Kwanini watu wanapata shida na dhiki duniani, Mungu hana huruma?

Kwanini watu wanapata shida na dhiki duniani, Mungu hana huruma?

Shida mateso ni matokeo ya dhambi ukiishi kwa kufuata kanuni na mipango ya Mungu vyote kwako ni historia
Unaposema shida na mateso ni matokeo ya dhambi,

Unataka kuniambia yale makanisa na misikiti inayobomoka kwenye matetemeko,
Wale watu wanaokufa wote kwenye majanga kama Tsunami na matetemeko hawamtumainii Mungu?

Unataka kusema Wale wasabato wakitoka kumuimbia huyo huyo Mungu, at the same day wakiwa njiani wanapata ajali wanakufa na wengine wanabaki na makovu na ulemavu wa kudumu, hao hawamtumanii Mungu?
 
10% ni kubwa sana, ungepewa tu 1% ya nguvu za MUNGU ambazo ndani yake ni pamoja na kuona yajayo pamoja na kuweza kuona siri za wanadamu katika fikra zao nakuhakikishia ungekuwa umeshateketeza nusu na robo ya population ya huu ulimwengu wa wanadamu.

Nitakupa mifano kadhaa kuliezea hili.

Mfano wa kwanza, hebu mfikirie mtu yoyote katili unayemjua wewe ambaye siku ulipojua matendo yake ukatetemeka kwa hasira na jazba ukajiapiza kama wangekupa nafasi ya kumuadhibu basi ungemkatakata vipande na nyama yake ulishe mbwa wako ili ujiridhishe kuwa na yeye alikufa kwa mateso.

Sasa basi, wazia MUNGU amekupea nguvu zake za kujua mabaya na mema ya watu kabla hawajatenga, halafu akakurudisha siku za utotoni za huyu mtu akiwa kichanga, akakuachia maamuzi, je utaweza dhuru kitoto kichanga vile kikiwa hakina hatia ili uje uokoe wale wahanga wa ukatili utakao kuja fanywa na hiki kichanga kitakapokuwa mtu mzima, unaweza ua kichanga kwa msukumo wa hasira, ni vipi nikikwambia kila mtu mbaya leo aliwahi kuwa kichanga once na alitetewa na kulindwa kwa upendo ndio maana amekuwa mtu mzima ila still akawa katili?!

Mfano wa pili, MUNGU amekupea hizo power, huyo unayemuona ni masikini au fukara akiteseka hapo, ni kanuni za asili zimeamua iwe hivyo, na MUNGU ndie asili yenyewe sasa ya ulimwengu.

Imagine hiyo mtu unaamua sasa kumpa utajiri anaanza kuimarika na kuwa vema kifedha, ila sasa anakuja kuwa na vitu vifuatavyo, anakuja kuwa anatumikisha kingono watoto, anauwa watu kwa hila ili kufanikisha mambo yake, ananyanyasa masikini, anadhurumu wajane, anatumia pesa kudhurumu haki za wengine na kadhalika, je hautajutia maamuzi yako?!

Maisha ni fumbo kubwa sana ila inatakiwa kutumia akili kidogo sana kuelewa maudhui yake na kwann tunaishi hivi tunavyoishi. Kwakifupi mambo yapo sawa sawa ila hatujui.

Mfano unaweza jiuliza kwann watanzania wanateseka sana na kupitia dhuruma kubwa sana kiasi hiki hadi maisha yao ni magumu hivi, why asitokee mtu apambane na hawa wanaowafanyia hila kiasi hiki, then unakuja kugundua kuwa CCM wao ndio wanaiweka na akitokea mtu anataka kuitoa wao wanaitetea tena [emoji23][emoji23][emoji23] yaani Stockholm Syndrome Politics. [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kuna mtu anavuta pumzi ya bure huku anaandika Mungu hayupo...
Hakuna anayetoza kodi hiyo pumzi, wala hayupo anayeimiliki.

Kwahiyo Pumzi inamilikiwa na mwenye nayo ambae ni mtu mwenyewe, nkiamua hapa nijitolee pumzi nafanya mwenyewe tu.

Unaweza kupinga hayo madai ya hao unaodai wanavuta pumzi ya bure halafu wanaoandika Mungu hayupo?
 
Unaposema shida na mateso ni matokeo ya dhambi,

Unataka kuniambia yale makanisa na misikiti inayobomoka kwenye matetemeko,
Wale watu wanaokufa wote kwenye majanga kama Tsunami na matetemeko hawamtumainii Mungu?

