Kwanini watu wa kamera wanaruhusiwa kuhujumu ziara ya Rais Samia?

Kwanini watu wa kamera wanaruhusiwa kuhujumu ziara ya Rais Samia?

11 Agosti 2022
Lupembe, Njombe
Tanzania [emoji1241]

Mh. Rais Samia Hassan awapiga kijembe waandishi wa habari


Watu ni wengi lakini mitandao inasema vingine, hivyo waandishi wa habari wapewa changamoto kuonesha ukweli ya kinachojiri katika safari yake ndefu ya kikazi kukagua maendeleo nyanda za juu kusini mikoa ya Mbeya, Njombe na Iringa
Source : mwanahalisi TV
Mbona ameeleweka au mnataka maneno tu?
 
Kama ilivyo suala la sensa, mtu una njaa utasubiri hadi uhesabiwe huku ukiulizwa maswali karibu 100
 
Namsubiri masuod kipanya na kibonzo chake juu ya huu ujumbe wa maushungi.
 
Rais Mh. Samia Suluhu Hassan ameonyesha wazi kutoridhika na utendaji kazi wa wapiga picha waliokuwa kwenye msafara wake kwa kushindwa kupiga picha nzuri zinazoonyesha umati wa watu wanaofika kumpokea. Rais Samia akiwa Njombe amelazimika kuwaagiza wapiga picha kupanda juu ya magari ili waweze kuchukua picha za umati wa watu na kuzifikisha kwenye umma ili kuondoa uzushi unaosambazwa kwenye mitandao kwamba mikutano yake haina watu wanaokwenda kumpokea zaidi ya maafisa wa serikali tu.

"Watu wa kamera pandeni juu ya gari, chukueni huu umati wa watu. Labda hawawaoni ndio maana wanaandika, na kila mkifika kila kituo chukueni umati wa watu" amesema Rais Samia. Sote tunajiuliza, iweje hao wapiga picha washindwe kutekeleza majukumu yao hadi kufikia hatua ya mkuu wa nchi kuwalalamikia kwamba wanashindwa ku cover mikutano yake vizuri. Je tukisema wapiga picha hao wanaendesha hujuma nzito dhidi ya ziara za Rais ili aonekane kwenye umma hapokelewi na watu wa kutosha tutakuwa tumekosea?

Mnaofahamu zaidi tuambizane.​
Na hili nalo mkalitizame kwa ukaribu
 
Jiwe alipanga kikosi kweli
kweli,hata Msigwa ni Jiwe
alimuweka na Wana undugu
wa kuoleana..
Ikulu na kila sehemu kulikuwa
timu Jiwe na bado wako wengi
Sana..
Kuwa na watu wengi ni sahihi
kwa sababu alikaa miaka 5 so
hata wewe lazima uweke timu
yako..
SSH hawezi pangua wote at par
ila atawang'oa taratibu.
Mimi nilidhani Jiwe alikuwa na watu wenye kumuogopa tu.
 
Yeye kaona anahujumiwa ili hali sisi tunapomuuliza maswali mustakabali wa kero zetu anatuuelekeza tukawaambie wa chini yake, kwani sisi hatujawaona hao wa chini yake? Kwaiyo kaona lake halijawekwa sawa ndio anaropoka.Vip kuhusu matatizo yetu? Tunapomueleza afu anayatupa kapuni ww kwa ubongo wako ni sawa?Mbona Magufuli alikua anayatatua hapo kwa papo kama linahusiana na mahakama anampa mtu wa mahakama aliangalie kwa haki.
Ukiwa na nchi ambayo matatizo yanatatuliwa na rais kwa mfumo wa hapo kwa papo, una tatizo kubwa kuliko rais wako.

Una tatizo la kukosa mfumo.

Na ndiyo maana huyo Magufuli mnayemsifia kwa kutatua matatizo yeye mwenyewe hapo kwa papo kama jambo hilo ni zuri, wengine tuliona jambo hilo ni baya.

