Kwanini watu wa kamera wanaruhusiwa kuhujumu ziara ya Rais Samia?

Kwanini watu wa kamera wanaruhusiwa kuhujumu ziara ya Rais Samia?

saidoo25

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2022
Posts
624
Reaction score
1,456
Rais Mh. Samia Suluhu Hassan ameonyesha wazi kutoridhika na utendaji kazi wa wapiga picha waliokuwa kwenye msafara wake kwa kushindwa kupiga picha nzuri zinazoonyesha umati wa watu wanaofika kumpokea. Rais Samia akiwa Njombe amelazimika kuwaagiza wapiga picha kupanda juu ya magari ili waweze kuchukua picha za umati wa watu na kuzifikisha kwenye umma ili kuondoa uzushi unaosambazwa kwenye mitandao kwamba mikutano yake haina watu wanaokwenda kumpokea zaidi ya maafisa wa serikali tu.

"Watu wa kamera pandeni juu ya gari, chukueni huu umati wa watu. Labda hawawaoni ndio maana wanaandika, na kila mkifika kila kituo chukueni umati wa watu" amesema Rais Samia. Sote tunajiuliza, iweje hao wapiga picha washindwe kutekeleza majukumu yao hadi kufikia hatua ya mkuu wa nchi kuwalalamikia kwamba wanashindwa ku cover mikutano yake vizuri. Je tukisema wapiga picha hao wanaendesha hujuma nzito dhidi ya ziara za Rais ili aonekane kwenye umma hapokelewi na watu wa kutosha tutakuwa tumekosea?

Mnaofahamu zaidi tuambizane.​
 
Kulikuwa hakuna haja ya kuwaita wapande juu ya magari ili kupata picha.

Umati unaonekana tu hata ukiwa chini.

Watu wana njaa, maisha yamepanda mno, ashughulikie hilo,
Wapande juu ya magari huku njaa zinawauma na hawajui familia zao itakuwaje huko majumbani.Miguu inatetemeka tu.Utalamba mkono wenye vumbi?
 
Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan ameonyesha wazi kutoridhika na utendaji kazi wapiga picha walioko kwenye msafara wake kwa kushinda kupiga picha nzuri zinazoonyesha umati wa watu wanaofika kumpokea.

Rais Samia akiwa Njombe amelazimika kuwaagiza wapiga picha kupanda juu ya magari ili waweze kuchukua picha za umati wa watu na kuzifikisha kwenye umma ili kuondoa uzushi unaosambazwa kwenye mitandao kwamba mikutano yake haina watu wanaokwenda kumpokea zaidi ya maafisa wa Serikali tu.

"Watu wa kamera pandeni juu ya gari chukueni huu umati wa watu labda hawawaoni ndio maana wanaandika na kila mkifika kila kituo chukueni umati wa watu" amesema Rais Samia.

Sote tunajiuliza iweje hao wapiga picha washindwe kutekeleza majukumu yao hadi kufikia hatua ya Mkuu wa nchi kuwalalamikia kwamba wanashindwa ku Cover mikutano yake vizuri.

Je tukisema wapiga picha hao wanaendesha hujuma nzito dhidi ya ziara za Rais ili aonekane kwenye umma hapokelewi na watu wa kutosha au tutakuwa tumekosea?

Mnaofahamu zaidi tuambizane.
Tuandike comments za kujenga maana JUKWAA hili viongozi wanasoma sana!!!!!!!!

Mwambie awafukuze Mwigulu na Makamba ni chanzo Cha Yeye kususiwa na wananchi.
 
