Kwanini Watanzania wengi hufukuza ama kupiga wanyama bila sababu?

Kwanini Watanzania wengi hufukuza ama kupiga wanyama bila sababu?

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Hebu chukulia mfano yanayoendelea Ukraine, mtu unamkuta anaenda kutafuta hifadhi pamoja na mnyama wake, leo hii sitashangaa hapa kwetu mtu akihamia hata mtaa wa nne basi atamtelekeza mbwa wake.

kuwatesa wanyama ni kumtemea mate usoni Mwenyezi Mungu alieumba viumbe vyote,

kuna hizi tabia mbaya sana zimezoeleka na watanzania wengi kwa wanyama 👇👇

-unakuta tu mtaani mbwa anajipitia zake, mtu anaanza kumrushia mawe.

-nyumbani kwako unafuga paka, ukimualika mgeni anaanza kumfukuza sshh tokaa!! aende wapi sasa wakati hapo ni kwao ?

-Mtu kavimbiwa nyama, zile zilizobaki ambazo hata hajazila anaenda kutupa badala ya kumpa hata mbwa au paka wanaeishi nae

-kuku yupo bize anatafuta chakula, mara mtu anaanza kumkimbiza tu bila sababu.

-Mbuzi ameletwa kwajili ya nyama ya sherehe, usiku umefika anaachwa ukutani, yani mtu hata hajali kama kuna baridi, mvua, mbuzi angalau apumzike vizuri siku yake ya mwisho, n.k.

-usiombe kukutana na mtu anatumia ng'ombe kulima, yani hizo stiki huyo ng'ombe anazokula na matusi juu ni balaa.

-Dume limempanda jike, mtu anaanza kuwarusha mawe.

-mbuzi analia meee meee kwavile ndivyo alivyoumbwa, mtu anachukia anaenda kumpiga.

-Punda anabebeshwa mizigo mizito yani hata kutembea inakuwa shida lakini mtu wala hajali.

-Mbwa kila usiku anakulinda wewe, familia yako na mali ila kibanda chake hakijasafishwa mwaka mzima kimejaa viroboto, chakula chake ni makombo kila siku, yani mtu hajiongezi hata kumpa nyama mara moja kama shukrani ya ulinzi anaompa.


Hivi hawa wanyama wanakosa lipi?
 
unakuta tu mtaani mbwa anapita mtu anaanza kumrushia mawe?

unakuta umemualika mgeni nyumbani kwako unafuga paka, utasikia sshh tokaa!!

wanyama wanakosa lipi?
Ni tabia mbaya mno....
Ni kukosa kulelewa vyema utotoni....

Ni roho za kishetani na kutomtambua Mwenyezi Mungu vilivyo.....

Ni kutoipenda dunia na ULIMWENGU.......

Ni kutohofu yasiyoonekana.....

Wanyama ni viumbe ambao kutowaheshimu huleta laana katika koo zetu na ndio maana UMASIKINI umetamalaki katika kaya nyingi za watanzania......

#YetzerHatov
#DO NOT DO HARM

#SIEMPRE JMT🙏
 
Asante umenena mkuu yan mtu namualika nyumbani anamfukuza paka sebuleni hajui pale paka nae ni mwenyeji wake!
wanakera sana, paka katulia kibarazani, lakini mgeni akipita hapo kibarazani anamfukuza, hapo hajui kwamba huyo paka ni kama mwana familia na ana bajet yake maalum ya chakula, matibabu, n.k
 
Ni tabia mbaya sana, Wanyama ni viumbe ambao kutowaheshimu huleta laana maana ni vimbe walioumbwa na Mwenyezi Mungu, viumbe hivi kuvifanyia ubaya ni kumdhihaki Mwenyezi Mungu.

unakuta tu mtaani mbwa anapita mtu anaanza kumrushia mawe.

nyumbani kwako unafuga paka, ukimualika mgeni anaanza kumfukuza sshh tokaa!!

kuku anatafuta chakula kwenye jua kali, mara mtu anaanza kumfukuza tu bila sababu.

mbuzi analia meee meee kwavile ndivyo alivyoumbwa, mtu anachukia anaenda kumpiga


wanyama wanakosa lipi?
Nahisi watu wenye tabia hizo za kupiga wanyama ni watu wenye chuki na wachoyo
 
Binafsi napenda viumbe hai,nikimkuta nge porini ambapo hakuna watu nimuue ili iweje?ninafuga mbwa na nawapenda sana,mbwa wangu akizaa huwa simpatii mtu watoto hovyo,nikikuhisi utawatesa jua umewakosa sikupi hata kama utumie lugha gani .
Napenda sana mbwa, hawa viumbe wana mapenzi ya dhati kiukweli, ni wavumilivu sana, wapo tayari kufa ili waukokoe.
 
Back
Top Bottom