Kwa sababu hakutengeneza mifumo endelevu inayoweza kudumu hata yeye akifa, alijilimbikizia madaraka.

Tatizo, watu wetu wengi wenye akili fupi walioshindwa kuona mbali waliona rais kutatua matatizo kwa style ya hapo kwa papo bila kuimarisha mifumo ni kitu kizuri.
 
Rais Mh. Samia Suluhu Hassan ameonyesha wazi kutoridhika na utendaji kazi wa wapiga picha waliokuwa kwenye msafara wake kwa kushindwa kupiga picha nzuri zinazoonyesha umati wa watu wanaofika kumpokea. Rais Samia akiwa Njombe amelazimika kuwaagiza wapiga picha kupanda juu ya magari ili waweze kuchukua picha za umati wa watu na kuzifikisha kwenye umma ili kuondoa uzushi unaosambazwa kwenye mitandao kwamba mikutano yake haina watu wanaokwenda kumpokea zaidi ya maafisa wa serikali tu.

"Watu wa kamera pandeni juu ya gari, chukueni huu umati wa watu. Labda hawawaoni ndio maana wanaandika, na kila mkifika kila kituo chukueni umati wa watu" amesema Rais Samia. Sote tunajiuliza, iweje hao wapiga picha washindwe kutekeleza majukumu yao hadi kufikia hatua ya mkuu wa nchi kuwalalamikia kwamba wanashindwa ku cover mikutano yake vizuri. Je tukisema wapiga picha hao wanaendesha hujuma nzito dhidi ya ziara za Rais ili aonekane kwenye umma hapokelewi na watu wa kutosha tutakuwa tumekosea?

Mnaofahamu zaidi tuambizane.​
Mama yetu anapenda sana promo za mitandaoni
 
Hujuma za waziwazi hizi, wako ambao wanaumia kweli juu ya urais wa Mh. Samia. Alipaswa kubadilisha timu yote ya mwendazake mara moja, ndio wanaohujumu. Kwani hamfahamu katika ziara za namna hii hapo baadae hupunguza ugumu wa kampeni maana mama anakwenda kila chochoro nyanda za juu kusini huku akifungua miradi mingi kweli tena mizito, lakini maredioni hatuoni zile taarifa zilizotufikia wakati huu kama ilivyokuwepo wakati ule.
Kiukweli Mh, anafanya kazi kubwa sana, changamoto kubwa ni hali ya uchumi mtaani, watu wako busy kutafuta chochote cha kuweka kinywani.
 
Rais George Bush wa Marekani aliambiwa na waanndishi wa habari kwamba kiwango cha kukubalika kwake, yani, "approval rating", kiko chini sana, akaulizwa kama hilo linamtatiza na analifanyia kazi vipi.

Rais akajibu kwamba yeye huwa hajishughulishi kuangalia approval rating, kwani ana kazi nyingi sana za muhimu za kufuatilia, na watu wanaomkubali watamkubali kwa kazi yake tu, na wasiomkubali, hata akijaribu kuwapendeza inawezekana ana pishana nao kifalsafa pakubwa sana.

Rais alionesha kwamba, hasumbuliwi na maneno madogo madogo yanayohusiana na muonekano wake, kuliko mambo ya msingi ya utendaji kazi wake.

Hili ni jambo la msingi. Kila dakika anayotumia rais kujikita kwenye kuuza sura, ni dakika ambayo haitumii kuangalia mambo ya msingi.

Inawezekana wapiga picha hawafanyi kazi yao vizuri, hilo si jambo ambalo rais anatakiwa kulipa headlines katika mazungumzo ya kitaifa. Hilo ni jambo la kuongea vikao vya ndani kifupi tu.

Kwa kujikita kuendekeza mazungumzo hayo, Rais Samia amejionesha anajali sana mambo ya muonekano kuliko mambo ya msingi.

