Kwasababu CCM wanapenda uongo na magoli ya mikono, COVID-19 haipendi uongo itawaondoa madarakani!

Kwasababu CCM wanapenda uongo na magoli ya mikono, COVID-19 haipendi uongo itawaondoa madarakani!

Halafu ana kasi ya ajabu, sijui kama ni yeye peke yake anaitumia hiyo id. Wako kazini buku saba kueneza propaganda.
Unajua mtu ambae anajiandikia tu bila kufikiri lazima awe na spidi sasa wewe unafikiri unajenga hoja unaweka facts yeye anakuja anabwabwaja na kuhamia uzi mwingine
 
Ccm iondolewe madarakani na nani?

Chadema [emoji3][emoji3][emoji3]

Vijana acheni mbege za marangu zinaharibu ubongo

Tunapoelekea itabidi atokee mwendawazimu mmoja atakaye kuwa ameumizwa na kufiwa na ndugu yake tokana na Covid-19 awe na akili za Umkhonto We Sizwe amalize Kazi...!!
 
Atakuwa amekomolewa na maabara za Wuhan
Inasikitisha kweli,yani mnaombea wenzenu wakumbwe mabaya kisa kumkomoa Magufuli? Yani chuki zenu kwa mtu mwengine ambaye mmeshindwa la kumfanya matokeo yake athari za chuki zenu wanazipata watu wengine.
 
Utaratibu wa ccm kutawala nchi yetu umekuwa ukigubikwa na usiri mwingi, uchakachuaji wa data, uongo uongo, propaganda, wasiojulikana na magoli ya mikono! Vyote hivyo ni adui namba moja pale inapokuja kwenye corona virus [emoji3083]

Hivyo ccm lazima ipoteze hata wakiwapa wanachama wao barakoa za bure badala ya kofia, t-shirts ama pilau!

Lakini kwa haya yanayoendelea, baadaye mtakuja kusema labda rais alifanya makusudi ili aendelee kutawala. Kwanza ikifika wakati wa uchaguzi hali inaweza kuwa mbaya zaidi na minamba ikawekwa kujustify uchaguzi kufutwa indefinitely. Pamoja na campaign. Pesa itasemekana zinaenda kwenye corona. Kwasababu hata sasa namba zinatolewa kwa kauli kutoka juu!

Hii corona bila shaka itaondoka na serikali nyingi sana, maana gonjwa limekuja karibia na uchaguzi mkuu hata Marekani Trump naye ka panic hivyo hivyo anasema watu wajipige sindano za bleach na pia wajianike juani watapona corona![emoji2365]

Kiongozi wa ukweli anapimwa wakati wa mgogoro kama huu. Kabla hata ya corona, huu mwaka ulikuwa wa changamoto kubwa sana kwa ccm. Sasa corona imeingia, kama hakuna hatua madhubuti, ni bora wapinzani nao waanze kuja na mawazo mbadala ya namna tutakayokabiliana na corona, maana ni wazi litakuwepo kwa muda. Lakini kwa hali hii ya sasa, tutaenda kuuzika uchumi wetu!

Kwamfano hata hao watalii tunaowategemea, wakati huko kwao kukiwa sawa, unadhani serikali zao zita recommend raia wake waje nchini? Kwasababu hao watu wanakwenda na statistics, halafu pia wanafahamu yanayoendelea. Hata ufiche vipi kwanza now days kuna satellites mnaonekana wazi tu huko makaburini hata kama ni usiku wa manane kama wananchi wanavyodai.

Mods tafadhali musiichinjie baharini hii ni angalizo tu kwa uchaguzi mkuu ujao. Wananchi wanahitaji wasikie alternative ideas. Tuuachie usambae ambayo ni mode ya “The fittest survive”, ama tuende na partial lockdowns huku tukiongeza uwezo wa kupima.

Siyo ajabu wananchi tukajazuiwa kupiga kura kama kina Pasco wamekuwa wakisema hakuna haja ya uchaguzi bali Maghufuli kisha amkabidhi Makonda.
Fikiri nje ya kisanduku.

Badala ya kuhangaisha kichwa chako nani atatawala, data za uongo, propagabda, nk (rejea bandiko lako) jiridhishe kwanza na usalama wa maisha yako.

JILINDE UMLINDE JIRANI
 
Umesema kweli mkuu, CCM ina watu wake, ni wachache tu.
Na vyama vingine vina wa kwake nao ni wachache pia.

Kinachogombewa ni hilo kundi kubwa la watu ambao ni neutral.
Kuwapata watu hao ni lazima uwe na hoja za maana, uwe na mgombea wa maana, muaminifu, mgombea muadilifu.
Mgombea ambaye ikibidi apatikane kupitia kwenye chekecheke la kidemokrasia.
Hayumkini, kwa kuwa watu wameichoka CCM uje na mgombea wa kuokota okota, ukitarajia kuzipata bure bure kura za watu hao.
Kundi linaloamua matokeo ni kundi la watu wanaojitambua, linapima mambo mengi kabla halijaamua kukupa kura ya NDIYO.
Ni ushauri tu.
Mkuu kwanini unasahau kuwa nchi hii ina watu zaidi ya milioni 55? Unadhani miaka yote watu hawa wataendelea kupelekeshwa na kikundi cha watu wasiozidi milioni kumi kinachoitwa ccm?

