Kwanini watu wanaogopa sana kuiba umeme wa TANESCO kuliko maji ya DAWASCO?

duuh noma sana ajira nje nje
 
We nilishakuambiaga, ukitaka kujadili na mimi acha kuongea kama roboti au computer programme, ongea kama binadamu mwenye utashi. Sio ku-copy na kupaste majibu
 
Nilishawai kuiba umeme miaka miwili mfululizo kwenye mita ya luku. Japo ilikuwa inakera kwa zile kelele za kukujulisha unit zimeisha, lakini umeme haukatiki! Kwa sasa wameshtuka wanaweka mita juu ya nguzo'
 
Nilishawai kuiba umeme miaka miwili mfululizo kwenye mita ya luku. Japo ilikuwa inakera kwa zile kelele za kukujulisha unit zimeisha, lakini umeme haukatiki! Kwa sasa wameshtuka wanaweka mita juu ya nguzo'
Tunashukuru kukiri kosa tafadhali lipia kiasi husika kwa kujisalimisha TANESCO kwa kuwa hakuna mwizi anayeweza kukimbia mifumo yetu ipo imara.
 
Tunashukuru kukiri kosa tafadhali lipia kiasi husika kwa kujisalimisha TANESCO kwa kuwa hakuna mwizi anayeweza kukimbia mifumo yetu ipo imara.
Hahahahaha, we jamaa acha mikwara, utampatia wapi, labda atufundishe wanaibaje huo umeme? Si tumeambiwa kila mtu ale kwa urefu wa kamba yake 😂😂😂😂😀
 
Hivi kinachofanya watu waogope kiasi hiki kuiba umeme ni nini hasa? Mbona mitaani wanakata mabomba ya maji na ku-bypass bila uwoga?
Unaweza kunywa maji, kuogea, kunawa mikono, ila umeme kuusogelea tu, sio salama, mbali na kuwa kufanya yote hayo ni wizi.
 
Anaetaka kuunganishiwa umeme kwa kuiba units ani PM. Utalipa elfu 2 tu kwa mwezi kwenda kwenye mita yako ya umeme na mfumo wa tanesco hauta detect depletion ya Luku hivyo tumia uwezavyo. NB kununua umeme wa elf 2 kwa mwezi ni lazima ili kuwa deceive TANESCI kuwa ni mnunuaji wa umeme.
Njia hii ni salama na ni bora Kwani Tanesco watajua shida ipo kwenye mita yao. Na ukibadilishiwa mita zoezi zima litakuwa limekufa by Kitengo cha Mchongo na connection
 
Gusa unase , gusa unase , gusa unase, tutururuu, tururu, gusa unase🤸
 
Kwa majibu haya, mwizi mwenzio FRANCIS DA DON sidhani kama atakuwa na swali jingine
 
mimi ni muathirika wa vyote ...duuuu....ila kwa sasa nimeacha kabisa na sitaki tena.....nimeuiba umeme sana....ila dealer ni tanesco wenyewe...ila kwenye maji ni bypass za kutosha.........imebidi niache watoto wakuwa wakubwa wasije IGA.....
 
hahahahaha mkuu mmeanza kucomment siku hizi!? jiandaeni kwa changamoto za watanzania angalia tu usiitupe simu ya ofisi kupitia dirishani hapo makao makuu..
 
Tunashukuru kukiri kosa tafadhali lipia kiasi husika kwa kujisalimisha TANESCO kwa kuwa hakuna mwizi anayeweza kukimbia mifumo yetu ipo imara.
Wee bwana robot hivi unataka kusema hujawai kujichanganya,ukapita baadhi ya nyuzi ukakuta mada imekunogea basi ukajitoa ufahamu ukashusha coment bila kujua id uliyonayo vp haijawai kukutokea hiyi maana ule uzi pendwa bila kuacha komment si kitu rahisi
 
Wee bwana robot hivi unataka kusema hujawai kujichanganya,ukapita baadhi ya nyuzi ukakuta mada imekunogea basi ukajisajosahau ukashusha coment bila kujua id uliyonayo vp haijawai kukutokea hiyi
Hakuna robot anayeweza kujibu kama tunavyojibu, tunawasihi kudhamini na kujali kazi nzuri tunayofanya.Tumekuwa active muda wote kitu ambacho wapo wanaona mafanufaa ya sisi kuwa hapa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…