Kwanini Yesu anaitwa Mungu? Sababu na ushahidi huu hapa

Kwanini Yesu anaitwa Mungu? Sababu na ushahidi huu hapa

Kama uliyeandika hapa ni mwafrika basi ni mbwa,huwezi kumuita yesu mtu kama wewe kuwa ni MUNGU,upumbavu huu unawagharimu
Musa aliona mti na moto akaanguka kifudifudi na huo mti wenye moto ukasema mimi ni Mungu wa baba zako Ibrahim na isaka na yakobo ....sasa kati ya wanadamu na mti nikipi bora ? ...je kati ya mwanadamu na moto kipi bora ? ...sasa kama mungu alijigeuza mti uwakao moto na mtume musa akamsujudia unasemaje ni haramu mungu kujigeuza mwanadamu.. KUMBUKA BINADAMU NI MBORA WA VIUMBE KULIKO MITI NA MOTO
 
Labda ni kwenu tu lakini kwetu wanakufa.
Kwa hiyo labda kwenu huko ni miungu
Akili zako ni ndogo je watakatifu baada ya kiama wanakufa ? Hivyo kutokufa kwa kiumbe ni fadhiri za mungu tu kama ilivyo kwa kufa
 
Hapo Tito2:13 Mungu Mkuu ni Baba siyo Yesu Kristo Mwanawe.
Isipokuwa huwezi kumtenga Mungu na Neno lake,Yesu Kristo ni Neno la Mungu,
Yohana17:3
Hii haimainishi kuwa Yesu Kristo siyo Mungu! Hapana! Yesu Kristo ni Mungu kwa sababu amezaliwa na Baba (Mungu Mkuu)
 
Neno mungu katika maandiko linarejerea mtu au kitu chenye nguvu 2 wakorintho 4:4 kwa hiyo ukisema yesu ni mungu maana yake ana nguvu ila si za kumzidi baba yake (yehova) kwahyo kwa maneno mengine uungu/mungu ni majina ya cheo tu.
 
Hiyo injili unayotumia iliandikwa na waroma ikapitiwa karne kadhaa mbele na king james, original version haiongei huo upuuzi.
 
Katika injili ukisikia Yesu anasema "MWANA" maana yake mwili wake....na unapo sikia anasema "BABA" umaanisha nafsi yake ambayo ndiyo MUNGU MWENYEZI.
Yesu akawaambia wanafunzi wake 👉hata 'mwana' ajui siku ya kiama ila 'baba' ....maana yake kuwa Yeye yesu anajua siku yakiama ila wanafunzi wake wakadhani ana maanisha yeye ajui...waka acha kumsumbua kumuuliza.
Wewe ni mtoto wa Babaako huwezi kuwa Babaako japo mnaweza kulandana tabia au kufanana sura.
 
1. Ushahidi wa Kibiblia
Yohana 1:1 – "Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu."
Tito 2:13 – "Tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Mungu mkuu na Mwokozi wetu Yesu Kristo."

Yesu mwenyewe alikiri kuwa ni Mungu:
Yohana 10:30 – "Mimi na Baba tu umoja."
Yohana 8:58 – "Amini, amini, nawaambia, Kabla Abrahamu hajakuwako, Mimi niko."

2. Sifa za Kimungu alizo nazo Yesu
Uwepo wake wa milele – Mika 5:2
Uwezo wa kusamehe dhambi – Marko 2:5-7
Uwezo wa kutoa uzima wa milele – Yohana 10:28
Uwezo wa kuhukumu ulimwengu – 2 Wakorintho 5:10

3. Miujiza inayodhihirisha Uungu wa Yesu
Kubadili maji kuwa divai (Yohana 2:1-11) –
Kutembea juu ya maji (Mathayo 14:25-27)
Kutuliza dhoruba (Marko 4:39)
Kufufua wafu (Yohana 11:43-44)
Kupaa mbinguni (Matendo 1:9-11)

4. Unabii wa Agano la Kale ulitimia kuhusu Uungu wa Yesu
Katika Isaya 9:6 – Yesu anaitwa "Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele."
Katika Mathayo 1:22-23, tunasoma jinsi unabii huo ulivyotimia:
"Hayo yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa njia ya nabii, akisema, Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, Naye watamwita jina lake Imanueli; yaani, Mungu pamoja nasi."

5. Watu Walimwabudu Yesu na kukiri kuwa ni Mungu
Mathayo 28:9,17 – Wanafunzi wake walimsujudia.
Yohana 20:28 – Tomaso akajibu, akamwambia, Bwana wangu na Mungu wangu! Yesu alipoambiwa na Tomaso kuwa ni Mungu, hakukanusha.

Kama unadai Yesu sio Mungu, toa sababu zako hapa
Wanaompinga wanaipinga biblia halafu unatetea hoja kwa kutumia biblia. Sijui mnakuwaga na akili gani
 
Wewe ni mtoto wa Babaako huwezi kuwa Babaako japo mnaweza kulandana tabia au kufanana sura.
Mbinguni kuna wafalme wangapi? .... sasa kwanini yesu alimjibu kaisari kuwa ufalme wake siyo wa dunia hii ...tumia akili wewe zuzu wa makanisani
 
Back
Top Bottom