Kwani hawajui kazi yao? Hawana wakaguzi? Hoja haina hoja
 
Rais ni taasisi si mtu
Hili swala ni la Elimu ya kawaida kabisa ya uraia
Hata pascal akiwa Rais tutaoka kwenda kupokea taasisi ya urais na sio pascal huyo mayala
 
Hujuma za waziwazi hizi, wako ambao wanaumia kweli juu ya urais wa Mh. Samia. Alipaswa kubadilisha timu yote ya mwendazake mara moja, ndio wanaohujumu. Kwani hamfahamu katika ziara za namna hii hapo baadae hupunguza ugumu wa kampeni maana mama anakwenda kila chochoro nyanda za juu kusini huku akifungua miradi mingi kweli tena mizito, lakini maredioni hatuoni zile taarifa zilizotufikia wakati huu kama ilivyokuwepo wakati ule.
 
Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan ameonyesha wazi kutoridhika na utendaji kazi wapiga picha walioko kwenye msafara wake kwa kushinda kupiga picha nzuri zinazoonyesha umati wa watu wanaofika kumpokea.

Rais Samia akiwa Njombe amelazimika kuwaagiza wapiga picha kupanda juu ya magari ili waweze kuchukua picha za umati wa watu na kuzifikisha kwenye umma ili kuondoa uzushi unaosambazwa kwenye mitandao kwamba mikutano yake haina watu wanaokwenda kumpokea zaidi ya maafisa wa Serikali tu.

"Watu wa kamera pandeni juu ya gari chukueni huu umati wa watu labda hawawaoni ndio maana wanaandika na kila mkifika kila kituo chukueni umati wa watu" amesema Rais Samia.

Sote tunajiuliza iweje hao wapiga picha washindwe kutekeleza majukumu yao hadi kufikia hatua ya Mkuu wa nchi kuwalalamikia kwamba wanashindwa ku Cover mikutano yake vizuri.

Je tukisema wapiga picha hao wanaendesha hujuma nzito dhidi ya ziara za Rais ili aonekane kwenye umma hapokelewi na watu wa kutosha au tutakuwa tumekosea?

Mnaofahamu zaidi tuambizane.
Rais akiitwa muuza sura atakataa?

Fanya kazi, itaonekana tu.

Ukubwa gunia la chawa. Lawama haziishi.

Yani rais kumtoa kwenye reli ni rahisi hivi?
 
Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan ameonyesha wazi kutoridhika na utendaji kazi wapiga picha walioko kwenye msafara wake kwa kushinda kupiga picha nzuri zinazoonyesha umati wa watu wanaofika kumpokea.

Rais Samia akiwa Njombe amelazimika kuwaagiza wapiga picha kupanda juu ya magari ili waweze kuchukua picha za umati wa watu na kuzifikisha kwenye umma ili kuondoa uzushi unaosambazwa kwenye mitandao kwamba mikutano yake haina watu wanaokwenda kumpokea zaidi ya maafisa wa Serikali tu.

"Watu wa kamera pandeni juu ya gari chukueni huu umati wa watu labda hawawaoni ndio maana wanaandika na kila mkifika kila kituo chukueni umati wa watu" amesema Rais Samia.

Sote tunajiuliza iweje hao wapiga picha washindwe kutekeleza majukumu yao hadi kufikia hatua ya Mkuu wa nchi kuwalalamikia kwamba wanashindwa ku Cover mikutano yake vizuri.

Je tukisema wapiga picha hao wanaendesha hujuma nzito dhidi ya ziara za Rais ili aonekane kwenye umma hapokelewi na watu wa kutosha au tutakuwa tumekosea?

Mnaofahamu zaidi tuambizane.
Inawezekana yeye anawaona wengi kumbe ndio hao hao sie tunawaona wachache!
 
Tuandike comments za kujenga maana JUKWAA hili viongozi wanasoma sana!!!!!!!!

Mwambie awafukuze Mwigulu na Makamba ni chanzo Cha Yeye kususiwa na wananchi.
Baada ya awamu ya kwanza ya Kikwete wananchi wengi wanaokwenda kwenye mikutano ya kiserikali wanavutwa yeye si wa kwanza. Kwa Magufuli walikuwa wanasombwa kwa malori kupelekwa wilayani.
 
Back
Top Bottom