Kwanini Yesu anaitwa Mungu? Sababu na ushahidi huu hapa

Shalom Mtumishi.

Yesu siyo Mungu maana yeye mwenyewe ana Mungu. Kwenye Yohana 20:17 anasema hivyo.

Yesu akamwambia, “Usinishike; sijaenda bado juu kwa Baba. Lakini nenda kwa ndugu zangu uwaambie: Naenda juu kwa Baba yangu na Baba yenu, Mungu wangu na Mungu wenu.”

Andiko la Yohana 1:1 limepotoshwa. Maneno Mungu yaliyoandikwa mara mbili hayamaanishi kitu kimoja. Biblia enzi hizo iliandikwa kwa Kigiriki. Ukiangalia andiko hilo kwa kigiriki utaona tofauti ya Mungu hizo. Mungu moja in V mwishoni na nyingine ina S. Hiyo ya pili inamaanisha yesu alikuwa na sifa za kimungu, na siyo kwamba alikuwa Mungu.



Yesu hajilinganishi na Mungu. Huko juu alisema naenda kwa baba yangu na baba yenu, Mungu wangu na Mungu wenu. Hapa chini anakazia kuwa huyo baba ni mkuu kuliko yeye. Na kuwa hawako sawa.

Yohana 14 28

Mlisikia ya kwamba mimi niliwaambia, Naenda zangu, tena naja kwenu. Kama mngalinipenda, mngalifurahi kwa sababu naenda kwa Baba, kwa maana Baba ni mkuu kuliko mimi.
 
Mungu nae anaomba?
Luka 6:12 .

Siku moja Yesu alikwenda milimani kuomba, akakesha usiku kucha akimwomba Mungu.
Kwanza kabla cjakujibu naomba ujibu hili swali kwanza ili uelewe kwa upana . Mungu ninani? Na kuabudu ni kufanyaje?
 
Yesu ni Mungu kwasababu yeye ndie mwana pekee wa Mungu na sio Mungu baba
 
Mimi huwa naamini yesu Ni Mungu lkn hawezi kuwa Mungu baba Bali Ni Mungu kwa kuwa alituumba sisi na yeye aliumbwa na Mungu baba.
 
Yesu anaitwa mwana pekee sababu alikuwa ndiyo wa kwanza kuumbwa. Ila Mungu ana wana wengi wengi.
Nimekuuliza Mungu ninani? Na kuabudu ni kufanya nini? Ukiweze kupata jibu hilo kila kitu kwako ni sawa
 

Nafikiri ume eleza vizuri japo ili hoja ikamilike ni lazima iwe na upande wa pili.
Na kwa sababu huku uandika; mimi nakusaidie kwa kifupi tu ikwa wale wanao sema Yesu sio Mungu;

1. Yesu amezaliwa na binadamu japo kwa miujiza kama vile Adam na Hawa walivyo patikana kwa miujiza
2. Yesu analala usingizi ina maana kuna nyakati watu hawakuweza kuwasiliana na Yesu kipindi akiwa usingizini, hivyo kupelekea wasubiri hadi atakapo amka.
3. Mara kwa mara alikuwa anasali na kuomba sana (inaonesha yupo mwingine mwenye nguvu kuliko yeye) aluiyekuwa anamuomba ili aweze kutimiza miujiza.
4. Ukisoma vizuri hasa biblia ambazo hazijatafsiriwa zinaonesha kuwa miujiza mingi alikuwa anaifanya kwa uwezo wa baba....
5. Alikuwa anakula chakula, kujisaidia nk nk
6. Alisulubishwa na binadam (Yaani, Binadamu walimkosea Mungu, wakampiga mungu hadi akafa, ili awasamehe) hata kwa mtu ambaye hajasoma anaona kuna kitu hakipo sawa.

Nimalizie tu kwa kusema; Yesu sio Mungu ila alitumwa kwa kazi maalum na Mungu na kuna uwezekano Mungu aliamua kumtwaa Yesu mapema baada ya kuona watu wameamua kumuabudu yesu badala ya kumuamudu Mungu aliyemtuma
"WATU WANGU WATAKUJA KUANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA!"
 
Yesu si Mungu baba!
 
OK
 
OK sasa nijibu hapo kabla ya mwanzo(wakati)kulikuwa na nini na nani?
Maana yohana kasema hapo mwanzo maana yake ni kama Kuanza kwa jambo fulani

kuhusu kuumbwa kwa dunia hakuna sehemu kwenye biblia yako imeelezea zaidi ya vilivyomo ndani ya dunia!
 
Hapo mwanzo wa neno na mungu
je yohana alilkuwa anaongelea mwanzo wa dunia?
au "neno" maana yake ni dunia?
Anazungumzia mfumo wa kibinadamu. Mfumo uliomuumba mwanadamu umefungwa na muda. Yaan lazima ili mwanadamu akuelewe lazima iwepo time. Mwanzo na mwisho lakin ukija habar za Mungu au roho zinakaa eneo lililo vast halina mwisho wala mwanzo. So Yesu hana mwanzo wala mwisho, Mungu aliitengq hiyo nafs yake kwa kazi ya uumbaji. Ni kama vile unavyoona mwili wa mwanadamu una maeneo matatu. Mwili, roho, na nafsi.
 
Ngoja niishie hapa hiz mada za kilokole ligi yake ni ndefu sana

Muda wangu wa kuvuta ganja umeshafika!
 
Nauliza ilijulikanaje kuwa huyo neno ni yesu
Mbona jibu tayari umeishapewa: Amejaa Neema na Kweli. Yesu alisema Yeye Ndiye Njia na Kweli na Uzima.

Nani mwingine aliyejaa neema zaidi ya Yesu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…