Wanao shiriki maigizo yenu ya uchaguzi ni wajinga wenzenu wanaccm na wanachama na mashabiki wachache wa vyama ambao jumla yao hata haifiki 20 milioni sasa tell me hawa wengine zaidi ya milioni 40 wako wapi na wanafikiria Nini kuhusu siasa uchwara mnazoendesha hapa Tanzania
 
Umesema kweli mkuu, CCM ina watu wake, ni wachache tu.
Na vyama vingine vina wa kwake nao ni wachache pia.

Kinachogombewa ni hilo kundi kubwa la watu ambao ni neutral.
Kuwapata watu hao ni lazima uwe na hoja za maana, uwe na mgombea wa maana, muaminifu, mgombea muadilifu.
Mgombea ambaye ikibidi apatikane kupitia kwenye chekecheke la kidemokrasia.
Hayumkini, kwa kuwa watu wameichoka CCM uje na mgombea wa kuokota okota, ukitarajia kuzipata bure bure kura za watu hao.
Kundi linaloamua matokeo ni kundi la watu wanaojitambua, linapima mambo mengi kabla halijaamua kukupa kura ya NDIYO.
Ni ushauri tu.
Matokeo yanatanzwa kwa kadri yalivyopokelewa toka kwa makada wa ccm ambao ni wasimamizi wa uchaguzi,sasa hilo kundi linaamuaje? Hilo kundi lingekuwa linajihusisha na siasa zenu uchwara Magufuli angepewa kura milioni 8 tu out of 20 milioni? Pamoja na wasimamizi kuwa wanachama wenu na bao la mkono juu
 
Ccm iondolewe madarakani na nani?

Chadema [emoji3][emoji3][emoji3]

Vijana acheni mbege za marangu zinaharibu ubongo
Wewe waache waendelee kujiaminisha mitandaoni kiwa Chadema itashinda 2020. Hao vijana hawafanyi hata tathmini mitaani.
 
Hatuwaombei wenzetu tunamuombea yeye binafsi ili covid impende zaidi
Ila yeye pia akiwaambia watu waombe Mungu ili hili janga la corona liondoke mnamuona analeta siasa kweye jambo la kisayansi kwamba corona haiwezi kuondoka kwa maombi,ila nyienyie tena mnaosema corona haiwezi kuondoka kwa maombi ndio mnaamini kuwa mtu anaweza kupata corona kwa maombi. Sasa nyie na Magufuli mnatofauti gani? mliomba corona ije Tz sijui mlidhani itawapata maccm tu ila mkasahau corona haichagui,sasa hivi nyie mnasema watu wanakufa serikali inaficha mara sijui Magufuli kawakimbia. Yani ni upumbavu upumbavu tu kwa aina hii ya siasa zenu,halafu bado et mnaomba corona iende chato impate Magufuli tu mshasahau tena kuwa corona haichagui.

Kwa upumbavu kama huo halafu mnalalamikia viongozi wa afrika wakati hao viongozi wanatoka kwenye jamii zetu hizihizi zenye watu wenye siasa za kuombea watu wapate corona,ndio maana mie sikumshangaa sana Polepole alivyowafananisha wapinzani na corona maana nishazoe hizi siasa zenu. Wengi mna matatizo ya akili bila kujua.
 
Watumie njia mubadala waandike proposal huko kwenye mashirika makubwa jinsi wanavokabiliana na corona, pia njia za ku boost uchumi, mbona Kuna nchi ka Msumbiji, Malawi zimefutiwa madeni na kupewa msaada wa kupambana na covid, Sasa sie tukijfanya donor country tutaumia

Sent using Jamii Forums mobile app

Tatizo sisi tunawaita washirika wetu wa maendeleo ni mambuzi dume (Ma beberu), sasa katika hali hiyo, hata kama ni wewe, utatoa msaada kweli?

Naona tupunguze tambo na kutoa kauli zenye ukakasi hadharani. mambo yetu ya chini ya kapeti yaongelewe ndani siyo hadharani
 
Waongo wengine afya zao mgogoro,wamekimbia mji. wanajua wakionjwa kidogo na corona wanakwenda na maji
Lkn hii dunia nyamaza tu

TeNda wema nenda zako usisubiri Shukrani

Huwezi amini yule aliyekuwa anasema ikifika muda flani watu watahamia vijijini kumbe yeye ndiyo kawahi huko kijiji mapemaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ingekuwa ni amri yao Ccm wangeielekeza Corona kwa wapinzani tu.....ila ndio hivyo Mungu anatenda haki! Mpaka Baba J kakimbilia chaka huko!

Sent using Jamii Forums mobile app
Baada ya mbinu zote za kuuwa upinzani kubuma hata wanajilaza kwenye mawe kwa stress za kushindwa kuuwa upinzani huku wakifikiria mbinu mpya hii corona Ingekuwa inabebeka wallahi wangeielekezea kwa upinzani.
 
Lkn hii dunia nyamaza tu

TeNda wema nenda zako usisubiri Shukrani

Huwezi amini yule aliyekuwa anasema ikifika muda flani watu watahamia vijijini kumbe yeye ndiyo kawahi huko kijiji mapemaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
Wengine waliombea wenzao wafe wakatangulia wao.
Waliosema kufika June 2017 atakaebakia mjini ni mwanaume wamekimbia wao
 
Back
Top Bottom