, she concludes, “we are not associated with excellence. I will never forget that during training overseas a former CEO I served under said ‘putting the words ‘Tanzanian’ and ‘Excellence’ together would be an oxymoron.’ Even when convinced that you are indeed a Tanzanian they attribute your confidence and drive to foreign exposure. I find this insulting.”

Source: Have you ever wished you were not Tanzanian? < http://udadisi.blogspot.com/2009/09/have-you-ever-wished-you-were-not.html >
 
Nadhani jibu lipo kwenye nukuu hii:

Unfortunately", she concludes, "we are not associated with excellence. I will never forget that during training overseas a former CEO I served under said &#8216;putting the words &#8216;Tanzanian' and &#8216;Excellence' together would be an oxymoron.' Even when convinced that you are indeed a Tanzanian they attribute your confidence and drive to foreign exposure. I find this insulting."

Source: Have you ever wished you were not Tanzanian? < http://udadisi.blogspot.com/2009/09/have-you-ever-wished-you-were-not.html >
Mkuu nadhani hili ndio swali langu kubwa..
Tofauti na maelezo hayo hapo juu sidhani kama kuna ulazima kwetu ku prove anything to anyone..kwa maana ya maelezo yako kuwa, sii lazima tu prove our excellence to anyone.
We are Tanzanian and poor, damn poor and we can't prove otherwise...Na kama nimekuelewa vizuri inaonyesha somo hili ni an insult kiana au sio?..lakini turudi nyuma sisi kweli sii maskini na umaskini wetu una associate na Watanzania wote!..iweje kuwepo na excellence ktk failures based on individual perfomance.

Hata hivyo tofauti na mwandishi huyo hapo juu, mimi sina matatizo na uwezo wa Mtanzania hata kidogo au sisi kutojiamini maadam tunaelekea kufanikiwa..tatizo ni pale tunapotaka kuonyesha kwamba sisi sio maskini yaani tunaukataa umaskini wetu kwa lugha isemayo - Tanzania wapo maskini lakini sio mimi!....kwa hiyo usinidharau au kuni associate na umaskini wa Tanzania.
 
Mkuu nadhani hili ndio swali langu kubwa..
Tofauti na maelezo hayo hapo juu sidhani kama kuna ulazima kwetu ku prove anything to anyone..kwa maana ya maelezo yako kuwa, sii lazima tu prove our excellence to anyone.
We are Tanzanian and poor, damn poor and we can't prove otherwise...Na kama nimekuelewa vizuri inaonyesha somo hili ni an insult kiana au sio?..lakini turudi nyuma sisi kweli sii maskini na umaskini wetu una associate na Watanzania wote!..iweje kuwepo na excellence ktk failures based on individual perfomance.

Hata hivyo tofauti na mwandishi huyo hapo juu, mimi sina matatizo na uwezo wa Mtanzania hata kidogo au sisi kutojiamini maadam tunaelekea kufanikiwa..tatizo ni pale tunapotaka kuonyesha kwamba sisi sio maskini yaani tunaukataa umaskini wetu kwa lugha isemayo - Tanzania wapo maskini lakini sio mimi!....kwa hiyo usinidharau au kuni associate na umaskini wa Tanzania.

Tanzania tuna 'collective economic poverty'. Hii inatokana na 'collective mental poverty'. Na kama makala hiyo niliyoposti inavyoonesha, hili ni zao la 'our collective imbecillization'!

e.g. Mzee wa Vijisenti ni tajiri individually ila as a part of the collective yeye ni maskini - economically and mentally regardless of his Harvard Degree and Jersey Money!
 
Tanzania tuna 'collective economic poverty'. Hii inatokana na 'collective mental poverty'. Na kama makala hiyo niliyoposti inavyoonesha, hili ni zao la 'our collective imbecillization'!

e.g. Mzee wa Vijisenti ni tajiri individually ila as a part of the collective yeye ni maskini - economically and mentally regardless of his Harvard Degree and Jersey Money!

Na Afrika tuna collective nini? Maana Afrika nzima kimaendeleo iko similar sana
 
Na Afrika tuna collective nini? Maana Afrika nzima kimaendeleo iko similar sana

What is so similar between Tanzania and Botswana in the South? Or Tanzania and Libya in the North? Or even Tanzania and Mauritius in the East? Or Tanzania and Cape Verde in the West?

Tanzania 'collective imbecillization' is of its own kind - ask Ortello & Barrick!
 
Tanzania tuna 'collective economic poverty'. Hii inatokana na 'collective mental poverty'. Na kama makala hiyo niliyoposti inavyoonesha, hili ni zao la 'our collective imbecillization'!

e.g. Mzee wa Vijisenti ni tajiri individually ila as a part of the collective yeye ni maskini - economically and mentally regardless of his Harvard Degree and Jersey Money!