Na ndiyo maana hata mambo ya maendeleo yanakuw magumu, kwa sababu Rais anapenda picha za kuonesha maendeleo ku;liko maendeleo yenyewe.
Bush unamchukuliaje mkuu
 
Bush unamchukuliaje mkuu
Katika lipi mkuu?

Watu wana pande nyingi sana ambazo zinakinzana.

Rais George W. Bush alikuwa rais mkubwa wa Africa, na alisaidia sana harakati za kutokomeza Malaria Tanzania.

Kwa hilo namuheshimu sana.

Ila kuna mambo ya kijinga kama kuiingiza Marekani kwenye vita Iraq, kwa ushahidi wa uongo wa WMD, naona alisababisha vita isiyo na sababu na kupelekea watu wengi - Wamarekani na wasio Wamarekani- kufariki.
 
Kama Raisi ana mandate! Alikua sawa kwa mtazamo wake
Hata kwa aliyo na mandate nayo, kuna calculus inatakiwa kuangalia.

Nini cha kufanya, nini cha kutofanya.

Hata cha kufanya, kipi cha kufanya wazi, kipi cha kufanya nyuma ya pazia na wasaidizi wake.

Rais kugombana sana na wapigapicha wake waziwazi anaweza kuonekana kama Kim Kardashian.
 
Hata kwa aliyo na mandate nayo, kuna calculus inatakiwa kuangalia.

Nini cha kufanya, nini cha kutofanya.

Hata cha kufanya, kipi cha kufanya wazi, kipi cha kufanya nyuma ya pazia na wasaidizi wake.

Rais kugombana sana na wapigapicha wake waziwazi anaweza kuonekana kama Kim Kardashian.
Anatumia ule wadhifa alionao bila kujua Kuna vitu anawakisea na kuwakwaza sana raia wake! Huyu mama 2025 akigombea tena atatumia pesa / nguvu nyingi sana!!
 
Anatumia ule wadhifa alionao bila kujua Kuna vitu anawakisea na kuwakwaza sana raia wake! Huyu mama 2025 akigombea tena atatumia pesa / nguvu nyingi sana!!
Tatizo si huyu rais, tatizo ni uongozi mzima wa Tanzania.

Huyu unaona mapungufu yake kwa kuwa yuko juu anamulikwa sana tu, ukimtoa na kumuweka mwingine naye utaona mapungufu yake hivyo hivyo.

Kikwete na Magufuli nao walikuwa hivyo hivyo.

Sasa utamtoa huyu umuweke nani ambaye atakuwa tofauti?
 
Rais Mh. Samia Suluhu Hassan ameonyesha wazi kutoridhika na utendaji kazi wa wapiga picha waliokuwa kwenye msafara wake kwa kushindwa kupiga picha nzuri zinazoonyesha umati wa watu wanaofika kumpokea. Rais Samia akiwa Njombe amelazimika kuwaagiza wapiga picha kupanda juu ya magari ili waweze kuchukua picha za umati wa watu na kuzifikisha kwenye umma ili kuondoa uzushi unaosambazwa kwenye mitandao kwamba mikutano yake haina watu wanaokwenda kumpokea zaidi ya maafisa wa serikali tu.

"Watu wa kamera pandeni juu ya gari, chukueni huu umati wa watu. Labda hawawaoni ndio maana wanaandika, na kila mkifika kila kituo chukueni umati wa watu" amesema Rais Samia. Sote tunajiuliza, iweje hao wapiga picha washindwe kutekeleza majukumu yao hadi kufikia hatua ya mkuu wa nchi kuwalalamikia kwamba wanashindwa ku cover mikutano yake vizuri. Je tukisema wapiga picha hao wanaendesha hujuma nzito dhidi ya ziara za Rais ili aonekane kwenye umma hapokelewi na watu wa kutosha tutakuwa tumekosea?

Mnaofahamu zaidi tuambizane.​
Ikiwezekana kila anapoenda aongozane na nguzo au miti ile mirefu akifika kwa mkutano aisindike,wapiga picha wapande wachukue picha umati wa watu..
 
Back
Top Bottom