Kware: Ufugaji bora wa Kware, Na faida ya bidhaa zitokanazo na Kware

Kware: Ufugaji bora wa Kware, Na faida ya bidhaa zitokanazo na Kware

Jamani Nahitaji Kufanya Ufugaji Wa Kwale, Lakini Sina Uzoefu Wowote Kuhusu Ufugaji Wa Kwale, Kwa Hiyo Anayefahamu Vizuri Naomba Anijuze 0719044015 NIPO MBEYA
 
Jamani Nahitaji Kufanya Ufugaji Wa Kwale, Lakini Sina Uzoefu Wowote Kuhusu Ufugaji Wa Kwale, Kwa Hiyo Anayefahamu Vizuri Naomba Anijuze 0719044015 NIPO MBEYA

Mkuu kwenye thread hii hapo juu kuna maelezo ya awali ya ufugaji kwale kama utakuwa na swali au unahitaji ufafanuzi zaidi usisite kuwasiliana nasi kwa namba 0654 163 784 muda wowote ule.
 
Kaka nimeona nikupe feedback, ndege wangu wanakuwa vizuri nadhani muda si mrefu nitaanza kukuuzia mayai lol
 
Hawa ndege wanasumbuliwa Sana na ugonjwa wa macho,dawa ipi nzuri?

Kaka Kwale wako wanasumbuliwa na mafua na si ugonjwa wa macho, Nenda kwenye duka la dawa za mifugo na uwaeleze kuwa kwale wako wanamafua yaliyopelekea kuvimba macho, hatua ya kuvimba macho ni hatua ya juu ya ugonjwa wa mafua na hii itasababisha upungufu katika kutaga, tegemea kukusanya mayai machache kwa muda huu.

Kinga: Jitahidi sana usichanganye kwale wako na mifugo wengine na waepushe kwale wako na Vumbi, mara nyingine vumbi hutokea kwenye chakula (chick mash), jitahidi kisitoe vumbi pindi unapowawekea kwenye vyombo vyao vya chakula.

NOTE: Dawa za mafua ziko nyingi chukua dawa za Holland na ile ya poda na si maji.
 
Mimi niwajuavyo kwale ni ndege wa porini na nishawahi kuwala sana kwa kwatega shambani,wako very shy na wanakimbia sana wanapoona mtu karibu,najiuliza wanakaaje bandani bila kutoroka? Na unaweza kuwaachia kama kuku wa kienyeji?
lakuongezea hapo mbona hawa ni nyara ya serkali itakuwaje ukishikwa na hawa ndege?au siku hiz ruksa kuwafuga
 
Kaka Kwale wako wanasumbuliwa na mafua na si ugonjwa wa macho, Nenda kwenye duka la dawa za mifugo na uwaeleze kuwa kwale wako wanamafua yaliyopelekea kuvimba macho, hatua ya kuvimba macho ni hatua ya juu ya ugonjwa wa mafua na hii itasababisha upungufu katika kutaga, tegemea kukusanya mayai machache kwa muda huu.

Kinga: Jitahidi sana usichanganye kwale wako na mifugo wengine na waepushe kwale wako na Vumbi, mara nyingine vumbi hutokea kwenye chakula (chick mash), jitahidi kisitoe vumbi pindi unapowawekea kwenye vyombo vyao vya chakula.

NOTE: Dawa za mafua ziko nyingi chukua dawa za Holland na ile ya poda na si maji.

Kama watakuwa bado wanakusumbua baada ya siku tano za tiba, nijulishe

Asante mkuu,ngoja nifatilie dawa.
 
Hv kitu kiko kwenye mayai ya kwale wa kufuga nyumbani ambacho kinatofautisha yai lake na la kuku?
 
Hv kitu kiko kwenye mayai ya kwale wa kufuga nyumbani ambacho kinatofautisha yai lake na la kuku?

Mayai ya KWALE yameonekana kuwa chanzo muhimu sana cha Vitamini A, B1, B2, B6, B12 na Vitamini D, chuma, kopa, magnesiamu, zinki, shaba, fosforas na virutubishi vidogovidogo vingine muhimu, madini na aside ya amino, ambayo ni sababu mayai haya hupendekeza kwa ajili ya matumizi ya mara kwa mara ya binadamu. Mayai ya KWALE yamejulikana kuwa bidhaa bora ya tiba za asili
 
Ni muda gani yai la kware linaweza kukaa kabla ya kuanza kuharibika likiwa halipo kwenye friji?
 
Kama watakuwa bado wanakusumbua baada ya siku tano za tiba, nijulishe

nilivutiwa sana na huu mjadal wa kware na nimeanza kuwafuga wapo poa na afya tere hofu yangu ni soko la mayai yk ninaanzia wapi sijui nitayauza wapi kwani waru wengi wajui hiki kitu napata wacwac sana nisaidieni..
 
nilivutiwa sana na huu mjadal wa kware na nimeanza kuwafuga wapo poa na afya tere hofu yangu ni soko la mayai yk ninaanzia wapi sijui nitayauza wapi kwani waru wengi wajui hiki kitu napata wacwac sana nisaidieni..

Wafugaji wakubwa mara nyingi hununua mayai kwa wingi kutoka kwa wafugaji waliowauzia vifaranga, kwa kuwa wao huwa na wateja wengi wa mayai na vifaranga, kumbuka hawa wako established tayari na wameshajitanga, wanajulikana. Hata sisi hununua mayai kutoka kwa wafugaji tuliowauzia vifaranga.

Jaribu kuwasiliana nao na biashara ni matangazo jaribu hata kuongea na ndugu, jamaa na marafiki
 
Matrix scheme ni watu wachache wanaanzisha biashara yao na kuitangaza kwa kiwango cha juu kiasi ambacho watu wengi wanatamani kuingia; hivyo kusababisha mahitaji(demand) kubwa hivyo wale waliowahi wanauza sana tena kwa bei kubwa. Baada ya wafanya ile biashara kuwa wengi soko linakuwa na wauzaji wengi wateja ni wale wale, hivyo bei inashuka. Wale walioanza saa hizo wanakuwa matajiri wa kutupa na kwa wakati huu hukaa pembeni. Inawezekana bidhaa husika ni nzuri kweli au ni fake, lakini itakuwa imetangazwa vya kutosha ili kusababisha demand kubwa wakati supplier ni wachache. Mara nyingi huwa ni bidhaa mpya iliyopambwa kwa maelezo yaliyopitiliza(kwani bidhaa tulizozoea watu hawatakubali hkudanganyika kwa urahisi). Miaka ya nyuma unaweza kumbuka Aloevera, mlonge, uyoga wa Kichina n.k. Wakati mwingine sio vyakula, anaweza mtu akaenda Benki leo na kuomba sarafu nyingi za 500, baada ya kuwa na za kutosha, akaweka tangazo ananunua hizo sarafu kwa @5000; watu wakileta anawapa 5000 kweli kwa hiyo biashra inaanza hapo. Baada ya awareness kuwa kubwa, anawatafuta watu wake anawagawia zile alizokuwa nazo na chache alizonunua na kuziingiza sokoni labda atauza 2000; then anatoweka, kwa hiyo watu wa kati wanabaki nazo mkononi bila wanunuzi na yule aliyeanzisha biashra ameshatengeneza faida kubwa. Hizi link hapo chini zinaonesha kinachowatokea Wakenya sasa hivi; waliokopa benki wabalia sasa.

Hard reality as market forces shift against quail bonanza - News | Daily Nation

Quail farmers facing challenges as market saturates - Counties | Daily Nation
 
Back
Top Bottom