Unataka kusema Wale wasabato wakitoka kumuimbia huyo huyo Mungu, at the same day wakiwa njiani wanapata ajali wanakufa na wengine wanabaki na makovu na ulemavu wa kudumu, hao hawamtumanii Mungu?
Wangemtumainia Mungu hangewaepusha na ajali.
Dini nje ndani shetani
 
Mtu anapozaliwa kiziwi na kipofu sometimes plus na ukiwete. Ni matendo yake akiwa tumboni?
If no.
Je, una uhakika wewe uliyezaa watoto wasio walemavu u mtakatifu kuliko wazazi wa watoto walemavu?
Asee unajibu kwa akili kubwa🙏👍
 
Kumbukumbu la Torati 15:7‭-‬11
Kama akiwapo mtu maskini pamoja nawe, nduguzo mmojawapo, ndani ya malango yako mojawapo, katika nchi yako akupayo BWANA, Mungu wako, usifanye moyo wako kuwa mgumu, wala usimfumbie mkono wako nduguyo maskini; lakini mfumbulie mkono wako kwa kweli, umkopeshe kwa kweli yatoshayo haja yake katika ahitajiayo. Jitunze, msiwe na neno lisilofaa moyoni mwako, kusema, Umekaribia mwaka wa saba, mwaka wa maachilio; jicho lako likawa ovu juu ya nduguyo usimpe kitu; naye akamlilia BWANA juu yako, ikawa ni dhambi kwako. Mpe kwa kweli, wala moyo wako usisikitike utakapompa; kwa kuwa atakubarikia BWANA, Mungu wako, kwa neno hili katika kazi yako yote, na katika kila utakalotia mkono wako. Kwa maana maskini hawatakoma katika nchi milele; ndipo ninakuamuru na kukuambia, Mfumbulie kwa kweli mkono wako nduguyo, mhitaji wako, maskini wako, katika nchi yako.
 
Kifo ni uamuzi wangu??
You ain't sreous

Kifo na uzima ni uamuzi wa MTU.
Wewe ndio haupo Serious na kama hujui Jambo hilo basi bado ni mdogo haujakua.
Maana mpaka Wanyama wanalijua Hilo.

Ukitaka Kufa unakufa hata sasa hivi,
Ukishazaliwa na ukakua kifo na uzima ni maamuzi yako tuu.

Nenda porini au angalia filamu za wanyama utaelewa ni Kwa kifupi kifo na uzima ni maamuzi.
Ndio maana kuna sheria, ndio maana unasikia njaa lakini unauamuzi wa Kula au usile.
 
Imagine hiyo mtu unaamua sasa kumpa utajiri anaanza kuimarika na kuwa vema kifedha, ila sasa anakuja kuwa na vitu vifuatavyo, anakuja kuwa anatumikisha kingono watoto, anauwa watu kwa hila ili kufanikisha mambo yake, ananyanyasa masikini, anadhurumu wajane, anatumia pesa kudhurumu haki za wengine na kadhalika, je hautajutia maamuzi yako?!

Sasa basi, wazia MUNGU amekupea nguvu zake za kujua mabaya na mema ya watu kabla hawajatenga, halafu akakurudisha siku za utotoni za huyu mtu akiwa kichanga, akakuachia maamuzi, je utaweza dhuru kitoto kichanga vile kikiwa hakina hatia ili uje uokoe wale wahanga wa ukatili utakao kuja fanywa na hiki kichanga kitakapokuwa mtu mzima, unaweza ua kichanga kwa msukumo wa hasira, ni vipi nikikwambia kila mtu mbaya leo aliwahi kuwa kichanga once na alitetewa na kulindwa kwa upendo ndio maana amekuwa mtu mzima ila still akawa katili
Huyo Mungu unayemtetea hapa hayupo kwenye uhalisia, labda kama tu unabisha.

Kwasababu kama kweli angekuwepo na anauwezo wa kujua ya baadae kwa kile kiumbe amekitengeneza mwenyewe asingeweza kumuumba shetani kama kitabu chako kinavyokufunza.

Mungu mjuzi wa yote, Mungu muweza wa yote na mwenye upendo wote inawezekana vipi akaumba ulimwengu huu tunaouona wenye mabaya kuwezekana?
 
Imeandikwa:
Isa 1:19
Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi
Kwa lugha nyingine unasema asilimiaa 98% ya watu wasiokula mema hawajmkubali?

Kwanini waumini ni mafukara waliojaa njaa ila wachungaji wanaendelea na maisha yao?

Kwa nini maskini anayesali na kufuata taratibu zote bado hatoboi kwa tajiri asiyesali wala kumuamini Mungu/Shetani?

Kwanini walokole mmekubuhu kwenye dhambi kuzidi watu wasio okoka?
 
Wanadamu ndio wanachagua Maisha. Kasome Jiografia utajifunza Factors zinazopelekea Watu kuanzisha Maisha na makazi katika sehemu Fulani. Ila yote ni uchaguzi.
Mkuu umeandika mambo mengi sana kujaribu kumnasua Mungu wako ambae hayupo, na hawezi kujinasua kwenye hii mitego.

Hyo elimu unayoisema ni zao la baadae sana baada ya watu kujifunza kuhusu matetemeko,

Je kabla ya elimu hii ya tetemeko kwanini Mungu hakuwajulisha kwa kuwapa allert msiishi maeneo hayo?

Na kama anaupendo wote kwanini ameweka tetemeko, tetemeko ni la kazi gani yeye sasa kuliweka?

