Kwanini Watanzania wengi hufukuza ama kupiga wanyama bila sababu?

Kwanini Watanzania wengi hufukuza ama kupiga wanyama bila sababu?

Ni tabia mbaya mno....
Ni kukosa kulelewa vyema utotoni....

Ni roho za kishetani na kutomtambua Mwenyezi Mungu vilivyo.....

Ni kutoipenda dunia na ULIMWENGU.......

Ni kutohofu yasiyoonekana.....

Wanyama ni viumbe ambao kutowaheshimu huleta laana katika koo zetu na ndio maana UMASIKINI umetamalaki katika kaya nyingi za watanzania......

#YetzerHatov
#DO NOT DO HARM

#SIEMPRE JMT[emoji120]
Yani mimi kupiga mbwa koko aliyeko Road, ambaye anayemfuga anashindwa mjali kwa msosi qnakuja kuwinda kuku wangu inaleta laana katika ukoo wangu.
Na niipate kwa kweli na mwenye mijibwa yake tutagawqna hiyo laana wallah
 
Ni tabia mbaya mno....
Ni kukosa kulelewa vyema utotoni....

Ni roho za kishetani na kutomtambua Mwenyezi Mungu vilivyo.....

Ni kutoipenda dunia na ULIMWENGU.......

Ni kutohofu yasiyoonekana.....

Wanyama ni viumbe ambao kutowaheshimu huleta laana katika koo zetu na ndio maana UMASIKINI umetamalaki katika kaya nyingi za watanzania......

#YetzerHatov
#DO NOT DO HARM

#SIEMPRE JMT🙏
Unasemaje roho za kishetani na kutomtambua Mungu!?

Hujaenda nyumba ya mlokole anayemiliki maji ya Bulldozer, Hadi mende, mjusi huwa anamwagiwa maji, na kupigiwa kelele shindwaaaaah!
 
Ni tabia mbaya sana, Wanyama ni viumbe ambao kutowaheshimu huleta laana maana ni vimbe walioumbwa na Mwenyezi Mungu, viumbe hivi kuvifanyia ubaya ni kumdhihaki Mwenyezi Mungu.

unakuta tu mtaani mbwa anapita mtu anaanza kumrushia mawe.

nyumbani kwako unafuga paka, ukimualika mgeni anaanza kumfukuza sshh tokaa!!

kuku anatafuta chakula kwenye jua kali, mara mtu anaanza kumfukuza tu bila sababu.

mbuzi analia meee meee kwavile ndivyo alivyoumbwa, mtu anachukia anaenda kumpiga

Mbwa anakulindia maisha yako, nyumba na mali zako ila mwaka mzima unashindwa kujiongeza hata kumpa msosi wa maana kidogo kama shukrani, huu ni uungwana kweli?


wanyama wanakosa lipi?
Bado wana akili za babaric. Unaweza ona mtoto anafukuza paka wakati huyo paka hana time na yeye yuko bize tu kujitafutia panya na vijusi
 
Back
Top Bottom