Evelyn Salt
JF-Expert Member
- Jan 5, 2012
- 70,916
- 141,437
Tunakula tu matumbo yajae ila ugali hapana, chakula gani hakiliki bila mboga?!! Ndizi, viazi, mihogo wali vinapanda tu inakuja ugali sasa...Ni chakula kizuri tu mkuu usifatishe Sana mitandao.
Swala la akili na kula ugali havina uhusiano kabisa.
Cha kushangaza,Ugali wa dona una viritubisho vingi vya protein. Huu ni mzuri sana.
Tatizo ukikoboa unaondoa protein yote unabakisha wanga tu, usio na virutubisho. Ni nishati tu isiyo na virutubisho.
Na Watanzania wengi wanakula ugali wa kukoboa.
Mbwa ukimpa ugali anakula tu huku anakuangalia jicho flani la dharau......tofauti na ukimpa minyama nyamaHuwa nikiona mbwa na kuku wanavyoukwepa nabak kucheka tu,tunazidiwa akili na kuku
Wakaka wanapiga ugali mzuri hawakai kihasara hasara...Kumbe umesoma tengeru boys
Enzi hizo tulikuwa tunawaona wakaka wa pale ni mahandsome tunaawashindanisha na wakaka wa ilboru 🤣
Ugali uupige na nyamachoma, ndimu na kachumbari ya kwenda.Ila ugali bwana una mboga zake
Ukila ugali maharage lazima uuchukie ugali
Kuku wanakula ugali.Huwa nikiona mbwa na kuku wanavyoukwepa nabak kucheka tu,tunazidiwa akili na kuku
Ulifanya utafiti, au una backup yeyote ya utafiti?Ugali unadumaza akili ndo mana Africa hatunaga akili. Je akili ni nn? ukitoa kile ulichofundishwa kinachobaki kichwani mwako ndo akili. Ndo mana hatuna ubunifu kama wazungu kila kitu tunasubiri wazungu wabuni kisha na ss tutumie. Mfano kadhaa ni cm, gari, meli, ndege, na vitu vngine kibao
Una mawazo kama yanguNyumbani nimekula ugali saana, bado shule nikala ugali saana sasa najitegemea kwakweli ugali utanisamehe nishaula mno.
Mbwa ukimpa ugali anakula tu huku anakuangalia jicho flani la dharau......tofauti na ukimpa minyama nyama
Wanakula pale wanapokosa kabisa chakula wanachokipendaKuku wanakula ugali.
Kuku wa kienyeji anaejua kujitafutia anakula ugali.
Mbwa koko aliyepigika akiona kesho haifiki ugali anagonga mbona.
Ugali ni chakula cha matatizo,ndio maana mkiwa mnaula mpaka mvue mashati utafikiri mnachimba shimo kwa Jembe.ugali mbona mtamu ukipata mboga nzuri?
nakumbuka shule waliluwa wananiita mr bean kwa jinsi nilivyokuwa nafakamia ugali maharage
na sijawahi tena kula ugali maharage mtamu kuliko ule wa pale tengeru boys sekondari
#ugalimenukali
Hahahahaaaa,eti tunawachanganyia ugali na mchuziMbwa ukimpa ugali anakula tu huku anakuangalia jicho flani la dharau......tofauti na ukimpa minyama nyama
NaaamUgali uupige na nyamachoma, ndimu na kachumbari ya kwenda.
Ugali ule na kambale alioungwa na nazi 🤣
Ugali na kitimoto rosti acha kabisa.
Ss Africa tuna nn zaidi ya siasa zetu za maji taka na uchu wa madaraka +ubunifu zero akili za ovyo kutaka kumtawala maskini hata kidogo alicho nacho unataka kumnyang'anyaUlifanya utafiti, au una backup yeyote ya utafiti?
Muulize Rayns
Wadau habari ya Jioni,
kwani ugali una shida gani, mimi
nilijua ni hapa tu jamiiforum kumbe hata majumbani kwa watu.
Mimi ni mzanaki wa pale Kyabakari mbona kule kwetu tunakula ule ugali wa mtama na tupo fresh tu.
Tena ukila ugali wa mchanganyiko wa udaga na mtama alafu mboga yako ikawa kuku wa kienyeji jogoo ukalipika chuku chuku mbona tunakuwa tupo strong tu, kimwili na kiakili.
Watanzania tuachane na mambo ya kuzungu, Kama unapenda ugali basi dondosha comment yako kwa aina ya ugali unaopikwa kwenye kabila lako.
Nawasilisha;