Huwezi ishi Jangwani au sehemu yenye matetemeko(iliyopitiwa na blonde la Ufa, au lenye Plate movements Kwa Chini) alafu siku tetemeko kilitokea mkifa useme hukuchagua.
Huwezi ishi eneo la mabondeni kama Pale Jangwani alafu yatokee mafuriko Watu wafe(mfe) alafu useme haukupenda.

Huwezi amua ishi maeneo yenye Tufani na vimbunga vya baharini alafu siku tsunami ikitokea useme Mungu kawaadhibu.
Huwezi ishi sehemu yenye Mvua chache au yenye ujangwa alafu useme Mungu anataka mfe na Njaa. Utakuwa punguani wa mwisho Kabisa
Hapo ni unajitetea tu, na hoja yako haina mashiko.
Kama mungu ameyaumba yote hayo, kwanini hajawapa nauli watu wahame wasiishi hayo maeneo yenye matetemeko kama unavyodai.

Huoni wale watoto wasio ma uwezo wa kujiamlia kuhama maeneo hayo, wakikumbwa na matetemeko utasema wamechagua?
Watoto walichagua kuzaliwa hayo maeneo.
Bado haujanielewa?
Sijakuelewa na hoja yako haina mashiko.

Sasa nijibu hapa chini nikubali kama kweli mabaya ni uchaguzi, 👇👇

Vipo visa vya vimondo kuua watu ni pamoja na tukio la meteoriti lililotokea mnamo mwaka 2013 huko Chelyabinsk, Urusi. Kimondo kilichoingia angani kilipasuka juu ya mji huo, kusababisha vioo vingi kuvunjika na watu wengi kujeruhiwa kutokana na vipande vya vioo.

Moja ya visa maarufu ni lile la Tunguska huko Siberia, Urusi mnamo tarehe 30 Juni 1908. Kimondo kikubwa sana kilipasuka angani na kusababisha mlipuko mkubwa,

Je hapa unasemaje kuhusu dhana yako ya uchaguzi?
 
Mkuu umeandika mambo mengi sana kujaribu kumnasua Mungu wako ambae hayupo, na hawezi kujinasua kwenye hii mitego.

Hyo elimu unayoisema ni zao la baadae sana baada ya watu kujifunza kuhusu matetemeko,

Je kabla ya elimu hii ya tetemeko kwanini Mungu hakuwajulisha kwa kuwapa allert msiishi maeneo hayo?

Na kama anaupendo wote kwanini ameweka tetemeko, tetemeko ni la kazi gani yeye sasa kuliweka?


Hapo ni unajitetea tu, na hoja yako haina mashiko.
Kama mungu ameyaumba yote hayo, kwanini hajawapa nauli watu wahame wasiishi hayo maeneo yenye matetemeko kama unavyodai.

Huoni wale watoto wasio ma uwezo wa kujiamlia kuhama maeneo hayo, wakikumbwa na matetemeko utasema wamechagua?
Watoto walichagua kuzaliwa hayo maeneo.

Sijakuelewa na hoja yako haina mashiko.

Sasa nijibu hapa chini nikubali kama kweli mabaya ni uchaguzi, 👇👇

Vipo visa vya vimondo kuua watu ni pamoja na tukio la meteoriti lililotokea mnamo mwaka 2013 huko Chelyabinsk, Urusi. Kimondo kilichoingia angani kilipasuka juu ya mji huo, kusababisha vioo vingi kuvunjika na watu wengi kujeruhiwa kutokana na vipande vya vioo.

Moja ya visa maarufu ni lile la Tunguska huko Siberia, Urusi mnamo tarehe 30 Juni 1908. Kimondo kikubwa sana kilipasuka angani na kusababisha mlipuko mkubwa,

Je hapa unasemaje kuhusu dhana yako ya uchaguzi?

Aliyekuambia Elimu ya Jiografia ni Elimu ya baadaye ni Nani?

Kasome Geomorphology ndio utajua kazi ya matetemeko, volcano, tsunami n.k. katika huu Ulimwengu. Uache ujinga na umbumbumbu kwenye mambo usiyoyajua.

Unafikiri pasipo volcano(ambayo pia husababisha tetemeko la Ardhi) milima Kama mlima Kilimanjaro ungekuwepo?
Visiwa vingekuwepo?

Hii Dunia kuna michakato inaendelea kama vile mwilini mwako mifumo ya mwili unavyofanya kazi.
Sasa Kwa vile hujui ukisemacho, basi tunasema sio kosa lako.

Ila elewa kila kinachotokea kwenye Dunia kinafanya kazi Fulani ambayo ni muhimu katika mustakabali wa Ulimwengu.
 
Kule kumtaja kwa jina tu "Mungu" tayari umekiri uwepo wake. Kisichokuwepo hakiwezi kuwa na jina!
Spider man yupo.

Kwahiyo kulitaja jina spiderman nmekiri kuwa yupo?
 
Back
Top Bottom