Kwanini watu wanachukia sana Ugali. Kwani ugali una kosa gani jamani?, Wanasayansi njoeni basi mtupe Elimu

Kwanini watu wanachukia sana Ugali. Kwani ugali una kosa gani jamani?, Wanasayansi njoeni basi mtupe Elimu

Ugali wa dona una viritubisho vingi vya protein. Huu ni mzuri sana.

Tatizo ukikoboa unaondoa protein yote unabakisha wanga tu, usio na virutubisho. Ni nishati tu isiyo na virutubisho.

Na Watanzania wengi wanakula ugali wa kukoboa.
Cha kushangaza,

Nilivyoanza kuishi morogoro na dar es salaam, nilishangaa sana watu kudharau dona na kusema ni chakula cha masikini. Eti dona inanenepesha.

Halafu ni kama ugali unachukiwa zaidi huku dar es salaam kuliko mikoani.
 
Ugali unadumaza akili ndo mana Africa hatunaga akili. Je akili ni nn? ukitoa kile ulichofundishwa kinachobaki kichwani mwako ndo akili. Ndo mana hatuna ubunifu kama wazungu kila kitu tunasubiri wazungu wabuni kisha na ss tutumie. Mfano kadhaa ni cm, gari, meli, ndege, na vitu vngine kibao
Ulifanya utafiti, au una backup yeyote ya utafiti?
 
ugali mbona mtamu ukipata mboga nzuri?

nakumbuka shule waliluwa wananiita mr bean kwa jinsi nilivyokuwa nafakamia ugali maharage

na sijawahi tena kula ugali maharage mtamu kuliko ule wa pale tengeru boys sekondari

#ugalimenukali
Ugali ni chakula cha matatizo,ndio maana mkiwa mnaula mpaka mvue mashati utafikiri mnachimba shimo kwa Jembe.
 

Wadau habari ya Jioni,

kwani ugali una shida gani, mimi
nilijua ni hapa tu jamiiforum kumbe hata majumbani kwa watu.

Mimi ni mzanaki wa pale Kyabakari mbona kule kwetu tunakula ule ugali wa mtama na tupo fresh tu.

Tena ukila ugali wa mchanganyiko wa udaga na mtama alafu mboga yako ikawa kuku wa kienyeji jogoo ukalipika chuku chuku mbona tunakuwa tupo strong tu, kimwili na kiakili.

Watanzania tuachane na mambo ya kuzungu, Kama unapenda ugali basi dondosha comment yako kwa aina ya ugali unaopikwa kwenye kabila lako.

Nawasilisha;
Muulize Rayns
 
Back
Top Bottom