Unazungumza kawa Tanzania iliwahi kuwa tajiri vile.
 
Unazungumza kawa Tanzania iliwahi kuwa tajiri vile.
"Tazama ramani utaona nchi nzuri; yenye mito na mabonde mengi ya nafaka nasema kwa kinywa halafu kwa kufikiri..." - Wimbo wa Enzi za Utajiri wa Ujamaa
 
What is so similar between Tanzania and Botswana in the South?

Both are third world countries!!

Or Tanzania and Libya in the North?

Last I checked Libya was not an industrialized country. It's a third world country.

Or even Tanzania and Mauritius in the East? Or Tanzania and Cape Verde in the West?

Tanzania kuna nyumba za udongo zilizoezekwa mapaa ya nyasi na huko Mauritius na Cape Verde pia wanazo nyumba za udongo zenye mapaa ya nyasi. Nimetembea karibu Uingereza nzima, nusu nzima ya Ujerumani, Uholanzi, Ubelgiji, na pia ninaishi Marekani, kamwe hata siku moja sijawahi kuona nyumba ya udongo au watu wakienda kuteka maji. Tanzania, Mauritius, na Cape Verde vitu na mambo hayo ni commonplace!!!
 
Tanzania kuna nyumba za udongo zilizoezekwa mapaa ya nyasi na huko Mauritius na Cape Verde pia wanazo nyumba za udongo zenye mapaa ya nyasi. Nimetembea karibu Uingereza nzima, nusu nzima ya Ujerumani, Uholanzi, Ubelgiji, na pia ninaishi Marekani, kamwe hata siku moja sijawahi kuona nyumba ya udongo au watu wakienda kuteka maji. Tanzania, Mauritius, na Cape Verde vitu na mambo hayo ni commonplace!!!

Ningekuamini kama ningekuwa sijafika kule kusini mwa Miami karibu na 'Haiti Ndogo na Mashariki mwa Ujerumani'!
 
Unazungumza kawa Tanzania iliwahi kuwa tajiri vile.
Mkuu Zakumi Tanzania is very rich, it has never been poor. Perhaps, its people. Kuna propaganda kuwa Tanzania ni nchi masikini ili masikini (watawala wa Tanzania na mabwana/wake?? zao wa Ulaya na marekani) waweze kupora vizuri utajiri na kuwa matajiri ili mwisho wa siku Tanzania iwe masikini kweli. Na ndo safari imeanza kwa kuachiwa mashimo na sumu za kuchimbia madini.

Mkuu hebu fikiria tukiahamishwa hapa wakaletwa Wachina au Wamalay kutatokea nini? Almasi kule, dhahabu hapa, uranium bwerere, maji usiseme, milima na mabonde ndio hayo ngedere kibao Serengeti jamani roho za kimasikini na uvivu wa kufikiri wa viongozi wa Tanzania jumlisha na ujinga wa Watanzania ndio tatizo. Hebu tuache ujinga kwanza
 
Hebu fikiria mlalahoi mmoja amebuni mradi wa icecream (malai,barafu). Mawazo yake ni siku moja atapata mtaji wa kuanzisha biashara kubwa kupitia mradi wake huu wa icecream, cha kushangaza anaacha kibubu cha kuhifadhia fedha bila uangalizi wowote. Watoto wanaporudi toka shule wanajichotea tu kilichopatikana na kwenda kutumia, mwisho wa siku anajikuta amebakiwa na kidogo tu. Baada ya muda mrefu watu wanamuuliza vipi, mbona miaka inapita huonekani kuendelea?. Biashara ni ile ile tena katika hali ya uduni uleule, naye pia anashangaa kwa nini haendelei!.

Inashangaza kusikia viongozi wetu wanashangaa kwa nini hatuendelei wakati ulinzi wa kibubu chetu uko mashakani, wapo wachache wenye uwezo wa kuchota watakavyo. Mbali na mambo mengine yaliyosemwa juu ya sababu ya kwa nini hatuendelei hii nayo ni sababu moja. Hivi vidogo tunavyovipata vilihitajika kutunzwa kwa uangalifu, kutumiwa kwa uangalifu. Leo hii tunawaona watunzaji wetu wa kibubu wakipelekwa mahakamani kwa makundi, ishara tosha kuwa kibubu hakipo salama. Tujwe kwanza kukitunza na kutumia kwa vipaumbele vinavyostahili ndipo nasi tutaanza kuona treni yetu ikianza safari ya maendeleo.
 
Back
Top Bottom